Werrason
JF-Expert Member
- Nov 5, 2014
- 13,226
- 39,942
Nikisomaga habari kama hizi naharibu mood.....alafu kuna mtu anajidai ananyoosha injiWakati tukiwa bado na pilikapilika za kinachoelezwa kubana matumizi, LUGUMI Enterprises iliyopewa mkataba wa kifisadi na kulipwa Tshs bilioni 34 kwa ajili ya tenda ya kuchukua alama za vidole kwenye vituo vya polisi nchini bila kufanya chochote, Tshs bilioni tano zilitumika kama mafunzo pekee. Ambapo waliopewa mafunzo hayo ni watu watano (5) huku baadhi yao wakiwa ni watendaji wakuu wa wizara ya mambo ya ndani na taasisi zake.
Aidha inadaiwa kuwa mafunzo hayo yalifanyika moja ya mataifa ya barani Ulaya huku kukiwa na ukiukwaji mkubwa wa matumizi.
Swali la kujiuliza ni kwanini hayo yafanyike huku kukiwa na ukimya kutoka serikalini?
Uchunguzi pia unabaini kuwa LUGUMI Enterprises ilipewa tenda huku ikishinikizwa kuwa na ubia na kampuni ya Infosys inayomilikiwa na waziri Charles Kitwanga pamoja na mkurugenzi mkuu mpya wa NIDA. Kwanini hayo yafanyike?
Tuelezwe kuwa Infosys na LUGUMI Enterprises waligawana asilimia ngapi kila mmoja kwenye mradi kinyume cha taratibu?
Mafunzo ya wastani wa mtu mmoja kugharamiwa Tshs bilioni moja ni ya aina gani?
Ni kwanini mkataba huo hauwasilishwi PAC kama inavyotakiwa? Nini hasa kinafichwa ufisadi ufisadi.