Makapuku Forum

Makapuku Forum

Pichani namuona Ronald Koeman ambaye enzi hizo alisifika kama beki mahiri anayecheza sana jihadi. Kwa kifupi alikiwa ni beki wa kukata na shoka.

Pia anashikilia rekodi ya kuwa beki aliyefunga magoli mengi zaidi katika mchezo wa soka. Alikuwa ni moto wa kuotea mbali katika kupiga faulo na mikwaju ya penati.

Kwa sasa ni kocha wa Everton ya Uingereza.

Nyakati ngumu hazipiti ila watu wgumu wanapita.
Na anatechnic kali sana za ufundishaji
 
Waliupiga mpira mwingi sana, atleast waliikaribia Uholanzi ya Kombe la Dunia la Mwaka 1974 pale Ujerumani, ambapo Uholanzi ile iliongozwa na Nahodha na Johan Cruyff na Johan Neeskes. Walifungwa fainali na mwenyeji Ujeruman.

Lakini kivutio kikubwa ilikuwa ni total football waliyoitandaza kamwe hawatasahaulika, maana mchezo wa fainali walifunga goli bila mchezaji yoyote wa Ujerumani kuugusa mpira.

Yohan Cruyff akahamishia falsafa ya total football alipokwenda Barcelona na yeye ndio mwasisi wa chuo maarufu cha mpira cha Barcelona kijulikanacho kama " La Masia " kinachotoa wachezaji mahiri kama Xavi, Iniesta, Messi, Busqet nk.
1472749217173.jpg
1472749225095.jpg
1472749231152.jpg

Niliona video yao walitisha sana
.........
 
Niliipenda sana kwa sababu ya Edgar Davis,sedoff, Frank deboer, Dennis Bergkamp, kruveit na wengineo Cocu
Wote hao.. Ila bergkamp kwa hakika alikuwa ananikosha zaid kwa soka lake, very talented player with skills and vision.. Amongst most completed player i have ever seen.

Seedorf nae alikuwa fundi.. Ronald na frank de boer.. Hapa patrik mzee wa heda, philip cocu, marc overmars n.k.. Walikamilika sana.. Watasubir kuja kupata kizaz kama hicho..
 
Huyo pichani ni Marco Van Basten, anachukuliwa kama mmoja kati ya Wafungaji hodari kuwahi kucheza soka.

Kitu pekee kilichomfanya asiingie katika rekodi za wafungaji bora wa wakati wote ni kustaafu kwake soka mapema akiwa na miaka 26 kutokana na jeraha la goti lililoshindwa kupona.

Alikuwa kocha wa Uholanzi World cup ya mwaka 2006 pale Ujerumani.
Bastern nilishawahi kutafuta video zake ....jamaa alikuwa mkali sana
.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom