Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mtumishi. Majaribio ya aina hii ni unethical kwa sababu implications zake ni hatari mno. Cross-breeding, DNA crossing/splicing na uhamishaji huu wa seli za ubongo hautakiwi kuachiwa tu ufanyike kiholela. Kuna siku atatokea rogue scientist huko North Korea achanganye DNA ya simba na binadamu kwenye lab ili kuzalisha wanajeshi wasioogopa halafu atuletee matatizo. Kama binadamu hatupaswi kuingilia uumbaji wa Mungu na kuanza kuhamisha DNA hovyo hovyo lakini huko ndiko tunakoelekea kwa sababu tiba za magonjwa mengi inaonekana zimejificha katika DNA na kwa kadri siku zinavyokwenda wanasayansi wanadai itafikia mahali wataweza kuzalisha binadamu asiyeugua wala kuzeeka.

Kama leo tunaweka brain cells za binadamu kwenye ubongo wa panya, vipi tukiweka kwenye ubongo wa simba au tiger? Tunacheza na moto!
bb98d89f620e20c0df0e9692668b9e36.jpg

Upuuzi wa Wanasayansi

.......
 
Hatari sana, wataalamu wa DNA wanasema sisi binadamu tunatumia 4%tu ya DNA zetu, je 96% ziko wapi na zinatumikaje?
Hili bado ni fumbo kubwa. Wanasema kuwa siku tukiweza kusoma kila code na kuelewa kila kitu kilichomo basi si ajabu tutaweza kufumbua mafumbo yote ya maisha yetu - tumetoka wapi? Kwa nini tuko hapa? Kwa nini tunazeeka? Kwa nini huwa tunaugua? Twaweza kuishi milele? The possibilities are endless! Wanasema siri zote - ikiwemo kama kuna ndugu zetu wengine huko katika sayari na malimwengu (universes) mengine pengine zimefichwa katika DNA zetu. Ndiyo maana Genetics bado ni mojawapo ya nyanja za sayansi zinazosisimua sana tangu mlango ufunguliwe na mtawa Gregory Mendel zaidi ya miaka 120 iliyopita.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom