Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Ni mwisho wa James Mbatia NCCR-Mageuzi? Hili ndilo swali wanalojiuliza wengi baada ya chama cha NCCR-Mageuzi kuitisha mkutano mkuu jijini Dodoma wiki ijayo, lengo likiwa ni kumweka kiti moto Mbatia, aliyesimamishwa Mei 21, mwaka huu.
Kwa miezi kadhaa sasa, chama hicho kimekumbwa na mgogoro uliokigawa makundi mawili, moja linaloungwa mkono na Mwenyekiti Mbatia, la pili ni lile linaloungwa mkono na Katibu Mkuu wake, Martha Chiomba.
Kundi hilo la Martha linalomhusisha pia Mwenyekiti mpya wa Baraza la Wadhamini wa NCCR-Mageuzi, Joseph Selasini ndilo linaloonekana kuwa na nguvu kubwa na baraka za Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa nchini Tanzania.
Hii inathibitishwa na ukweli kuwa kikao cha Halmashauri Kuu ya NCCR-Mageuzi cha Mei 21, mwaka huu kilichomsimamisha uongozi Mbatia na Makamu Mwenyekiti wake Tanzania Bara, Angelina Mtahiwa, kilihudhuriwa na Naibu Msajili, Sisty Nyahoza na alikitambua.
Wakati NCCR-Mageuzi upande unaoungwa mkono na ofisi ya Msajili ukiitisha mkutano mkuu utakaofanyika jijini Dodoma wiki ijayo, kumekuwa na taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa Mbatia anajiandaa kujiunga na Chadema.
Katika mitandao hiyo ya kijamii, yakiwamo makundi ya WhatsApp yenye uhusiano na Chadema, kumekuwa na wanajukwaa wanaoandika maneno kama “Karibu Chadema Mbatia”, huku wengine wakidai amekata shauri kujiunga Chadema.
Mbatia mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia hicho kinachoendelea katika mitandao ya kijamii, hakukubali wala kukataa zaidi ya kujibu kwa kifupi tu kuwa “Hilo nitalitolea ufafanuzi baadaye”.
Kwa miezi kadhaa sasa, chama hicho kimekumbwa na mgogoro uliokigawa makundi mawili, moja linaloungwa mkono na Mwenyekiti Mbatia, la pili ni lile linaloungwa mkono na Katibu Mkuu wake, Martha Chiomba.
Kundi hilo la Martha linalomhusisha pia Mwenyekiti mpya wa Baraza la Wadhamini wa NCCR-Mageuzi, Joseph Selasini ndilo linaloonekana kuwa na nguvu kubwa na baraka za Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa nchini Tanzania.
Hii inathibitishwa na ukweli kuwa kikao cha Halmashauri Kuu ya NCCR-Mageuzi cha Mei 21, mwaka huu kilichomsimamisha uongozi Mbatia na Makamu Mwenyekiti wake Tanzania Bara, Angelina Mtahiwa, kilihudhuriwa na Naibu Msajili, Sisty Nyahoza na alikitambua.
Wakati NCCR-Mageuzi upande unaoungwa mkono na ofisi ya Msajili ukiitisha mkutano mkuu utakaofanyika jijini Dodoma wiki ijayo, kumekuwa na taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa Mbatia anajiandaa kujiunga na Chadema.
Katika mitandao hiyo ya kijamii, yakiwamo makundi ya WhatsApp yenye uhusiano na Chadema, kumekuwa na wanajukwaa wanaoandika maneno kama “Karibu Chadema Mbatia”, huku wengine wakidai amekata shauri kujiunga Chadema.
Mbatia mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia hicho kinachoendelea katika mitandao ya kijamii, hakukubali wala kukataa zaidi ya kujibu kwa kifupi tu kuwa “Hilo nitalitolea ufafanuzi baadaye”.

yaani napenda kupiga simu zaidi, Mimi Rasta hizo bucha za nyama situmii
️ Antony
04– Kevin De Bruyne