Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo June 11, 2023
Screenshot_20230611_063906_Opera%20Mini.jpg
 
Kipa wa Inter Milan raia wa Cameroon Andre Onana amefikia makubaliano ya kimsingi na Chelsea lakini Inter wamekataa dau la awali la pauni milioni 34 la The Blues kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Tuttomercatoweb)

Screenshot_20230611_070453.jpg
 
The Gunners, Arsenal wanaripotiwa kupiga hatua kubwa kwenye mazungumzo ya mkataba mpya na beki wake Mfaransa William Saliba ili isimpoteze kwenye dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi barani Ulaya.
.
Saliba alikuwa kwenye ubora mkubwa kwenye timu ya Arsenal msimu wa 2022-23 na jambo hilo limefanya klabu kibao kuhitaji saini yake ikiwamo mabingwa wa soka wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.
.
Saliba aliumia Machi na kushindwa kuitumikia timu yake, lakini kabla ya kuumia alifunga mabao matatu na kuasisti mara moja katika mechi 33 na hakika aliunda kombinesheni matata kabisa na beki mwenzake Gabriel Magalhaes. Na sasa kocha Mikel Arteta anahangaika kuhakikisha kwamba anamsainisha mkataba mpya beki huyo ili kuepuka kusumbuliwa na timu nyingine zitakazohitaji saini ya mchezaji huyo.

Screenshot_20230611_070604.jpg
 
Kiungo wa Chelsea, Mateo Kovacic anatarajiwa kujiunga na Manchester City wiki ijayo baada ya kuripotiwa amefikia makubaliano kutua Etihad. Mkali wa habari za usajili Ulaya, Fabrizio Romano amesema ofa itatolewa baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya leo dhidi ya Inter Milan.
.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England walishaanza mazungumzo kwa ajili ya kiungo huyo wa kimataifa wa Croatia tangu wiki iliyopita na Kovacic alikiri katika mahojiano mojawpo kwamba ataondoka baada ya Chelsea kuzingua msimu uliopita.
Screenshot_20230611_071210.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom