Makapuku Forum

Makapuku Forum

Farhan Jr

Naandika hii post saa 4:34 usiku huu kutoka kwenye mitaa ya kawaida na vyumba bei chee Ubungo, naandika hii leo tarehe 13 Juni, 2023 siandiki kwa ajili yetu bali naandika kwa ajili ya wale wanaoitazama hii picha mwaka 2123 takribani miaka 100 kutoka hivi sasa, msiache picha hii ipotee.

Huenda soka kipindi hicho wanacheza Marobot ya Elon Musk lakini kutoka dunia yetu tunawaambia kuwa zama hizi Binadamu walisukuma kabumbu na kuipa Yanga Afrika matokeo uwanjani, majina na kumbukumbu zote rejeeni Google na Maktaba, washeni mishumaa kuwaombea zaidi pumziko jema.

Huenda miaka 100 kutoka sasa msifahamu hapo ni wapi! Hapo ni Kariakoo ilikuwa mitaa maarufu ya kibiashara ambapo TRA waliwahi kuvutana na Wafanyabiashara rejeeni kumbukumbu mtaona, ila hii siku Kariakoo ilifurahi kwa pamoja! Wananchi walipita na makombe yao! Mfanyabiashara na Mteja walibeba simu zao na kurecord kumbukumbu kwa pamoja, once in a lifetime.

Dear Future naomba niwaambie kuwa Yanga alicheza mechi nne ndani ya siku nane, mechi mbili za NBC dimba gumu la Sokoine, mechi moja Algiers na nyingine Pwani ya Kaskazini Tanga ya FA! Dear Future, kama Mashabiki tu walichoka kusafiri basi hadi wachezaji waliamka tu na mazoezi kidogo kisha wakaingia kwenye mechi, haikuwa rahisi uliza kiatu kwa sauti ya DJ Mark.

Huu ni msafara wa timu ya mpira, mitaa ilifungwa bila nguvu ya Polisi bali Mamlaka ya hisia na Mapenzi ya kweli kwa mpira wa miguu, walikatiza Msimbazi nyumbani kwa Simba na wala haikuwa vita kwakuwa Simba wanasema MY GAME IS FAIRPLAY, msigombane kisa hizi timu mmoja akifanikiwa pigeni makofi na mizimu itafurahi na mbingu za baraka zitafunguka, ninyi ni watani na sio Maadui.

Dear Future msiwe Wachoyo endeleeni kuandika kwa ajili ya vizazi na vizazi, tunzeni vyema kumbukumbu zenu kama ambavyo Mimi nilitunza hizi kwa ajili yenu.

One more time, hongereni sana Wananchi

Screenshot_20230614_145943_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

DUNIA YA TAASISI, Vijana wenzangu unapoaminiwa sehemu yoyote ile hakikisha unalinda sana mdomo wako na taswira yako kwa Wafanyakazi wenzako na Maboss wako, wao ndio Mabalozi wa kwanza kwako nje na ndani!

Ukiwa CLOUDS MEDIA jifunze kuiheshimu TBC! Ukiwa TMichezo basi waheshimu betting wengine, ukiwa CHADEMA waheshimu CCM ama viceversa, kuna leo na kesho ili usipate shida ya kujielezea sana basi chagua sana kutanguliza busara kwenye kila kitu, usinene ukamaliza! Usile ukavimbiwa sana.

Vijana wenzangu hapo ofisini kwako mheshimu kila Mtu, Mfagiaji anaweza asiwe na jukumu hilo tu unalojua maana dunia ina siri nyingi sana! Mpishi anaweza asiwe tu Mpishi maana dunia ina mengi, wakati unamheshimu HR usimsahau Mlinzi! Tengeneza Mabalozi wengi kuliko maadui, ofisini tembea mabega chini.

Ukifanya kazi Yanga usiwaseme Simba vibaya kwa unafki ama majungu, ukiwa Simba usiwakandie Yanga kwa unafki au majungu kwakuwa taasisi hazigombani duniani, leo na kesho ulichosema gizani kitakuwa mwangani, fanya kazi yako kwa taaluma yako kisha acha uwezo wako ujitetee.

Dunia ya taasisi ipo tofauti sana! Wanapokutuma ukaongee kwa niaba ukiweza kataa, waambie napendelea maandishi kuliko mdomo! Andika maneno sahihi na pitia kwa usahihi! Ogopa mdomo ukishasema watu wananukuu, itakusumbua kesho.

Vijana wenzangu mchana huu kama una bahati ya kuketi kiti cha ofisini basi tambua nje kule kuna wengi wana uwezo kuliko wewe ila wamekosa nafasi, ukianza kujiona mkubwa kuliko taasisi basi ni Paka amekubali kulala chali, omba ruhsa kazini.

Mungu atubariki sote! Tusisahau kuficha hatua zetu, tutembee peku kwa kunyata kwakuwa hakuna anayetaka mafanikio yako zaidi yako, ukifanikiwa FICHA, ukipanda cheo KAUSHA, una mshahara mkubwa VUNGA, maisha yako ni code yako, ni password yako! IFICHE.

Be average, usikae kwenye njia za watu! Be normal usikere watu japo huwezi kuridhisha wote ila jipe muda wa kuhakikisha huvuki mstari wako! Be cautious tunaishi mara moja tu.

Usisahau kuheshimu Mkubwa kwa Mtoto! Watu wanatembea na risiti, ukimdharau leo atakutunzia kisha kesho atakupatia risiti yako, I LOVE YOU ALL, LETS WIN, HOME SIO SAFI
 
Kinda raia wa Uingereza Jude Bellingham (19) ametambukishwa rasmi Real Madrid akitokea Borussia Dortmund ya Ujerumani

Bellingham amesaini mkataba wa miaka 6 kuwatumikia wababe hao wa Hispania na Ulaya
Screenshot_20230614_151907_Instagram.jpg
 
Kocha wa timu ya Taifa Adel Amrouche na Shirikisho bado hawajatangaza Kikosi rasmi kilichoingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Niger lakini sisi kama Wadau tunajaribu kutafuta taarifa kutoka vyanzo mbali mbali ili angalau Watanzania wapate kujua ni Wachezaji gani wameitwa, kwa mwanzo huu huwenda wahusika wakatoka hadharani na kutuambia ni Wachezaji gani wameitwa .

Kwa kufuatilia kwangu mitandao nimeona baadhi ya Wachezaji kama

Msuva
Samatta
Himid Mao
Novatus Dismas
Mudathir Yahya
Tiba John na
Abdi Banda

(Banda yeye ameweka alama ameingia Nchini nahisi anaweza kuwepo kwani ni muda mrefu hajaitwa )

Naendelea kufuatilia na tutajuzana Walioitwa kwa mtindo huu wakati tunasubiri taarifa rasmi ya Wahusika .
Screenshot_20230614_152013_Instagram.jpg
 
Mbappé kuhusu Messi kuondoka ndani ya PSG

"Bado sielewi kwanini watu wamefurahi Messi kuondoka Klabuni yule ni Legend anatakiwa kuewa heshima ni mmoja wa wachezaji bora katika historia ya soka Duniani sio habari njema Kwa mtu kama huyu kuondoka ndani ya timu ”

“Sielewi kabisa ni kwa nini watu wengi hawakumpa heshima anayo stahili ndani ya ndani ya Ufaransa "

Wafaransa bado wanaikumbuka Fainali ya Kombe la Dunia , wamemkunjia GOAT
Screenshot_20230614_152142_Instagram.jpg
 
Kylian Mbappé ameweka sawa juu ya tetesi za kuhusishwa na Madrid .

"Sijaomba kuondoka PSG wala sijaomba kujiunga na Madrid , nimeiambia Klabu kuwa sipo tayari kurefusha mkataba mpaka itakapofika June 2025 , nina furaha sana kuwa hapa kwa msimu ujao "

#DaudaSports
Screenshot_20230614_152253_Instagram.jpg
 
Siku kama ya leo Mshambuliaji Erling Haaland alijiunga rasmi na Manchester City na leo hii akiwa anatimiza mwaka mmoja haya ni sehemu ya mafanikio yake .

Ubingwa UEFA
Ubingwa FA
Ubingwa EPL
Tuzo ya Mfungaji bora

Screenshot_20230614_152400_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom