Mkuu hapa umekengeuka kabisa nimepata ukakasi sana haswa kwenye maneno yako ya awali hapo ...Ungeweza kutumia namna ingine na ujumbe ungemfikia mlengwa tena kistaarabu sana...Tusikubali kabisa kuvunja undugu na ujamaa tulioujenga kupitia hapa kwani hata members wa hapa KAPUKU tukikutana kwenye majukwaa mengine tunakuwa na ile feeling ya undugu....Na nikushauri kitu Prezda labda hata na mimi kuna mtu nimemkwaza hapa kwa namna moja au nyingine bila mimi kujua mtu huyu kwanza yapasa aniambie mimi hata kwa PM kuwa unanikwaza na sipendi 1,2,3..Akiona sisikii anaweza kureport ishu kwako..Na wewe lazima ukalie kiti na nafasi yako kwa hekima na busara iingia huko PM niambie kuna 1,2 ,3 hakika nitakuwa msikivu maana lengo hapa si kukwazana kwa namna yeyote ile ni kijiwe cha kufanya tucheke tufurahi wakati maisha ya upande mwingine yanaendelea...So please itakuwa vizuri na Member wengine waache uwoga ama unafiki nikikuuzi niambie straight forward tu ili kuepusha mpasuko hapa kijiweni..Naomba nenda PM na Jambilo mwambie 1,2,3 kuwa ni member yupi huyo amelalamika then mmalize na maisha yaendelee kama kawa ida hapa..
Wakuu nimewaza saana na kutafuta kosa langu lakini hadi sasa silioni, labda mnifungue akili.
LAKINI nimeitwa Kifaru Yaani mjinga, zoba, mshamba na mtu anaitwa BITOZ.
Ameniuliza Hivi mimi ni mtu mzima Kweli? Mbona ninafanya mambo yakijinga!!!??
Nimejiuliiza,
Hivi niko jukwaa gani? Jibu ni chit chat..Yaani jukwaa lisilo na lengo mahususi, utani unaweza kuwepo nk Lakini nisiudhi au kudhalilisha mtu.
Nilichokifanya nimekuwa nikitaniana na Patience123 ambaye kimsingi ni rafiki yangu ndani na nje ya kapuku tena utani kwa ridhaa yake na yangu. Lakini yeye na mpambe wake Boris wanaudhika, nimewakosea nini ktkt hili?
Bitoz unataka kujifanya tulia akson kwa social forums za watu!
Kosa liko wapi?
Linamo pia nimemtania.
Kwa ridhaa yake mwenyewe
Kosa liko wapi?
Je! Patience au linamo wamelalamika?
Kama wamelalamika kwa Bitoz..walishindwaje kuniambia ilihali twawasiliana nje ya jukwaa?
Nimesikitika sana kwa mtu kuthubuti kujiita kiongozi halafu akapungukiwa na hekima, busara na maarifa mara litokeapo tatizo.
Kimsingi sijapokea malamiko au onyo hivyo ni uongo kudai nimeonywa.
Hivi unawezaje kujiita rais kwenye mtandao wenye wenyewe?
Hivi unawezaje kuwachagulia watu kitu cha kusema?
Namjua vyema aliyekuja pm nimepata mashaka na uwezo wake kiakili.
Napata taabu na uwezo wa kufikiri wa Bitoz
Napata mashaka na uelekeo wa makapuku
Je makapuku ni watumwa wa fikra wa Bitoz?.
Hapana bali anataka heshima, aogopwe, atambuliwe kama mmiliki wa makapuku.
Ninakutangazia sikuogopi na sitakaa nikuogope.
Pia hapa sitoki niko tayari kufungiwa ikibidi kwani siishi kwa kutegemea kapuku au jf bali niko kwa ajili kufurahiana na jamaa na Marafiki
Jitafakari kijana, umewakimbiza wengi sana but mimi nooooo
Inabidi wapewe semina... Maaana unaweza kuta mtu maarufu mjuaji alafu hajui maaana Yake...
Shame...
Yaishie huko huko....ukiyaleta humu utaleta mgongano....na ugomvi....
Kama mtu anaona sio vema kusema hapa....then usilete hapa Haata nucta.
Kama kuna mtu analalamikiwa pm kamueleze pm huko...
Ukiamua kuleta hapa Basi leta full issue tujadili....
Kwa Hiyo akiwa mbishi ndio aitwe kifaru??? Aghhhhrrr....busara wapi???
Umekomalia hilo neno tu
.............
Ila wakuu mnajua maana ya ChitChat
Wengine tuna midevu ila tunajichanganya kuondoa stress hvyo Tuheshimiane kwa kila mmoja wetu mambo ya pm na malalamiko ya pm malizianeni pm haina maana ya kudhalilishana wakati tu Familia moja
AMANI ITAWALE
SOTE TU WAMOJA