Makapuku Forum

Makapuku Forum

Haha si nimefichwa na wewe

Mi naonaga mnafanana tu asee

Ujue binafsi kuna makabila baadhi ya watu wake nikiwaona tu kwa mara ya kwanza, naweza kuhisi huyu atakuwa kabila fulani na unakuta asilimia kubwa inakuwa kweli, mfano wanyakyusa, wachagga, wamasai, waluo, nk kutokana na kwamba wengi wanafananafanana
Wanyakyusa sababu ya pua au?
Kweli wachaga, wambulu na wamasai wako na sura zao.
 
Haha si nimefichwa na wewe

Mi naonaga mnafanana tu asee

Ujue binafsi kuna makabila baadhi ya watu wake nikiwaona tu kwa mara ya kwanza, naweza kuhisi huyu atakuwa kabila fulani na unakuta asilimia kubwa inakuwa kweli, mfano wanyakyusa, wachagga, wamasai, waluo, nk kutokana na kwamba wengi wanafananafanana
Kwahiyo auntie wangu ye ni wa wapi eti zoo
 
Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imetoa ufafanuzi kuhusu picha na taarifa inayosambaa katika Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii yenye kichwa cha habari 'Uwanja wa Mkapa Unaanza Kutia Aibu’ ambapo imesema picha zinazotumika pamoja na ujumbe ho ni picha ambazo zilichukuliwa siku za nyuma (mara baada ya tukio la Mkesha lililofanyika tarehe 16/12/20 katika uwanja
huo).

“Kufuatia hali hiyo iliyojitokeza wakati huo, Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ilichukua hatua mbalimbali ili kuhakikiksha kuwa hali hiyo haijitokezi tena ambapo Wizara ilifanya mabadiliko ya Menejimenti ya Uendeshaji wa Uwanja huo”

“Wizara pia kwa kushirikiana na Bodi ya Ligi ambayo ndiyo Mdau mkubwa imeandaa muongozo wa matumizi wenye lengo la kudhibiti masuala ya usafi, Wizara imeunda pia kikosi kazi kidogo cha usafi na mazingira ambacho kinafanya ukaguzi wake kabla na baada ya uwanja kutumika ili kuimarisha usafi na Wizara limuelekeza Mzabuni wa uwanja huo kuboresha huduma ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vibarua wa usafi wakati wa matukio”

“Wizara inatoa rai kwa Wadau wa michezo na umma wote wa Watanzania kushirikiana katika kuvitunza viwanja vyote kwa kuzingatia usafi wakati wa matumizi yake na kujiepusha na aina
yoyote ya uharibifu”
Screenshot_20230206_184752_OGInsta%2B.jpg
 
Moja kati ya habari kubwa tulizoanza nazo mwaka huu ni huduma ya kuwekewa puto tumboni kwa ajili ya kupunguza uzito ambayo inatolewa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila na tayari Mwimbaji Peter Msechu @peter_msechu amebainisha kupungua kilo saba, siku 7 tu baada ya kuwekewa puto katika Hospitali hiyo ili kumsaidia kupunguza uzito mwilini mwake.

@ayotv_ imefika hadi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili - Mloganzila na kupata fursa ya kuona Mtu akiwekewa puto pamoja na kuongea na Madaktari ambao wameelezea mengi tusiyoyafahamu kuhusu huduma hiyo.

“Gharama za kuwekewa puto ni Tsh. Milioni 4.2 na tayari tumeshawawekea Watu 34 wakiwemo Watu maarufu ambao wengine hawajataka kujitangaza”

Madaktari wanasema ukiwekewa puto likiwa tumboni unaweza kufanya mazoezi na sarakasi nyingine zozote ila hautoruhusiwa kunywa bia na soda kwakuwa ukinywa vinaathiri puto na linaweza kupasuka… kuitazama video hii kwa urefu ingia Youtube ya MillardAyo.
Screenshot_20230206_184904_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali imesema hapa nchini kuna takribani Marubani 106 kati ya hao Marubani 11 ni Wanawake na 95 ni Wanaume na hao Wanawake wana uwezo wa kurusha ndege zote.

Kati ya hao 106, Marubani 105 wote ni Watanzania na mmoja tu ndio ambaye si Mtanzania, takwimu hizo zimetolewa Bungeni Dodoma leo February 6, 2023 wakati wa kipindi cha maswali na majibu ambapo Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete amejibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum, Angelina Adam Malembeka ambaye alitaka kujua hadi sasa Tanzania kuna Marubani wangapi.
Screenshot_20230206_185029_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom