Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220905-052650_Opera%20Mini.jpg
 
STARS KUPINDUA MEZA KIBABE
.
Baada ya kupoteza mechi ya kwanza ya mtoano nyumbani ikifungwa 1-0 dhidi ya Uganda, Taifa Stars leo saa 10 jioni itahitaji kupindua meza kwenye mchezo wa marudiano kuwania kufuzu CHAN ikihitaji ushindi wa mabao mawili au zaidi kufuzu.
.
TFF ilimtimua kocha mkuu, Kim Poulsen baada ya kupoteza mechi ya kwanza na Uganda kisha kumteua Mzambia Honour Janza kuwa kocha mkuu akisaidiwa na manahodha wa zamani wa Stars Mecky Mexime.
.
Stars inahitaji kufuzu fainali hizo kwa mara ya tatu baada ya kufanya hivyo mara mbili mwaka 2009 na 2020.
.
Kila la kheri @taifastars_ View attachment 2346016
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Binamu nimekumiss
Nimekumiss sana pia aunt, mambo yanapandana sana, niko site kule nnakosema lakini inabidi niongeze juhudi

Ujue nini binamu, vipengele unavyoweka hapa vinalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.

Afu haihusiani, lini unamuacha anko wangu Lee sababu siku hizi kawa mlevi anasema sababu ni wewe
 
Mahakama ya Juu nchini Kenya imeidhinisha Uchaguzi wa William Ruto kuwa Rais Mteule wa Kenya baada ya kesi iliyowasilishwa na Mpinzani wake katika Uchaguzi huo Raila Odinga kukosa ushahidi wa kutosha.

Majaji wa Mahakama hiyo walioongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome wamesema ushahidi uliotolewa na Raila Odinga ulikuwa umejaa uvumi na porojo, Jaji Martha Koome amesema Ruto alifanikiwa kupita kikwazo cha kura 50% na moja ya kikatiba.

Martha Koome amesema kura zilizokataliwa haziwezi kujumlishwa katika hesabu ya kumtafuta aliyeibuka mshindi na kusisitiza kwamba mbinu iliyotumika na Tume ya Uchaguzi kupata asilimia 64.4 ya Wapiga kura ilikuwa sahihi.

Itakumbukwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) Wafula Chebukati, alimtangaza Dkt Ruto kuwa Rais mteule baada ya kupata kura Milioni 7,176,141 ( 50.49%) dhidi ya Milioni 6,942,930 za Odinga ( 48.85%) ), Prof George Wajackoyah wa Roots Party alipata kura 61,969 (0.44%) huku David Mwaure Waihiga wa Agano Party akiibuka wa nne kwa kura 31,987 ( 0.23%).
Screenshot_20220905-140830_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi nchini Canada inawasaka Washukiwa wawili katika tukio ambalo Watu kumi wameuawa kwa kuchomwa kisu na wengine karibu 15 kujeruhiwa katika eneo moja la jamii ya kiasili lisilo na wakaazi wengi.

Mauaji hayo ya Watu wengi ndio makubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya sasa nchini Canada, Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema mashambulizi hayo katika eneo la Saskatchewan ni ya kutisha na ya kuvunja moyo.

Polisi imewataja Washukiwa wawili Damien Sanderson mwenye umri wa miaka 31, na Myles Sanderson mwenye umri wa miaka 30, na kutoa picha zao na maelezo lakini hakuna taarifa zaidi kuhusu nia yao wala kuhusu wahanga, Polisi ya Saskatchewan imesema inaonekana kuwa baadhi ya Wahanga huenda walilengwa na wengine walishambuliwa bila mpangilio.
Screenshot_20220905-140934_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Abiria na Wananchi mbalimbali aliosafiri nao kwa Meli ya M.V Kilimanjaro 4 alipokuwa akiondoka katika Bandari ya Malindi Zanzibar akielekea Jijini Dar es Salaam leo tarehe 05 Septemba, 2022.
Screenshot_20220905-141026_OGInsta%2B.jpg
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amesema Chama hicho kinaridhishwa na mwenendo wa ujenzi wa Daraja la Magufuli linalounganisha kati ya Mkoa wa Mwanza na Geita ambalo linajengwa eneo la Kigogo-Busisi.

Akizungumza wakati akikagua Daraja hilo Kinana ambaye yupo katika ziara ya kukagua uhai wa Chama na kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, amesisitiza Daraja hilo ujenzi wake unakwenda kwa wakati kama ilivyopangwa, hivyo mwaka 2024 nchi itakuwa imepata alama kubwa ya kuwa na Daraja refu lenye urefu wa karibu kilomita 3.2.

“Najaribu kukumbuka madaraja mangapi katika Afrika yenye urefu huo kama hili halitwakua la kwanza basi litakuwa katika tatu bora, hivyo niwapongeze wote wanaoshiriki ujenzi wa daraja hili ndugu zetu wa kutoka Korea, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wajenzi kutoka Kampuni ya China na Watanzania wote wanaoshiriki”

Kinana akiwa kwenye Daraja hilo baada ya kulikagua na kupata maelezo ya ujenzi wake ambao umefikia asilimia 51, amepata nafasi ya kuwasilimia Wajenzi wa Daraja hilo na kuwapongeza kwa kazi nzuri “Mnafanya kazi nzuri sana, mnafanya kazi kubwa na Rais (Samia Suluhu Hassan) ametumina nije niwasalimie na niwambie kwamba anangojea aje kuwa Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa daraja hili litakapokamilika”
Screenshot_20220905-141131_OGInsta%2B.jpg
 
Nimekumiss sana pia aunt, mambo yanapandana sana, niko site kule nnakosema lakini inabidi niongeze juhudi

Ujue nini binamu, vipengele unavyoweka hapa vinalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.

Afu haihusiani, lini unamuacha anko wangu Lee sababu siku hizi kawa mlevi anasema sababu ni wewe
 
Club ya Azam FC imemtangaza Denis Lavagne (58) Raia wa Ufaransa kuwa Kocha wao Mkuu na sasa anarithi mikoba ya Abdihamid Moalin.

Lavagne ana leseni ya juu ya Ukocha ya UEFA (UEFA Pro Licence) na ana uzoefu mkubwa wa soka la Afrika ngazi ya Club na Timu za Taifa.

Denis Lavagne amewahi kufundisha soka vilabu mbalimbali lakini soka la Afrika ana uzoefu nalo kwa miaka zaidi ya 14 sasa toka alipoanza Coton Sport ya Cameroon (2007-2011), Cameroon (2011-2012), na mara ya mwisho 2021 alikuwa anaifundisha USM Alger ya Algeria.
Screenshot_20220906-052206_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Mteule wa Kenya Dr. William Ruto leo amehutubia Taifa hilo ikiwa ni mara ya kwanza baada ya Mahakama nchini humo kumtaja kuwa Mshindi katika kesi ya kupinga matokeo ya Urais iliyokuwa imefunguliwa na Muungano wa Azimio la Umoja ukiongozwa na Mgombea Urais Raila Odinga.

Katika hotuba yake isiyopungua dakika 40 ambayo tayari ipo kwenye Youtube ya millardayo (link kwenye bio), Ruto huku akicheka alisema hajaongea na Rafiki yake mpendwa Rais Uhuru Kenyatta kwa miezi mingi lakini atampigia simu hivi karibuni ili wafanye mazungumzo ya kukabidhiana madaraka.

"Nafahamu alifanya bidii sana kwa namna yake lakini Wakenya wamefanya maamuzi ya chaguo lao ambapo hata hivyo hatuna shida na maamuzi yoyote ya kidemokrasia yanayofanywa na Mkenya yoyote" —— amesema Dr. William Ruto,
Screenshot_20220906-052312_OGInsta%2B.jpg
 
Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC), imeishauri Serikali kuharakisha mchakato wa utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuhamisha umiliki wa Ndege 11 kutoka Wakala wa Ndege za Serikali(TGFA) kwenda Shirika la Ndege(ATCL) ili kuondokana na tatizo la kuwa na mtaji hasi wa Tsh.Bilioni 239.

Katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) ya mwaka 2020/21, alibaini ATCL ina madeni makubwa kushinda mali zake.

Akitoa agizo hilo leo September 5 2022 baada ya kukutana na TGFA na ATCL, Mwenyekiti wa PIC, Jerry Silaa amesema Ndege hizo 11 zina thamani ya Tsh.Trilioni 1.47 hivyo mali hizo zikihamishwa itasaidia kuondokana na kuwa na mtaji hasi na gharama kubwa za ukodishaji ili ATCL ipate faida
Screenshot_20220906-052424_OGInsta%2B.jpg
 
Mvulana mmoja mwenye umri wa miaka 13 amefariki baada ya kulishwa sumu na Mama wa Mwanafunzi mwenzake baada ya kumshinda katika masomo Shuleni eneo la Mji wa Pwani wa Karaikal Kusini mwa India.

Bala Manikandan ambaye alikuwa ni Mwanafunzi wa Darasa la 8, alishika nafasi ya kwanza katika masomo na shughuli za ziada Shuleni, jambo lililomkwaza Mama wa Mwanafunzi mwenzake ambaye kwa sasa amekamatwa kwa tuhuma za mauaji.

Siku ya Ijumaa, Mshukiwa aliyetambulika kwa jina la Sahayarani Victoria, alidaiwa kujifanya Mama Mzazi wa Bala na kwenda kumfuata katika mlango wa Shule hiyo na kumkabidhi Kijana huyo chupa iliyokuwa na kinywaji.

Kijana huyo alikuwa akijiandaa kutumbuiza kwenye hafla ya kitamaduni ya siku ambayo hufanyika kila mwaka katika shule hiyo na ndipo alipokunywa kinywaji hicho ambapo muda mchache akaanza kujisikia vibaya, kutapika kabla ya kufariki jumamosi usiku.

Wazazi wa Bala waliwasilisha malalamiko katika Kituo cha Polisi cha eneo hilo baada ya kanda ya CCTV kumuonesha Victoria akimwomba Mlinzi ampelekee mvulana huyo chupa hizo, Madaktari wamesema Mvulana huyo alifariki kutokana na kukosa hewa baada ya chembechembe za chakula kuingia kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Screenshot_20220906-052534_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali imetangaza msamaha wa kutoshtakiwa kwa Mtu yeyote ambaye atasalimisha silaha anayoimiliki isivyo halali kwa masharti ya kwamba msamaha unaanza September 01, 2022 hadi October 31, 2022 na utafanyika katika Vituo vya Polisi, Ofisi za Serikali za Mitaa au Vijiji na kwa Watendaji wa Kata na Mtu yeyote atakayepatikana na silaha baada ya muda huo wa msamaha kuisha watachukuliwa hatua.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Jumanne Abdallah Sagini leo September 05, 2022 Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa kampeni maalumu ya kusalimisha silaha haramu kwa hiari.

Sagini amesema wapo baadhi ya Watu wanamiliki silaha za Ndugu zao ambao wamefariki, wengine wanamiliki silaha kihalali lakini afya zao au umri wao hauwawezeshi tena kuendelea kuhimili matumizi ya silaha hivyo amewaomba nao pia kusalimisha silaha hizo.
Screenshot_20220906-052654_OGInsta%2B.jpg
 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewataarifu Wateja wake wa malipo ya awali (LUKU) kuwa kutakuwa na matengenezo kinga kwenye kanzi data ya mfumo wa manunuzi ya umeme (LUKU) kwa siku nne kuanzia Jumatatu September 12 hadi September 15,2022.

Wateja wataweza kununua umeme wakati wote isipokuwa wakati wa matengenezo kwa vipindi vifupi nyakati za usiku kama inavyoonekana kwenye jedwali (ukiswipe).

“Shirika linawashauri Wateja kununua umeme wa ziada au kufanya manunuzi ya umeme nje ya muda uliotajwa ili kuepuka usumbufu” ——— imeeleza taarifa ya TANESCO.
Screenshot_20220906-052910_OGInsta%2B.jpg
 
Kundi la Wafugaji na Wakulima limevamia kambi ya Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) na kusababisha mauaji ya Watu wawili na majeruhi sita katika msitu wa Makere Kusini Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma.

Kundi hilo linatajwa kuondolewa katika Hifadhi hiyo kutokana na kuendesha shughuli za kibinadamu ambapo mpaka sasa Watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi ambapo pia katika tukio hilo uharibifu wa mali mbalimbali ikiwemo trekta, pikipiki na nyumba ulifanyika.

RPC Kigoma ACP. Filemon Makungu amesema wawili ambao wamefariki katika uvamizi huo ni Wananchi wa Kijiji cha Mvinza ambao walikuwa ni vibarua katika kazi ya kuotesha na kupanda miti na wametambulika kwa majina ya Thomas Alfred (53) na Salvatory (50).

Wananchi wa Kijiji cha Mvinza wamesema eneo ambalo linatajwa kama Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini ni la kwao na wamekuwa wakilitumia kwa kilimo na ufugaji tangu mwaka 1956.

Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Msitu wa Mkere Kusini Deogratius Kavisha kutoka TFS amesema eneo hilo ni Hifsdhi ya Taifa ya Misitu lenye ukubwa wa hekta 65178 ambalo kwa sasa linaendelea kupandwa miti kutokana na kuharibiwa na Wakulima na Wafugaji.
Screenshot_20220906-053021_OGInsta%2B.jpg
 
Mgombea Urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Kenya mwaka 2022 kwa tiketi ya Azimio la Umoja Raila Odinga amesema anaheshimu uamuzi wa Mahakama uliomuidhinisha Ruto kuwa Rais Mteule Kenya lakini amesema licha ya kuuheshimu hakubaliani na uamuzi huo wa Mahakama.

Katika taarifa yake aliyoitoa leo Jumatatu, September 5,2022, Odinga amewataka Wafuasi wake kudumisha utulivu “Tumezingatia uamuzi wa Mahakama ya Juu kuhusu uchaguzi wa Urais uliofanyika tarehe 9 Agosti 2022, siku zote tumesimama kutetea utawala wa sheria na katiba, katika suala hili, tunaheshimu uamuzi wa Mahakama ingawa hatukubaliani na uamuzi wa Mahakama wa
leo”

“Mawakili wetu walitoa ushahidi usiopingika na ukweli ulikuwa upande wetu, kwa bahati mbaya, Majaji waliona vinginevyo, tunaona ni ajabu kwamba Majaji walitoa maamuzi dhidi yetu kwa sababu zote tisa pamoja na sababu za kutumiwa kwa lugha kali kupita kiasi katika kukataa madai yetu.

“Uamuzi huu si mwisho wa harakati zetu, kwa hakika, inatutia moyo kuongeza juhudi zetu za kubadilisha nchi hii kuwa demokrasia yenye ustawi ambapo kila Mkenya anaweza kupata ukamilifu wake, tunawashukuru Wafuasi wetu na Wakenya kote nchini kwa kusimama nasi, tutakuwa tukiwasiliana katika siku za usoni kuhusu mipango yetu ya kuendeleza mapambano ya uwazi, uwajibikaji na demokrasia”
Screenshot_20220906-053117_OGInsta%2B.jpg
 
Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Wilaya ya Igunga, Ally Hemed amesema moja kati ya changamoto kubwa iliyojitokeza Wilayani humo kwa baadhi ya maeneo ni Makarani wa Sensa kukutana na vitendo vya kishirikina ambapo walipokuwa wakienda kwenye makazi au nyumba wanakutana na miti au vichaka badala ya kuona makazi halisi.

“Baada ya kuonesha dhahiri jambo hili litaathiri zoezi la Sensa, Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa Igunga ambaye ni Mkuu wa Wilaya, Sauda Mtondoo alifunga safari kwenda kuonana na Wazee Wilayani humo na kuelezea kadhia hiyo ndipo wakatoa baraka zao na baadaye Makarani walipokuwa wakienda kufanya kazi hiyo ya Sensa walikuta makazi na kuwakuta Watu halisi badala ya vichaka na miti”

Mkuu huyo wa Wilaya ya Igunga amesema tukio hilo liliwapa somo na kujua umuhimu wa kuonana na Viongozi wa kimila na Wazee kabla ya kufanya chochote.

Kwa upande wa Wilaya ya Tabora Mjini changamoto ilikuwa ni Mtemi wa Jamii inayoishi kwenye Hifadhi ya Igombe iliyopo jirani na Kijiji cha Ikomwa kuzuia Watu wake wasikubali kuhesabiwa jambo ambalo Mkuu wa Wilaya hiyo Paul Chacha alifika kuongea naye ndipo akakubali kuwaondoa Watu wake ndani ya Hifadhi ili kusogea Kijiji jirani na kuhesabiwa.
Screenshot_20220906-053239_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati, January Makamba, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwenye Mkutano wa Viongozi wa Dunia unaojadili Programu ya Afrika ya kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Africa Adaptation Summit) unaofanyika Rotterdam, Uholanzi leo tarehe 5/9/2022.

Mkutano huo unalenga kushawishi Washirika wa Maendeleo, Taasisi za Kifedha na Sekta binafsi na marafiki wa Afrika kuchangia fedha kwenye Programu hiyo ya Afrika ambayo inahitaji Dola za Marekani Bilioni 25 ifikapo 2025, Benki ya Maendeleo ya Afrika imechangia Dola za Marekani Bilioni 12.5.

Mkutano huu unafanyika kama sehemu ya maandalizi ya mkutano wa 27 Nchi Wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya Tabianchi ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba mwaka huu huko Sharm El Sheik Mistri ambako suala la kuhimili mabadiko ya Tabianchi kwa Afrika ni moja ya agenda muhimu ya mkutano huo.

Katika Mkutano Waziri wa Nishati amekutana na Viongozi wa Dunia, Wakuu wa Taasisi na Mashirika mbalimbali na kujadiliana nao fursa mbalimbali ikiwa pamoja na namna bora ya Tanzania kunufaika na Mpango huo wa AFRICA ADAPTATION ACCELERATION PROGRAM (AAAP) ambao utaharakisha mipango ya nchi katika kukabiliana na majanga yakiwemo UVIKO19, ukame, njaa, ajira kwa vijana na mafuriko.

Mkutano huo uliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Senegal na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika pamoja Mhe. Macky Sally, na Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa pia Mwenyekiti wa Kituo cha kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (GCA) Ban Ki-Moon.
Screenshot_20220906-053400_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom