Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa mchakato wa makabidhiano ya madaraka kwa utawala mpya yanaendelea huku akisisitiza kuwa yatakuwa ya amani.

Katika hotuba yake ambayo ameitoa leo Jumatatu Septemba 5, 2022 jioni baada ya Mahakama ya Juu kuthibitisha matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Rais mteule William Ruto, Rais Kenyatta amesema maagizo yote ya kuwezesha mchakato huo wa kukabidhiana madaraka yameshatolewa.

"Nia yangu ni kusimamia makabidhiano ya amani kwa utawala ujao na maagizo yote muhimu ya kuwezesha mchakato huu tayari yametolewa" amesema Kenyatta wakati akitoa hutuba yake ya kwanza hadharani tangu uchaguzi ufanyike.

Rais huyo ambaye wakati wa kampeni za uchaguzi huo uliofanyika Agosti 9 mwaka huu alikuwa anamuunga mkono Odinga, amesema anaheshimu uamuzi wa Mahakama ya Juu wa kuidhinisha ushindi wa Ruto kama Rais mteule.

“Nilipoapishwa kuwa Rais, niliahidi kuheshimu sheria. Leo Jumatatu Mahakama ya Juuu imeidhinisha matokeo ya urais kama yalivyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC). Ninaheshimu uamuzi wa Mahakama” amesema

Wakati wa hotuba yake, Rais Kenyatta hakumtaja kwa jina Rais mteule William Ruto wala kumpongeza kwa ushindi wake lakini aliwapongeza Wakenya kwa kudumisha amani wakati wote wa mchakato wa uchaguzi na wakati matokeo yalipopingwa mahakamani.
Screenshot_20220906-053827_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema Tanzania inahitaji dola 150 milioni za Marekani (Sh345 bilioni) kwa mwaka kujenga uwezo wa kukabiliana na athari za mabadili-ko ya tabianchi.

Makamba amesema fedha hizo zinatakiwa kutumi-ka kujenga uwezo katika sekta ya kilimo, afya, miundombinu, nishati na maji hivyo kuziomba nchi zilizoendelea na wabia wa maendeleo kufadhili mchakato huo.

Amesema hayo leo Jumatatu, Septemba 5, 2022 katika mkutano wa viongozi wa dunia unaojadili Programu ya Afrika ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Africa Adaption Summit) unaofanyika Rotterdam nchini Uholanzi.

“Nina furaha kuwa Kituo cha Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi Duniani (GCA) na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) zimeungana kuiendeleza Programu ya Kuharakisha Afrika Ina-kabiliana na Majanga (AAAP) ya mabadiliko ya ta-bianchi ukiwamo Uviko-19, ukame, ukosefu wa ajira na mafuriko,” amesema.
Screenshot_20220906-053954_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi amemteua Ali Abdalla Ali kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa leo leo Jumatatu, Septemba 5, 2022 na Katibu Mkuu Kiongozi Zena Said, imesema uteuzi huo unaanza leo.

Kabla ya uteuzi huo, Ali alikuwa Ofisa Mwandamizi ofisi ya Rais.

Uteuzi huo umekuja siku chache baada ya aliyekuwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Ahmed Khamis Makarani kujiuzulu nafasi hiyo.

Makarani alijiuzulu kutokana na kauli ya Rais Mwinyi kuitaka mamlaka hiyo ijitathmini baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Agosti 27, 2022 iliyobainisha ubadhirifu wa fedha za umma unaofanywa na watendaji lakini taasisi hiyo haichukui hatua.

Screenshot_20220906-054046_OGInsta%2B.jpg
 
Zikiwa zimepita wiki mbili tangu Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema afariki dunia, chama hicho kimeanza mchakato wa kujaza nafasi yake.

Tayari imetangaza Ijumaa, Septemba 9, 2022, kikao cha sekretarieti kitafanyika ili kumpata atakayekaimu nafasi hiyo wakati mkutano mkuu ukiandaliwa.

Mwenyekiti mpya atapatikana kwenye mkutano mkuu baada ya kupigiwa kura na wajumbe wengi wa mkutano huo. Tarehe ya mkutano huo itatangazwa baadaye baada ya sekretarieti kufanya maandalizi.

Mrema alifariki Jumapili, Agost 21, 2022, saa 12.15 asubuhi, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam. Amekuwa mwenyekiti wa chama hicho tangu alipojiunga nacho mwaka 1999 akitokea NCCR Mageuzi.

Akizungumzia mchakato huo leo Jumatatu, Septemba 5, 2022, Katibu Mkuu wa TLP, Richard Lyimo amesema mwenyekiti mpya atapatikana kwenye mkutano mkuu lakini sasa ameitisha kikao cha sekretarieti kwa ajili ya kukaimisha nafasi hiyo.

Screenshot_20220906-054200_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi amesema ipo haja Ofisi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Zanzibar na Tanzania Bara kushirikiana ili kudhibiti taasisi za Muungano katika upotevu wa fedha.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Septemba 5, 2022 Ikulu wakati akizungumza na CAG wa Tanzania, Charles Kichere aliyefika ofisini kwake kujitambulisha ambapo amesema licha ya taasisi hizo kuanza kushirikiana, bado kuna kazi kubwa ya kufanya.

Amesema kuna matatizo makubwa katika idara ya uhamiaji Zanzibar ambapo kuna wakati ulifanyika ukaguzi maalumu na kukutwa fedha nyingi zimepotea kwa kipindi kifupi.

“Kuna wakati ilitumwa kamati kwenda kufanya ukaguzi maalumu na kugundua kiasi cha Sh8 bilioni zilikuwa zimepotea ndani ya miezi sita, bado kuna kazi ya kufanya,” alisema Dk Mwinyi.
Screenshot_20220906-054323_OGInsta%2B.jpg
 
Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu (LHRC), kimefungua shauri la kupinga tozo za miamala ya kielektroniki, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam dhidi ya Waziri wa Fedha na Mipango na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Felista Mauya akizungumza na Mwananchi Digital, leo Jumatatu Septemba 5, 2022 amesema shauri hilo limefunguliwa Septemba 1, 2022 na kupewa namba 42/2022.

Amesema LHRC imeomba Mahakama kuweka zuio la muda (temporary Injection) kuendelea kutumika kwa kanuni hizo hadi kesi ya msingi itakapofika mwisho.

Amesema kwa upande wake Serikali imeomba Mahakama kuipa siku 14 kujibi hoja za mleta maombi ambapo majibu hayo yatawasilishwa Septemba 14, 2022.
Screenshot_20220906-054506_OGInsta%2B.jpg
 
Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, imeshtushwa na kasi ya kuvunjika kwa ndoa nchini chanzo kikubwa kikiwa ni kumomonyoka kwa maadili huku Mkoa wa Dar es Salaam pekee ndoa ni zaidi ya 300 zikivunjika kwa mwezi.

Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Stanslaus Nyongo, leo Jumatatu Septemba 5, 2022 baada ya kukutana na wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia na makundi Maalum.

“Tumepata hesabu (ya ndoa kuvunjika) kwa mfano Dar es Salaam pekee yake zaidi ya ndoa 300 kwa mwezi zinavunjika. Hili tunaona ni tatizo kubwa ni janga. Sisi kama kamati tunaona haja kubwa ya kuishauri Serikali kuona jinsi gani kuchukua hatua kwa ajili ya kupambana na hali hii iliyopo,”amesema.

“Hili limeshamiri sana katika jamii yetu. Na kwakweli kuna haja ya Serikali kutafuta kwa kina chanzo nini na kuona ni hatua gani za kuchukua,” amesema.
Screenshot_20220906-055426_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro linamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Siloam lililopo katika Kijiji cha Manda Chini wilayani Rombo, Amani Upendo kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wakati akimfanyia maombi.

Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Kanali Hamis Maiga amesema tukio hilo lilitokea Septemba 30, 2021 wakati binti huyo alipokwenda kwenye maombi, baada ya familia yake kuzunguka kwa muda mrefu kumtafutia tiba ya ugonjwa wa kuanguka uliokuwa ukimsumbua.

“Huyu mchungaji anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kumbaka mwanafunzi, aliyekuwa na ugonjwa wa kuanguka, baada ya familia kujaribu kumtibu hospitalini pamoja na sehemu nyingine ikashindikana.

“Hivyo wakaamua kumpeleka kwenye maombi, kwa hiyo akiwa kwenye maombi ndipo mchungaji alipofanikiwa kumbaka," amesema Kanali Maiga.
Screenshot_20220906-055514_OGInsta%2B.jpg
 
Timu ya mawakili wa aliyekuwa mgombea urais wa Kenya, Raila Ondinga wamesema wameupokea lakini hawaukubali uamuzi wa Mahakama ya Juu ya nchi hiyo iliyotupilia mbali maombi yao ya kupinga matokeo ya uchanguzi uliompa ushindi William Ruto.

Kiongozi wa jopo hilo, wakili mwandamizi James Orengo amewaambia waandishi wa habari muda mfupi baada ya uamuzi huo kuwa uamuzi wa mahakama hiyo ulikuwa wa kiitikadi zaidi kuliko kisheria.

Kwa mujibu wa sheria tunalazimika kuupokea huu uamuzi lakini nadhani ulikuwa wa kiitikadi zaidi. Tunaupokea lakini hatukubaliani nao,” amesema Orengo.
Screenshot_20220906-060315_OGInsta%2B.jpg
 
Supastaa wa Bongofleva kutoka lebo WCB, Diamond Platnumz ameibuka mshindi katika tuzo za 15, The Headies za Nigeria ambazo zimetolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu Septemba 5, 2022 Georgia nchini Marekani.

Diamond ameshinda katika kipengele cha msanii bora Afrika Mashariki baada ya kuwabwaga Harmonize, Zuchu, Meddy (Rwanda), Eddy Kenzo (Uganda) na Nikita Kering (Kenya).

Hata hivyo, Diamond ameshindwa kufua dafu kwenye kipengle cha msanii bora wa Mwaka Afrika ambacho alikuwa anawania na Black Coffee, Davido, Soolking, Aya Nakamura, Wizkid na Burna Boy ambaye ameibuka mshindi.
Screenshot_20220906-060414_OGInsta%2B.jpg
 
Rais mteule wa Kenya, William Ruto ataapishwa Jumanne Septemba 13, 2022.

Hiyo ni baada ya Mahakama ya Juu nchini Kenya kutupilia mbali maombi ya kikatiba yalifunguliwa na Raila Odinga kupinga ushindi wa Ruto.

Akitoa uamuzi huo leo Jumatatu Septemba 5, 2022, Jaji Mkuu Martha Koome amesema Raila na waleta maombi wenzake wameshindwa kuthibitisha kuwa kulikuwa na udanganyifu na uchakachuaji wakati wa mchakato wa kuelekea uchaguzi, siku na baada ya kupiga kura.
Screenshot_20220906-060504_OGInsta%2B.jpg
 
“Tuisila Kisinda ni mchezaji wetu na atacheza CAF kama tukiingia hatua za makundi kwakuwa utaratibu upo wazi, atacheza pia ligi ya ndani kwakuwa tulifuata utaratibu.”

Saad Kawemba Diemba, Mkurugenzi wa mashindano @yangasc kupitia Sports Xtra ya Clouds fm
Screenshot_20220906-060634_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom