Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo June 24, 2023
Screenshot_20230624_063054_Opera%20Mini.jpg
 
Mwanafunzi wa Kidato cha Tano, Esther Noah wa Shule ya Sekondari Pandahili aliyepotea May 18, 2023 amepatikana katika chumba cha kupanga cha Mama Abdul kilichopo maeneo ya Ifisi Mbalizi Mkoani Mbeya na imebainika kuwa alipelekwa hapo na muuza mkaa aitwaye Baba Jose na kusema ni Mke wake hivyo anaomba hifadhi baada ya siku mbili angemchukua ili wakaishi wote.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema Baba Jose baada ya kukaa na Mtoto huyo kwa muda alienda kumpeleka kwa Mama Abdul na kuahidi kwenda kumchukua siku atayapota chumba Ili wakaendelee kuishi pamoja.

Akiongea ofisini kwake ambako Binti huyo amepelekwa akiwa na Mama yake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera ametoa rai kwa Walimu wa Pandahill kupunguza kasi ya kuchapa viboko Wanafunzi kwani ni miongoni mwa sababu inayoelezwa kuchangia Mtoto kukimbia Shule

Homera amesema vipimo vyote vya kiafya vimefanyika na Ester hana ujauzito na hivyo ataendelea kukaa na Maafisa ustawi wa jamii ili kumsaidia kumpa ushauri wa kisaikolojia arudi Shule, na Mwanaume huyo atasakwa mpaka akamatwe.

Amesema amepimwa pia kipimo cha mimba Ili kujua hali yake na majibu yameonyesha hana mimba na kwa siku zijazo akibainika ana mimba watampa nafasi ya kwenda kujifungua na kurudi Shule.
Screenshot_20230624_064151_Instagram.jpg
 
Serikali ya Uganda imesema inapanga kuongeza umri wa unywaji pombe kutoka miaka 18 hadi 21 ili kukabiliana na unywaji pombe unaopita kiasi.

Akiongea katika kongamano la pili la Wakuu wa Kitaifa 2023, tukio lililolenga kuandaa mikakati ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya kwa Wanafunzi nchini Uganda, Kamishna wa Wizara ya Afya, Afya ya Akili, Pombe na Dawa za Kulevya, Dkt. Hafsa Lukwata amesema dhamira ya sheria hiyo mpya ni kupunguza idadi ya Watu wanaonunua pombe.

Kwa mujibu wa Afisa huyo ikiwa Mtu hatumii kilevi chochote kabla ya kufikia umri wa miaka 21, uwezekano wa kunywa pombe kwenye maisha yake hupungua mpaka 48%.

Kulingana na ripoti ya mwaka 2023 iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa wastani, Raia wa Uganda hutumia lita 12.21 za pombe kila mwaka na Wanaume hunywa pombe nyingi zaidi kupita Wanawake ambapo Wanaume hutumia wastani wa lita 19.93 za pombe safi kila mwaka ikilinganishwa na lita 4.88 kwa Wanawake.

Ripoti hiyo inaonesha kuwa vifo milioni tatu (5.3% ya vifo vyote) Ulimwenguni pote hutokea kila mwaka kutokana na unywaji pombe. Shirika la Afya duniani WHO inasema unywaji pombe kupita kiasi ndio sababu kubwa ya magonjwa zaidi ya 200 Ulimwenguni.
Screenshot_20230624_064311_Instagram.jpg
 
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika leo ameongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam na moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba ipo haja ya mjadala mkubwa wa kitaifa kuhusu mkataba wa Bandari kuendelea kujadiliwa ili wakati wa kuhitimisha Bunge la bajeti, Serikali itoe majibu yatajayowaridhisha Wananchi kuhusu suala hilo.

“Bajeti hii ya mwaka 2023/24 imezungumzia miradi ya Bandari na Waziri wa Fedha amesema bajeti inaendeleza miradi ya kimkakati ikiwemo eneo la Bandari ya Bagamoyo na Bandari ya Dar es salaam, na uendelezaji wa Bandari ya Tanga, kwa Bagamoyo amesema hatua za ujenzi wa Bandari ya kina kirefu Bagamoyo unaendelea”

"Kwahiyo Serikali katika bajeti hii imepeleka mapendekezo ya matumizi ya fedha za Umma na za Washirika wa maendeleo katika uendelezaji wa Bandari, wakati Serikali inapeleka mapendekezo haya tayari kuna utata mkubwa kuhusu mkataba wa Bandari kati ya Tanzania na Dubai"

"Ni vema jambo hili tuendelee kulijadili, najua jana umejitokeza mjadala Bungeni na baadhi ya vyombo vyenu vya habari leo vimenukuu michango ya Wabunge jana wakijadili kuhsu Bandari, kabla sijaendelea mbele niwaombe Wanahabari kwamba jambo hili la Bandari nafahamu kwamba baadhi yenu mna maelezo ya kutoliandika au kutolirusha au kutofanya lizungumzwe sasa kama linazungumzwa Bungeni na Wabunge ni haki kulizungumza nje ya Bunge”

"Pengine baadhi yenu mnaweza kuona baada ya majibu ya Waziri Mkuu hili suala halihitaji mjadala, Mimi nina mtazamo kwamba hotuba ya Waziri Mkuu na mjadala wa Wabunge viwe sababu ya kuendeleza mjadala mkubwa wa kitaifa kuhusu jambo hili ili wakati wa kuhitimisha Bunge la bajeti Serikali itoe majibu”
Screenshot_20230624_064427_Instagram.jpg
 
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika leo ameongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam ambapo amehoji kwanini Bunge limedharau ushauri wa Wananchi wa kufanya mjadala kwanza kabla ya kuidhinisha mkataba wa makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kuhusu uendeshaji wa Bandari.

"Waziri Mkuu amesema anakaribisha ushauri kuhusu jambo la Bandari, sasa ni vizuri Waziri Mkuu akalieleza Bunge maana ile hotuba ameitolea kwenye nyumba ya Ibada, ni vizuri atoe hotuba Bungeni alieleze Taifa kwamba wao wanakaribisha ushauri sasa hivi lakini kabla tulitoa ushauri kabla ya kuidhinisha na Bunge tuwe na mjadala sasa wameacha ushauri wa Wananchi wakaidhinisha na sasa wanataka mjadala, Waziri Mkuu aeleze ni sababu zipi zilifanya wapuuze ushauri na wakaidhinisha”

"Waziri Mkuu amesema hili suala limeibuka sasa kwasababu Serikali hii tofauti na Serikali iliyopita imeamua kulipeleka jambo hili Bungeni, kwahiyo Wananchi wakisikiliza wanasema mjadala huu ni mkali kwasababu Rais Samia amemua mikataba ipelekwe Bungeni na kuwa wazi mjadala umekuwa mkali, kitu ambacho sio kweli, Mimi nikiwa Bungeni 2017 Serikali ilipeleka makubaliano ya mkataba kama huu wakati Rais akiwa Magufuli kuhusu ujenzi wa Bomba la mafuta, sasa kwanini mkataba ule haukuwa na utata mkubwa kama huu wa sasa jibu lipo kwenye masharti ya mkataba wa sasa"

"Waziri Mkuu amezungumzia kwamba hakuna hatari ya kiusalama kuhusu mkataba huu kwamba kuna Kituo cha Polisi Bandari wataendelea kuwepo, Jeshi la Wanamaji lipo pale , jambo la msingi ambalo Waziri Mkuu anatakiwa alitolee maelezo ni kifungu cha 6(2) cha mkataba ambacho kinaeleza mazingira ya usalama lazima yawe yamekubaliwa na pande zote mbili"

"Sasa Waziri Mkuu atueleze Serikali ya Tanzania akiona shida halafu Serikali ya Dubai ikaona hakuna shida kwa mazingira ya kiusalama kwa mkataba huu, je kifungu hiki hakiibani Tanzania kiusalama, Marekani iliingia kwenye ubishani kama huu, DP World ilinunua kampuni inayoendesha Bandari kadhaa Marekani lakini Bunge likasema hili jambo ni hatari kwa mazingira ya kiusalama, Bunge likamkatalia Rais Bush, kampuni ya DP World ikauza ile kampuni iliyonunua kwa kampuni nyingine ya Marekani"
Screenshot_20230624_064520_Instagram.jpg
 
GREENWOOD ARUDI MZIGONI
.
Kinda wa Manchester United, Mason Greenwood ameonekana kwa mara ya kwanza akifanya mazoezi na mwalimu wake binafsi. Kinda huyo alikuwa nje ya dimba kwa muda mrefu baada kukamatwa kwa tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia na kutishia kumuua mpenzi wake, Harrieth Robson.
.
Baada ya kesi yake kufutwa na Mahakama ya Great Manchester, Februari mwaka huu fowadi huyo sasa ameanza kufanya mazoezi akiwa sambamba na mwalimu wake ambaye anamsaidia kujiweka fiti. Greenwood alionekana akiwa na mpira mguuni huku akipiga mashuti katika mazoezi yaliyodumu kwa dakika 90 katika uwanjani wa kukodi.
.
Nywele zake zimeonekana kukua na hakuvaa njumu za Nike kwasababu kampuni hiyo ilivunja mkataba kufuatia kesi iliyokuwa ikimkabili. Uongozi wa Man United bado unaendelea na uchunguzi kwa kina kabla ya kufanya uwamuzi kuhusu hatima yake.

Screenshot_20230624_064622_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom