Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kuna watu wanajitahidi my dear, kuanzia kwenye namna ya uandishi hadi mpangilio wa matukio hadi unajikuta tu unasoma story nzima, binafsi huwa nasoma story za wale wanaoelezea maisha yao waliyopitia siyo za kutunga hizo hapana

Sasa hao niliowataja wanajitahidi sana hasa huyo wa pili kasimulia story tatu zote zinahusu maisha yake na akianzisha ni kama jf nzima inahamia kwenye uzi wake yuko vizuri sana

Hadi sister wangu kabisa naye na userious wake wote namuonaga huko huwa anacomment
Mie siku hizi hata sina mood kwakweli, hata ipangiliwe vipi.
 
Club ya Simba SC leo imezindua rasmi jezi zake mpya watakazotumia katika michuano ya Club Bingwa Afrika, jezi hizo ambazo za aina tatu za nyumbani, ugenini na third kit zina Mdhamini tofauti na Mdhamini Mkuu wa Simba M BET kwasababu ni Mshindani wa Mdhamini wa mashindano ya CAF, 1XBet.

Msemani wa Simba, Ahmed Ally amenukuliwa akisema “Jezi hizo zitauzwa Tsh. 35,000 kwa jezi moja na zitaanza kuuzwa Februari 15, 2023, Wachezaji wataanza kuvaa tukienda kucheza na Horoya”

“Tukisafiri tutakuwa na M-Bet, siku moja kabla ya mechi na siku ya mechi ndio tutakuwa tunatumia Visit Tanzania kama ilivyo matakwa ya CAF”
Screenshot_20230208_045818_OGInsta%2B.jpg
 
Boss wa Makampuni ya Marekani ya SpaceX, Tesla na Twitter, Elon Musk (51) ambaye ni miongoni mwa Matajiri wa dunia amesema kilichobaki kwenye mpango wake wa kuuleta mradi wa Starlink nchini Tanzania ni kibali tu kutoka kwenye Serikali ya Tanzania.

Tajiri huyu ameitoa kauli hii Kupitia mtandao wa Twitter Elon akimjibu Mwekezaji Mike Coudrey ambaye alimshauri kuileta Starlink Afrika Mashariki hususani Tanzania ili Watu wawe na internet ya uhakika ya kuwawezesha kupata taarifa na kuwa na kesho iliyo bora ambapo Musk alimjibu “Tungependelea hivyo, tunasubiri kibali kutoka kwenye Serikali”

Hata hivyo Waziri wa Habari, Teknolojia ya Habar na Mawasiliano Nape Nnauye ambaye Watanzania wengi walim-tag kwenye tweet hizo ili kupata kauli yake amenukuliwa akisema ——— > “Walishajibiwa siku nyingi, wana documents wanatakiwa kukamilisha ili mchakato uendelee, hawajakamilisha documents”

Kampuni ya SpaceX ya Elon imeendelea kuzindua satelaiti katika Nchi mbalimbali kama sehemu ya mradi wa Starlink ambao unalenga kutoa huduma ya internet ya kasi ya juu zaidi kutoka anga za juu hadi maeneo ya mbali Duniani na huwasaidia hadi Watu wanaoishi maeneo ya mbali ambayo hayawezi kupata internet ya kasi ya juu zaidi.
Screenshot_20230208_050040_OGInsta%2B.jpg
 
Huu ni muonekano wa maendeleo ya ujenzi wa reli ya SGR Sehemu ya Morogoro-Makutupora ambao umefikia asilimia zaidi ya 90 kwa sasa.

Gharama ya mradi ni USD 1,923,695,000 sawa na Tsh.Trilioni 4.4 ambapo mradi upo chini ya Mkandarasi Yapi Merkezi.

Mradi umesainiwa Sept 29, 2017 na umeanza kutekelezwa Feb 26, 2018 ambapo unatakiwa kukamilika February 20,2023.
Screenshot_20230208_050631_OGInsta%2B.jpg
 
Watu tisa Wilayani Nyang’hwale Mkoani Geita wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kulima bangi katika eneo la Msitu wa Hifadhi ya Mienze iliyopo Kijiji cha Wavu Wilayani humo, Watu hao wamekamatwa kufuatia operesheni inayofanywa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Polisi pamoja na Idara ya Misitu ambapo tayari mashamba yenye hekari zaidi ya sita yaliyolimwa bangi yameteketezwa.

Akizungumza wakati wa uteketezwaji wa mihadarati hiyo DC wa Nyang'hwale, @officialkingalamegrace amesema hayupo tayari kuona baadhi ya Watu wakifanya biashara ya kulima bangi Wilayani humo na kuwataka wenye tabia hiyo kuacha mara moja.

DC Kingalame amelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha Watendaji wanakuwa salama wanapotekeleza majukumu yao na wahakikishe wanafanya doria kwa kukomesha uhalifu.

Kwa upande wake Afisa Misitu wa Wilaya ya Nyanghwale Asafu Manya amesema taarifa za uwepo wa mashamba katikati ya msitu huo zimetolewa na Wasamaria wema na kuitaka Jamii kuacha kuingia maeneo ya misItu na kufanya uharibifu wa mazingira kwakuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.
Screenshot_20230208_050829_OGInsta%2B.jpg
 
Club ya Yanga SC imeondoka kuelekea Tunisia kwa ajili ya kuanza mchezo wake wa kwanza wa hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika US Monastir.

Afisa Habari wa Yanga Ally Kamwe amesema Timu itaondoka na kikosi cha Wachezaji 25, Aboutwalib Mshery atasafiri na Timu kwa ajili ya kwenda Tunisia kupatiwa matibabu wakati Bernard Morrison atabaki Dar es Salaam akitibiwa nyonga.

“Tuna Wachezaji 25 katika kikosi chetu lakini hawa 25 yupo pia Aboutwalib Mshery, Mshery anakwenda Tunisia kwa ajili ya matibabu”
Screenshot_20230208_051203_OGInsta%2B.jpg
 
Al Hilal ya Saudi Arabia imetinga fainali ya Klabu bingwa dunia baada ya kumwondosha Flamengo kutoka nchini Brazil, Wababe hao wa Mashariki ya kati wanamsubiri mshindi kati ya Real Madrid na Al Ahly.
Screenshot_20230208_051354_OGInsta%2B.jpg
 
Manchester City wanafikiria kuwasiliana na Lord Pannick KC ambaye ni moja kati ya Wanasheria wa Borris Johnson ili akasimame kwa niaba yao kwenye kesi dhidi ya Premier League.

Gwiji huyo hutoza Pauni 5,000 kwa saa moja na Pauni 80,000 kwa siku moja.
Screenshot_20230208_051626_OGInsta%2B.jpg
 
“Niushukuru uongozi wa Simba kwa namna walivyotupokea. Tumeridhis kutokana na mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo wanashiriki ikiwa ni timu pekee kutoka Tanzania. Tumekubali kabisa kuitangaza nchi yetu kimataifa.”

- Allen Mushi, Meneja Masoko M-Bet
Screenshot_20230208_051728_OGInsta%2B.jpg
 
Kasism Dewji MAESTAAFU, HAJAJIUZULU. Hivyo ni vitu viwili tofauti ambavyo watu wanachanganya.

Kujiuzulu ni kuachilia nafasi ya uongozi unayoitumikia/unazozitumikia kabla ya muda wa kustaafu haujafika au kabla ya muda ukomo wa kuitumikia nafasi hiyo/hizo.

Kustaafu ni kuamua kutojihusisha tena na kazi/uongozi fulani hata kama watu/taasisi bado inahitaji huduma yako.

Kassim Dewji amestaafu masuala ya uongozi na ataendea kubaki kuwa mwanachama. Pengine labda uongozi ungeamua kumteua kwenye kamati mbalimbali za Simba, kwa hiyo kustaafu kwake maana yake anataka viongozi wasimfikirie kwenye nafasi yoyote.
Screenshot_20230208_052037_OGInsta%2B.jpg
 
“Ukitaka kuchukua ubingwa wa Tanzania lazima ushindane kama wanaochukua ubingwa wanavyoshindana! Huu ni ushauri kwa Azam na timu nyingine zinazotaka ubingwa.”

“Ukishindana unavyojua wewe utaishia kufukuza makocha na kila wakati utasajili wachezaji wapya.”

- Amri Kiemba via #HiliGame on @cloudsfmtz

——————————————-

“Lazima ujue ratiba ipoje, ujue waamuzi gani watakao chezesha na waamuzi gani unataka wachezeshe mechci zako.”

“Mechi zako na wewe zichezwe dakika 99 kama matokeo sio mazuri kwako, waamuzi wakikosea iwe timu yako ndio inanufaika sio inaathirika.”

- Alex Luambano via #HiliGame on @cloudsfmtz
Screenshot_20230208_052141_OGInsta%2B.jpg
 
“Bernard Morrison amepata shida ya ‘groin’ kwa mujibu wa vipimo alivyofanyiwa, atakuwa nje ya uwanja kwa muda miezi miwili. Kwa hiyo hayupo kwenye safari ya Tunisia.”

“Atafanyiwa matibabu hapahapa Tanzania kwa muda wote atakaokuwa nje ya uwanja, kwa kuwa daktari alishauri Mshery afanyiwe upasuaji ndio maana amejumuishwa kwenye safari ya Tunisia kwa sababu atafanyiwa upasuaji akiwa huko.”

- Ally Kamwe, Afisa Habari Yanga.
Screenshot_20230208_052235_OGInsta%2B.jpg
 
“Timu zetu [Tanzania] bado hatujafikia hatua ya kuwa mabingwa wa mashindano ya Afrika kutokana na aina ya vikosi vya timu zetu.”

“Ukiangalia Simba ambao wamekuwa wakishindana vizuri kwenye michuano ya Afrika hivi karibuni, utaona ni kama bado wanatengeneza timu yao.”

“Ile timu iliyokuwa inashindana haipo tena baada ya wachezaji wengi kuondoka [Okwi, Miquissone, Lwanga, Dilunga, Kagere, Mugalu, Wawa, n.k] kwa sababu tofauti ikiwa ni umri, viwango n.k. Wachezaji wachache wamebaki ambao bado wana uwezo wa kutoa mchango ambao walikuwa wanautoa misimu mitatu nyuma.”

“Wana wachezaji wengi wapya ambao wamekuja ukiwa ni mpango wa kuandaa timu, hata Simba inavyocheza mechi za Ligi bado sio timu imara.”

“Ina wachezaji wenye madaraja ya juu ambao leo wanaweza wakacheza na timu kushinda kwa magoli 7 lakini mechi inayofuata wakapambana utafuta goli moja.”

“Bado haina mwendelezo wa kiwango ambacho imekuwa ikikionesha, kwa hiyo Simba ina wachezaji wazuri lakini bado hawana timu imara.”

“Yanga wana timu imara, wachezaji wengi hawapo kwenye kiwango kizuri kwa wakati husika. Wanacheza na kupata ushindi ndio maana kwenye Ligi yetu kwao kushinda sio habari tena haijalishi wamechezaje au wamepanga kikosi gani.”

“Kwa timu zetu kutoka hatua ya makundi kwenda hatua inayofuata inawezekana. Hatua ambazo watu wanaziota [Nusu Fainali, Fainali na Ubingwa] zinahitaji miujiza ya soka kuzifikia.”

- Amri Kiemba
Screenshot_20230208_052613_OGInsta%2B.jpg
 
Nyota Christian Atsu aliyenasa chini ya kifusi kufuatia tetemeko la ardhi nchini Uturuki amepatikana akiwa hai baada ya shughuli za uokoaji kufanyika kwa zaidi ya saa 20.
Screenshot_20230208_052904_OGInsta%2B.jpg
 
Kutokana na uamuzi huu wa CAS wa kupindua adhabu ya Man City kutoshiriki UEFA kwa misimu miwili basi kuna shida sehemu, kama City hana makosa kwanini apigwe tu faini? Na kama ana makosa sheria haisemi apigwe faini bali afungiwe, naamini kuna shida sehemu.

- Jose Mourinho, aliyasema haya Julai 2020 na taratibu yanakuja kutimia 2023.
Screenshot_20230208_053028_OGInsta%2B.jpg
 
Kwa mujibu wa sheria za Premier League, adhabu yoyote ambayo Manchester City watapewa baada ya tume huru kujiridhisha basi hawapaswi kwenda CAS ambapo ikumbukwe ndipo walipopona kwenye kesi iliyopita dhidi ya UEFA.
Screenshot_20230208_053134_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom