Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kwa mara ya kwanza katika historia Ndege ya Shirika la Ndege la Air France imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl Nyerere Dar es salaam na kumwagiwa maji kama ishara ya kupewa heshima kwakuwa ni mara ya kwanza inatua katika uwanja huo.

Mapokezi ya ndege hiyo yameongozwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa ambapo amesema ndege hiyo itakuwa na route za moja kwa moja mara tatu kwa wiki kutoka Ufaransa hadi Dar es salaam kupitia Zanzibar..

“Haya ni matunda ya ziara ya Rais Dkt. Samia nchini Ufaransa Mwezi February mwaka 2022 ambapo Ufaransa na Tanzania zilikubaliana kudumisha ushirikiano”
Screenshot_20230614_053126_Instagram.jpg
 
Rais wa Club ya soka ya Yanga Injinia Hersi Said @caamil_88 leo amemkaribisha rasmi kwenye Club hiyo Rais wa Wasafi Mwimbaji Staa Diamond Platnumz baada ya parade ya shangwe la kulipokea Kombe la Azam Federation, kauli ambayo ameitoa baada ya perfomance kubwa aliyoifanya Staa huyo Makao Makuu Jangwani wakati wa kupokea kombe hilo.

Rais Hersi ameweka picha yake na Diamond wakiwa wamelibeba kombe hilo na kuandika "Mwanamuziki bora Afrika katika Klabu bora Afrika, karibu diamondplatnumz katika klabu ya Wananchi, Mabingwa wa muda wote nchini Tanzania na finalist wa CAF CC, pokea ubingwa na iwe ishara ya utamaduni wa kufurahi pamoja katika mafanikio yetu"

"Leo pale Jangwani imepigwa show ya hatariiiiiiii... top performance kutoka kwa Mwamba diamondplatnumz nomaaaaa , ama hakika wananchi wamefurahi kibingwa!!!"

Siku chache zilizopita kwenye kusherehekea siku 100 za @manaratv__ Diamond Platnumz alikiri kushawishiwa na Semaji @HajisManara kuishabikia Timu hiyo aliyasema yafuatayo "Katika mambo ya kimpira hakuna asiyefahamu na hakuna ambaye atapingana na hili kwamba nguvu yako kubwa imesababisha kuongeza mwamko mkubwa katika football Nchini Tanzania”

“Wakina kama sisi sio Watu wa kujua mpira sana lakini tumekua tunapenda kufatilia mpira sana kwa sababu yako na nisiongee unafiki, ulipo nipo" alimalizia Platnumz.
Screenshot_20230614_053242_Instagram.jpg
 
Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC), limesema limepata taarifa ya Muuguzi msajiliwa wa Baraza (Jina linahifadhiwa) anayetuhumiwa kubaka Mama Mjamzito aliyefika katika Hospitali ya Wilaya ya Sikonge, Tabora kwa ajili ya kupata matibabu ambapo limelaani kitendo kicho ambacho Baraza limekitaja kuwa cha kinyama, ukatili uliopitiliza na ni kinyume na maadili ya Uuguzi na Ukunga.

Msajili wa Baraza hilo, Agnes Mtawa amesema “Baraza linatoa pole kwa Mama aliyepata madhila hayo lakini pia Baraza linawajulisha umma wa Watanzania kwamba baada ya taratibu za uchunguzi na Vyombo vya Sheria kuthibitisha Muuguzi huyu kutenda kitendo hicho, Baraza litachukua hatua za kinidhamu za kitaaluma kwa mujibu wa kifungu cha (25)(2)(c) cha Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya 2010”

“Nitoe wito kwa Wauguzi na Wakunga nchini, kutoa huduma kwa kuzingatia Utu, Taratibu, Kanuni na Sheria, kwa kuwa matendo kama haya yanaiaibisha taaluma ya Wauguzi ambao ni kiungo katika upatikanaji wa huduma bora za matibabu”
Screenshot_20230614_053351_Instagram.jpg
 
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR) imempa ushindi Mwanaharakati wa Katiba, Bob Wangwe katika kesi ya kupinga Wakurugenzi wa Halmashauri Kusimamia Uchaguzi kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Katika uamuzi huo ambao umetolewa leo mbele ya Jopo la Majaji Watano, pia Mahakama imeiagiza Serikali ya Tanzania kufanyia marekebisho vifungu vya Sheria ya uchaguzi 7(1) na 7(3).

Akiongea na Ayo Tv, Wangwe amesema “Kimsingi wamekubali kwamba vifungu vya sheria ya uchaguzi 7(1) na 7(3) katika sheria ya Taifa ya Uchaguzi vinavyoruhusu Wakurugenzi kusimamia uchaguzi vinakiuka mkataba wa Mahakama hiyo na mikataba mingine ya ya kimataifa ya haki za Binadamu kwakuwa havijaweka utaratibu wa kuwazuia Watu wenye itikadi za Vyama kutokuwa Wasimamizi wa uchaguzi na hivyo kuathiri ushiriki wa Wananchi katika kushiriki kwenye utawala wa Nchi kwakuwa pia vinaruhusu ubaguzi wa kiitikadi.

"Hivyo Mahakama imeagiza kuwa vifanyiwe marekebisho na Serikali haraka iwezekanavyo na ndani ya miezi 12 ipeleke ripoti ya utekelezaji katika Mahakama hiyo,".

Itakumbukwa kuwa May 24, 2019 Mahakama kuu ilifuta sheria iliyokuwa inawapa Wakurugenzi hao mamlaka ya kuwa Wasimamizi wa uchaguzi lakini Oktoba 17, mwaka huo huo Mahakama ya Rufani ikatengua uamuzi huo.
Screenshot_20230614_053447_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom