Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Aisee Dunia inakwenda fasta sana.. tumemaliza ya Titanic yanakuja ya Urusi ..sasa moto unawaka huko Urusi.
Vikosi vya wanajeshi vimeasi vinaongozwa na kundi la wanajeshi mamluki la Wagner. Rais wa Urusi Vladimir Putin ameapa 'kuwanyorosha' wanajeshi hao na amewataka wajisalimishe mara moja.
Kiongozi wa kundi hilo Bwana Yevgeny Prigozhin ambaye anadaiwa kuwa rafiki wa karibu wa Putin amesema yeye hataki kufanya mapinduzi lakini anataka mabadiliko katika Uongozi wa jeshi la nchi hiyo.
Kiongozi huyo amedai uvamizi wa Putin Ukraine ulikuwa umejaa uongo mtu na hakukuwa na sababu zozote za msingi za Urusi kuivamia Ukraine isipokuwa ilichochewa sana na Waziri wa Ulinzi Bwana Sergei Shoigu ili apande cheo.
Kundi la Wagner limehusishwa na matukio ya kikatili zaidi sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Afrika ya Kati, Syria, Msumbiji na vita inayoendelea huko Ukraine. Mpaka sasa kundi hilo limetangaza kuteka miji miwili katika nchi ya Urusi..je huu ndio utakuwa mwisho wa utawala Putin..!?
Vikosi vya wanajeshi vimeasi vinaongozwa na kundi la wanajeshi mamluki la Wagner. Rais wa Urusi Vladimir Putin ameapa 'kuwanyorosha' wanajeshi hao na amewataka wajisalimishe mara moja.
Kiongozi wa kundi hilo Bwana Yevgeny Prigozhin ambaye anadaiwa kuwa rafiki wa karibu wa Putin amesema yeye hataki kufanya mapinduzi lakini anataka mabadiliko katika Uongozi wa jeshi la nchi hiyo.
Kiongozi huyo amedai uvamizi wa Putin Ukraine ulikuwa umejaa uongo mtu na hakukuwa na sababu zozote za msingi za Urusi kuivamia Ukraine isipokuwa ilichochewa sana na Waziri wa Ulinzi Bwana Sergei Shoigu ili apande cheo.
Kundi la Wagner limehusishwa na matukio ya kikatili zaidi sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Afrika ya Kati, Syria, Msumbiji na vita inayoendelea huko Ukraine. Mpaka sasa kundi hilo limetangaza kuteka miji miwili katika nchi ya Urusi..je huu ndio utakuwa mwisho wa utawala Putin..!?
KIVUMBI NA JASHO.
Hatushabikii timu kwasababu ya Wachezaji au historia bali kutokana na mioyo yetu kujikuta sehemu ya timu, inakuwa maisha yetu na sehemu ya furaha yetu hii ni kaulimbiu ya Mashabiki wa soka duniani kote. 
