NUKUU YA LEO
We can not hope to solve our problems by pretending they do not exist
Hatuwezi kutatua matatizo yrtu kwa kujidanganya hayapo
Haya maneno yalipatwa kutamkwa na Baba wa Taifa la Tanzania Hayati Mwalimu Julius kambarage Nyerere aliezaliwa 13/04/1922 huku Butiama, mkoani Mara nchini Tanganyika.
Mwalimu Nyerere alifariki tar. 14/10/1999 akiwa na miaka 77.
Nyerere anakumbukwa kwa mengi Hapa Tanzania, Africa na Dunia nzima kwa simamia haki na usawa kwa watu wote..
Hayo maneno alitamka akimaanisha kukubali kuwepo kwa changamoto/matatizo ndio njia ya kuyatafutua ufumbuzi na jamaa inajua kuwa kuna changamoto kadha wa kadha za kutatuliwa.
Hili liko tofauti na Uongozi wa sasa hivi..Uongozi wa Tanzania baada ya miaka 50.
☞Sasa hivi kuna
Hali ya njaa kwa wananchi ila viongozi wanadai
Hakuna njaa nchini
☞Sasa hivi kuna
upungufu wa Dawa hospitalini lakini Viongozi wetu wanadai
kuna dawa za kutosha
☞ sasa hivi kuna changamoto ya
Nishati hasa umeme na gesi ila utasikia tuna umeme wa kuuza kwa nchi jirani.
Taifa linahitaji uwazi na uwajibikaji wa kila mwananchi ili tuweze kufikia malengo yetu.
Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania.
Mchana mwema.