Makapuku Forum

Makapuku Forum

04168fa7a0cfb38554274117b6aad0a7.jpg
 
Top Ten Writters/Authors of All time.

1.William Shakespeare;
(Aprili 1564 - 23 Aprili 1616) alikuwa mwandishi mashuhuri nchini Uingereza.

Waingereza mara nyingi humtazama kuwa mwandishi mkuu wa lugha yao. Aliandika hasa maigizo na tamthiliya. Alifanya pia kazi ya uigizaji.

Mwandishi huyo akiwa mdogo alikuwa anapenda kusoma sana hadithi mbalimbali ambazo zilikuwa zimeandikwa kwa lugha ya Kilatini. Shakespear alisoma zaidi kazi za wanafalsafa wakongwe wa Kigiriki Aristotle na Plato, pia alipenda sana teolojia.

Maigizo yake hupangwa katika vikundi vya:

Kutokana na wingi wa kazi na mada, wataalamu wengine hawakubali ya kwamba maandiko yote yanayojulikana kama ya "Shakespear" yameandikwa na mtu yeye yule, lakini walio wengi wameridhika ya kwamba huyu Shekespear wa kihistoria mwenyewe alikuwa mwandishi wa hayo yote.


Kati ya maandiko yake mashuhuri ni kama:

Michezo Tanzia
Tamthiliya za Kuchekesha
Tamthiliya za Kihistoria
  • [URL='https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Richard_III_%28tamthiliya%29&action=edit&redlink=1']Richard III
[/URL]

Mchezo tanzia "Julius Caesar" pamoja na tamthiliya ya kuchekesha "The Merchant of Venice" vimetafsiriwa na Mwalimu Julius Nyerere kwa lugha ya Kiswahili ("Julius Kaisari" na "Mabepari wa Venisi")
 
2.Charles Dickens (7 Februari 18129 Juni 1870) alikuwa mwandishi wa riwaya nchini Uingereza. Aliandika mengi na hadithi pamoja na riwaya zake zimetafsiriiwa katika lugha nyingi.

Alizaliwa Landport-Portsmouth kama mtoto wa pili kati ya wanane. Alipokuwa na umri wa miaka 10 babake alifungwa gerezani kwa sababu ya madeni na mama pamoja na kaka na dada zake walihamia gerezani palepale. Charles pekee alibaki nje akaanza kutafuta kazi ili apate kulisha familia.

Pamoja na watoto wengine alifanya kazi katika ghala. Alipokuwa na miaka 12 aliendelea na kazi ya kiwandani akashindwa kusoma shule mara kwa mara.

Baada ya baba kuachishwa gerezani mwaka 1824 Vharles alipata nafasi ya kusoma na tangu 1827 akaajiriwa na wakili kama mtumishi wa ofisi. Hakuridhika na kazi hii akajifundisha hati mkato akaendelea kuwa karani bungeni na tangu 1831 alipata kazi kama mwandishi wa magazeti. Hapa alianza mwaka 1836 kutoa sura za riwaya yake ya kwanza iliyoitwa "The Pickwick Papers"; kila mwezi sura mpya ilichapishwa kama daftari na kuuzwa. Riwaya hii iliunda sifa yake kama mwandishi mashuhuri.

1837 aliendelea na riwaya "Oliver Twist". Mwishowe alikuwa mhariri wa magazeti makubwa akiendelea kutoa masimulizi na riwaya. 1865 aliathiriwa na ajali ya treni ambamo hakujeruhiwa kimwili bali ndoto za ajli ziliendelea kumtesa hadi mwisho wa maisha yake. 1868 alinunua nyumba kubwa ya kikabaila ya Gadshill Place iliyokuwa mahali pa kukutana kwa wasanii na waandishi. 1870 Charles Dickens aliaga dunia kwake nyumbani Gadshill. Alipewa kaburi kwenye kitengo cha washairi katika kanisa la Westminster Abbey.
 
Imekaa vizuri
Top Ten Writters/Authors of All time.

1.William Shakespeare;
(Aprili 1564 - 23 Aprili 1616) alikuwa mwandishi mashuhuri nchini Uingereza.

Waingereza mara nyingi humtazama kuwa mwandishi mkuu wa lugha yao. Aliandika hasa maigizo na tamthiliya. Alifanya pia kazi ya uigizaji.

Mwandishi huyo akiwa mdogo alikuwa anapenda kusoma sana hadithi mbalimbali ambazo zilikuwa zimeandikwa kwa lugha ya Kilatini. Shakespear alisoma zaidi kazi za wanafalsafa wakongwe wa Kigiriki Aristotle na Plato, pia alipenda sana teolojia.

Maigizo yake hupangwa katika vikundi vya:

Kutokana na wingi wa kazi na mada, wataalamu wengine hawakubali ya kwamba maandiko yote yanayojulikana kama ya "Shakespear" yameandikwa na mtu yeye yule, lakini walio wengi wameridhika ya kwamba huyu Shekespear wa kihistoria mwenyewe alikuwa mwandishi wa hayo yote.


Kati ya maandiko yake mashuhuri ni kama:

Michezo Tanzia
Tamthiliya za Kuchekesha
Tamthiliya za Kihistoria
  • [URL='https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Richard_III_%28tamthiliya%29&action=edit&redlink=1']Richard III
[/URL]

Mchezo tanzia "Julius Caesar" pamoja na tamthiliya ya kuchekesha "The Merchant of Venice" vimetafsiriwa na Mwalimu Julius Nyerere kwa lugha ya Kiswahili ("Julius Kaisari" na "Mabepari wa Venisi")
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom