Mwanaume mmoja raia wa Ubelgiji hivi karibuni alifeki kifo chake kuona nani kati ya ndugu zake anamjali.
David Barten (45) , mkewe na watoto waliamua kushirikiana kuwalaghai ndugu na marafiki.
Ili kusambaza habari za msiba huo feki, mtoto wa David aliposti kwenye mitandao ya kijamii na kuandika ujumbe wenye kuhuzunisha juu ya kifo cha baba yake.
Wikiendi iliyopita mazishi yalipangwa kufanyika karibu na mji wa Liege, na yalihudhuriwa na ndugu pamoja na marafiki wengi waliovaa nguo nyeusi.
Kila mmoja alijawa na huzuni huku wakingojea kuwasili kwa mwili, ghafla ilikuja helikopta.
Video iliyopostiwa kwenye mtandao wa TikTok na mmoja wa waombolezaji ilimuonyesha David akishuka kutoka kwenye helikopta akifuatana na timu ya wapiga picha.
Watu wengi walishikwa na mshangao huku wengine wakilia, wakimkimbilia na kumkumbatia.
Kwa mujibu wa gazeti la The Times , David amesema alifeki kifo kuona nani katika familia yake anamjali,alikuwa akiona kila mmoja yuko kivyake, haalikwi popote na haonani na nduguze.
"Niliamua kuwapa somo, wasisubiri mtu akifa ndio wakutane naye.Sasa hivi wananijali, wananicheki kwa simu, kwahiyo mimi ndio mshindi."
View attachment 2658010