KINYWA CHAKO KIJAZWE NINI ILI KUMTUKUZA MUNGU NAKUWATIA MOYO WENGINE

ZABURI 71:8
Kinywa changu kitajazwa sifa zako,Na heshima yako mchana kutwa.

Tunapoianza siku mpya na wiki mpya hebu vinywa vyetu vijazwe furaha,upendo,uponyaji tunene maneno ya kuinuana na kumsifu Mungu kila wakati.

Tuwe waponyaji ,wafariji,watia moyo tukitamani kuona kila mtu anafurahia uumbaji na anauishi upendo...

Haijalishi unapitia changamoto gani..mahali hapa pawe faraja na nafasi ya kujiona kuwa unayosababu ya kuendelea kuwepo na kufurahia baraka tele Mungu anazotujalia

Vinywa vyetu vijazwe sifa na heshima kwa Mungu Baba ili duniani pawe mahali pazuri pa kuishi na kuwasaidia wengine wajisikie vizuri.
Tunakushukuru Mungu kutufikisha umbali huu hakika wewe ni Ebenezer,
Umetutoa mbali na hujawahi kutuacha wakiwa.
Asante kwa siku ya leo na wiki inayoanza leo tembea pamoja nasi.
Tunaomba kibali chako katika kila jambo tutakalotenda,Tupe kauli njema,tupe Roho ya Upendo,na kunyenyekea mbele zako.
Tuweke mbali na kuonewa,magonjwa,chuki,mikosi,hila na ajali mbaya.
Tupe ujasiri Amani na Imani katika Kristo Yesu kupitia jina la Yesu Mpatanishi na Mwokozi wetu Amen
WIKI NJEMA
KAZI NJEMA
JUMATATU NJEMA
MBARIKIWE