Makapuku Forum

Makapuku Forum

d947e6fe5d2d110db046ffd5af15aea6.jpg
7182aea8fb5b98e571bd094f3d4c58de.jpg
Mmh
 
TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE


MITHALI 25

21 Adui yako akiwa ananjaa ,mpe chakula;Tena akiwa anakiu ,mpe maji ya kunywa.

22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake;Na Bwana atakupa thawabu.

Katika suala gumu maishani moja wapo ni hili la kuwapenda maadui zetu,Lakini ndivyo ilivyo hata kwa Bwana Yesu alisema wasamehe maana hawajui watendalo.
Mtu akikukosea Mwambie Bwana Teta nao wanaoteta nami........Zaburi 35 ..................... usiwe na hasira ya kudumu.

Katika somo hili unapompenda na kumtendea mema adui

Bwana atakupa thawabu.
Utakuwa umemsaidia yeye kubadilika pia
Ni adhabu tosha maana neno lasema utakuwa umewasha makaa ya moto kichwani mwake.


Wapendwa siyo kazi nyepesi ila kwa msaada wa Roho Mtakatifu inawezekana.

Tunakushukuru Baba kwa ulinzi wako na kutuamsha salama ,asante kwa yote unayotutendea asante kwa afya ,riziki ,marafiki na maadui tunaomba uendelee kutuimarisha tuweze kuwa na uvumilivu wa kuwapenda maadui na kuwaombea.

Siku ya leo ponya roho zetu,ponya majeraha,ponya wafiwa,wagonjwa ,wenye mahitaji..

Tufundishe kuchukuliana mizigo kwa upendo na kuwa sababu ya furaha kwa wengine na kuwasaidia watu kubadilika na kutenda kadri wanavyopenda kutendewa

Asante Baba kwa sababu utatupa kushinda kila siku za maisha yetu na kutujenga kuimarishana maana hakuna mkamilifu.

Jumapili ya leo ikawe ya baraka ushindi na kutubdilisha.

Kwa jina la Yesu Mpatanishi na Mwokozi wetu Amen

WAPENDWA JUMAPILI NJEMA
asante mama mchuchu ubarikiwe sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom