Hiki Chombo kimepotea baharini jana. Kilikuwa na matajiri wa Uingereza na kilikuwa kinawapeleka kuona mabaki ya meli ya Titanic iliyozama miaka 111 iliyopita.
Chombo hiki kilikuwa na watu watano, miongoni mwao ni bilionea Hamish Harding.
Licha ya utajiri wake Hamish Harding amekuwa akicheza michezo ya hatari sana kama wafanyavyo malast born ikiwemo kukaa muda mrefu zaidi kwenye sehemu ya kina kirefu zaidi cha bahari hapa duniani.
Watu wengine waliokuwemo kwenye chombo hicho ni tajiri mwingine kutoka Uingereza bwana Shahzada Dawood aliyekuwa na mtoto wake.
Watu wanauwezo wa kukaa siku 3 wakiwa hai kwenye hicho Chombo cha Kampuni ya Ocean gate vinginevyo wanapoteza maisha kwa sababu kina uwezo wa kutunza Oxygen kwa siku 3 tu.
Kwa sasa mabaki ya meli ya Titanic yako kwenye kina cha mita 3962 katika bahari ya Atlantic. Ili kusafiri na chombo hicho kwenda kuona mabaki ya Titanic mtu mmoja analipa nauli ya Shilingi Milioni 600.
Pichani ndie Bilionea Hamish Harding mwenye michezo ya hatari kama last born..


Ana umri wa miaka 48.
Bilionea huyu anashikilia rekodi tatu za Guinness kutokana na hiyo michezo yake ya hatari.
Pia anashikilia rekodi ya binadamu wa kwanza kuizunguka dunia kwa spidi kubwa zaidi..!!
View attachment 2663230View attachment 2663231