Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mchana mwingine tena, narejea kukupa habari fupi na muziki unaotawaliwa na gitaa kwa sababu naamini kikundi chochote cha muziki chenye gitaa, ngoma na watendakazi kinakuwa ni sehemu ya kumfanya msikilizaji afurahie maisha kwa namna yoyote ile. Iwe ni kwenye furaha au huzuni, nyuzi za gitaa kwenye muziki zitakupa amani.

Mchana huu tumwangalie Ramadhan Mtoro aka Dr Remmy Ongala (Sauti ya Mnyonge), gwiji hili la muziki, alipata umaarufu wake mkubwa duniani akifanya muziki wake nchini Tanzania.

Muziki wake aliuita 'ubongo beat' maana yake 'radha za akili
Pamoja na umaarufu wake duniani, hakuna mwanamuziki ambaye anaweza kusema anajulikana kama Dr remmy, alijulikana sehemu nyingi tanzania iwe ni vijijini au mjini, alikuwa ni 'Michael Jackson' wa Tanzania. Ni mwanamuzi aliyefanya ziara nyingi za kimuziki zilizosimamiwa na WOMAD na hii ilimfanya kutumbuiza na magwiji wakubwa kabisa wa muziki duniani

mtaalamu wa kupiga gitaa na kutunga mashairi ya kutetea haki za mtu wa chini, na kuikosoa serikali na kufariji wanaosikiza vibao vyake,Dr remmy pamoja na kifo chake, muziki wake bado unaishi.

Sikiza clip hii ya YouTube , sikiza gitaa hapo, linalosikika zaidi alipiga yeye.

''walipewa madaraka wakashindwa kuwajibika...., barabara mashimo matupu, shehe anauza bangi, padri anauza sabuni za msaada, saa mbili asubuhi foleni kwenye supu, ofisi ipo na nani...'




Shunie anza na hii kwanza

Binamu asante sana kesho naomba kipenda roho sawa
 
NUKUU YA LEO

We can not hope to solve our problems by pretending they do not exist
966f950e8ff68462a82ef1fbca69270a.jpg


Hatuwezi kutatua matatizo yrtu kwa kujidanganya hayapo
a89d77d379e0da3a1dc3c9470ed6981e.jpg

Haya maneno yalipatwa kutamkwa na Baba wa Taifa la Tanzania Hayati Mwalimu Julius kambarage Nyerere aliezaliwa 13/04/1922 huko Butiama, mkoani Mara nchini Tanganyika.

Mwalimu Nyerere alifariki tar. 14/10/1999 akiwa na miaka 77.
5d3f8b6baa18c59e16813e53efaf2d33.jpg

Nyerere anakumbukwa kwa mengi Hapa Tanzania, Africa na Dunia nzima kwa simamia haki na usawa kwa watu wote..

Hayo maneno alitamka akimaanisha kukubali kuwepo kwa changamoto/matatizo ndio njia ya kuyatafutua ufumbuzi na jamaa inajua kuwa kuna changamoto kadha wa kadha za kutatuliwa.


Hili liko tofauti na Uongozi wa sasa hivi..Uongozi wa Tanzania baada ya miaka 50.

☞Sasa hivi kuna Hali ya njaa kwa wananchi ila viongozi wanadai Hakuna njaa nchini

☞Sasa hivi kuna upungufu wa Dawa hospitalini lakini Viongozi wetu wanadai kuna dawa za kutosha

☞ sasa hivi kuna changamoto ya Nishati hasa umeme na gesi ila utasikia tuna umeme wa kuuza kwa nchi jirani.


Taifa linahitaji uwazi na uwajibikaji wa kila mwananchi ili tuweze kufikia malengo yetu.


Mungu Ibariki Afrika,

Mungu Ibariki Tanzania.


Mchana mwema.
Asante shemela kwa nukuu ya leo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom