Makapuku Forum

Makapuku Forum

Top Ten Writters/Authors of All time.

1.William Shakespeare;
(Aprili 1564 - 23 Aprili 1616) alikuwa mwandishi mashuhuri nchini Uingereza.

Waingereza mara nyingi humtazama kuwa mwandishi mkuu wa lugha yao. Aliandika hasa maigizo na tamthiliya. Alifanya pia kazi ya uigizaji.

Mwandishi huyo akiwa mdogo alikuwa anapenda kusoma sana hadithi mbalimbali ambazo zilikuwa zimeandikwa kwa lugha ya Kilatini. Shakespear alisoma zaidi kazi za wanafalsafa wakongwe wa Kigiriki Aristotle na Plato, pia alipenda sana teolojia.

Maigizo yake hupangwa katika vikundi vya:

Kutokana na wingi wa kazi na mada, wataalamu wengine hawakubali ya kwamba maandiko yote yanayojulikana kama ya "Shakespear" yameandikwa na mtu yeye yule, lakini walio wengi wameridhika ya kwamba huyu Shekespear wa kihistoria mwenyewe alikuwa mwandishi wa hayo yote.


Kati ya maandiko yake mashuhuri ni kama:

Michezo Tanzia
Tamthiliya za Kuchekesha
Tamthiliya za Kihistoria
  • [URL='https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Richard_III_%28tamthiliya%29&action=edit&redlink=1']Richard III
[/URL]

Mchezo tanzia "Julius Caesar" pamoja na tamthiliya ya kuchekesha "The Merchant of Venice" vimetafsiriwa na Mwalimu Julius Nyerere kwa lugha ya Kiswahili ("Julius Kaisari" na "Mabepari wa Venisi")
Huyu nae alikuwa kichwa hatari
 
4.Fyodor Dostoevsky;
200px-Dostoevsky_1872.jpg


(11 Novemba 1821 (30 Oktoba ya Kalenda ya Juliasi) – 9 Februari 1881 (28 Januari ya kalenda ya kale) alikuwa mwandishi wa riwaya nchini Urusi. Mara nyingi ametajwa kama mwandishi Mrusi muhimu zaidi. Kati ya riwaya zake zianzojulikana kimataifa ni "Kosa na adhabu" pamoja na "Ndugu Karamasov".

Dostoyevski alizaliwa katika familia ya makabaila maskini babake alikuwa mganga. 1838-1843 alisoma uhandisi kwenye chuo kikuu cha kijeshi mjini Sankt Peterburg. 1839 alipata habari ya kwamba baba aliuawa na wakulima waasi alipokaa kwenye shamba lake. 1844 Fyodor alianza kutunga riwaya yake ya kwanza "Watu Maskini" iliyopokelewa vizuri na kuweka msingi wa kwanza kwa umaarufu wake.

1847 Dostoyevski alishiriki katika kundi la wanamapinduzi akakamatwa na kupewa adhabu ya kifo akasamehewa na Tsar Nikolai I na badala yake akapewa adhabu ya kufanya kazi nzito kwa muda wa miaka minne huko Siberia. Baadaye alipaswa kujiunga na jeshi hadi 1859.

Aliendelea kuandika na riwaya ya kwanza iliyopokelewa pia kimataifa ilikuwa "Kosa na Adhabu"iliyohusu kijana aliyekuwa mwuaji lakini baadaye anaanza kutambua dunia upya. Uwezo wa Dostoyevski wa kuonyesha roho na saikolojia ya watu ulionekana bora katika riwaya hii.

Kibinafsi Dostoyeski alipambana na hamu ya kucheza kamari iliyomsababisha kuwa na madeni makubwa.

Riwaya yake ya mwishi ilikuwa "Ndugu Karamasov" ambayo alishindwa kuimaliza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom