DEO KANDA UPDATES
- Nyota wa Mtibwa raia wa Kongo, Deo Kanda hatimae amepata leseni ya kuanza kuitumikia Mtibwa Sugar baada ya sakata la muda mrefu dhidi ya TP Mazembe
-Baada ya Mtibwa kuinasa saini ya Kanda, waliwekewa ngumu na miamba hiyo ya Lubumbashi ambao walidai wana mkataba na Kanda huku mchezaji mwenyewe akikakana
- Mgogoro huu ulifika mpaka FIFA na sakata limechukua zaidi ya miezi mitatu mpaka kupata ufumbuzi ambapo Mazembe wameshindwa kesi kutokana na kukosa vielelezo sahihi
- Kwa maana hiyo Kanda sasa ni ruksa kucheza mechi za Mtibwa, lakini pia tayari wamemalizana na Kitayose juu ya kulipa gharama ambazo nao walitoa kipindi wanaisaka saini yake
View attachment 2258925