Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wote hao.. Ila bergkamp kwa hakika alikuwa ananikosha zaid kwa soka lake, very talented player with skills and vision.. Amongst most completed player i have ever seen.

Seedorf nae alikuwa fundi.. Ronald na frank de boer.. Hapa patrik mzee wa heda, philip cocu, marc overmars n.k.. Walikamilika sana.. Watasubir kuja kupata kizaz kama hicho..
Sana makaveli
 
Pichani namuona Ronald Koeman ambaye enzi hizo alisifika kama beki mahiri anayecheza sana jihadi. Kwa kifupi alikiwa ni beki wa kukata na shoka.

Pia anashikilia rekodi ya kuwa beki aliyefunga magoli mengi zaidi katika mchezo wa soka. Alikuwa ni moto wa kuotea mbali katika kupiga faulo na mikwaju ya penati.

Kwa sasa ni kocha wa Everton ya Uingereza.

Nyakati ngumu hazipiti ila watu wgumu wanapita.
Sikuwahi jua rekodi hii....umetisha
.......
 
Niliipenda sana kwa sababu ya Edgar Davis,sedoff, Frank deboer, Dennis Bergkamp, kruveit na wengineo Cocu
Sasa hiyo unaizungumzia Dutch team ya World Cup 1998 pale Ufaransa, walifanya wonders sana, Timu ile iliundwa na wachezaji wengi toka Ajax Amsterdam kama vile Ronald Na Frank De boer, Van Der Sar.

Walifika Nusu wakatolewa kwa matuta, ila mechi dhidi ya Argentina, Denis Bergkamp alipiga goli la kideo sana.

Alipokea pasi ndefu ya juu toka nyuma, jinsi alivyoutuliza ule mpira na kumgeuza beki wa Argentina, Roberto Ayala ilikuwa ni burudani ya nguvu na kamwe haichoshi, kabla ya kufunga goli.

Pitia Youtube ujionee.
 
Wote hao.. Ila bergkamp kwa hakika alikuwa ananikosha zaid kwa soka lake, very talented player with skills and vision.. Amongst most completed player i have ever seen.

Seedorf nae alikuwa fundi.. Ronald na frank de boer.. Hapa patrik mzee wa heda, philip cocu, marc overmars n.k.. Walikamilika sana.. Watasubir kuja kupata kizaz kama hicho..
hahaha...uko vizuri mkuu.
 
Sasa hiyo unaizungumzia Dutch team ya World Cup 1998 pale Ufaransa, walifanya wonders sana, Timu ile iliundwa na wachezaji wengi toka Ajax Amsterdam kama vile Ronald Na Frank De boer, Van Der Sar.

Walifika Nusu wakatolewa kwa matuta, ila mechi dhidi ya Argentina, Denis Bergkamp alipiga goli la kideo sana.

Alipokea pasi ndefu ya juu toka nyuma, jinsi alivyoutuliza ule mpira na kumgeuza beki wa Argentina, Roberto Ayala ilikuwa ni burudani ya nguvu na kamwe haichoshi, kabla ya kufunga goli.

Pitia Youtube ujionee.
Huwa naliangalia sana hilo gori, kumbuka pia alikuwa na ugonvi na kocha na hakwenda kumpa mkono, japo ule ushindi ulikuwa muhimu sana kwa kocha
 
Wote hao.. Ila bergkamp kwa hakika alikuwa ananikosha zaid kwa soka lake, very talented player with skills and vision.. Amongst most completed player i have ever seen.

Seedorf nae alikuwa fundi.. Ronald na frank de boer.. Hapa patrik mzee wa heda, philip cocu, marc overmars n.k.. Walikamilika sana.. Watasubir kuja kupata kizaz kama hicho..
Bergkamp namkubali sana hasa alipokuja EPL, wachezaji wangu watatu bora wa kigeni kuwahi kucheza Epl miaka ya 2010 kurudi nyuma, Ronaldo, Henry na Bergkamp!!
 
Hapo viera anamchimba mkwara wazza, wazza alinywea kichizi, alikuwa anamuangalia kwa kisura fulani cha uwoga..

Mkuu nakukaribisha katika utunzi wa kitabu kiitwacho the rise n fall of arsenal on wenger's hands.
hahaha...sijaiifatilia sana Arsenal miaka ya karibuni haswa baada ya Wenger kupoteza ubora wake!!
 
Msimu uliopita nyuma yake, mechi kama hiyo iliyopigwa OT, Man Utd tulipata Penati dk za jioni kabisa, Van Nistelrooy akaenda kupiga akapiga mwamba wa juu akakosa.

Mechi ikaisha 0-0. Baada ya hapo Wachezaji wa Arsenal wakiongozwa na kamanda Martin Keown, Lauren, Ashley Cole na wengineo wakamfanyia vurugu kubwa kwa kumshika kichwa chake wakimtuhumu alijiangusha ndio maana Utd ikapata Penati.

Pia walimtuhumu kuwa alimdanganya refa hadi capyltain Vieira akapewa red card.
 
Tuwekee picha wakiwa Ac Milan.
1472750239607.jpg
1472750243950.jpg
1472750247999.jpg

Mwanaume
..........
 
Msimu uliopita nyuma yake, mechi kama hiyo iliyopigwa OT, Man Utd tulipata Penati dk za jioni kabisa, Van Nistelrooy akaenda kupiga akapiga mwamba wa juu akakosa.

Mechi ikaisha 0-0. Baada ya hapo Wachezaji wa Arsenal wakiongozwa na kamanda Martin Keown, Lauren, Ashley Cole na wengineo wakamfanyia vurugu kubwa kwa kumshika kichwa chake wakimtuhumu alijiangusha ndio maana Utd ikapata Penati.

Pia walimtuhumu kuwa alimdanganya refa hadi capyltain Vieira akapewa red card.
Nimekumbuka sasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom