Makapuku Forum

Makapuku Forum

“Kufunga bao siku ya fainali ilikuwa furaha kubwa sana kwangu ila nilifurahi zaidi baada ya Cristiano Ronaldo kunipa kombe nilinyanyue mbele ya mashabiki, ilikuwa furaha zaidi kwangu” Eder Lopes, mfungaji wa bao pekee la Ureno fainali ya EURO 2016
Screenshot_20220613-044333_OGInsta%2B.jpg
 
Liverpool ipo kwenye mikono salama sana, damu changa nyingi na wana umri muda mrefu wa kucheza

Elliot - 19
Carvalho - 19
Nunez - 22
Trent - 23
Konate - 23
Diaz - 25
Jota - 25

Kwenye hiyo orodha kuna Scouser mmoja tu, kutoka academy nae ni Trent Alexander
Screenshot_20220613-044435_OGInsta%2B.jpg
 
Mtihani wa Gareth Southgate nchini Qatar ni kuipa England ubingwa wa dunia, kwenye kundi lake wapo Marekani, Wales na Iran

Sio kundi jepesi sana kwa namna timu zilivyo, kazi kubwa inapaswa kufanyika kutokana na kizazi walichonacho, sidhani kama watamuelewa endapo wakina Kane watapita tena bila kombe
Screenshot_20220613-044928_OGInsta%2B.jpg
 
“Mwanangu bado sio mchezaji bora wa kiwango cha dunia, kufikia huko anapaswa kuongeza anachofanya sasa kwa 10% zaidi ndipo afike huko kwenye kiwango cha dunia” Baba mzazi wa Heung Min Son, mshambuliaji wa Tottenham

Mzee alijibia swali la mwanae kutojumuishwa kwenye kikosi bora cha EPL
Screenshot_20220613-045022_OGInsta%2B.jpg
 
Real Madrid watamuaga rasmi Marcelo ambaye alikuwa Nahodha wao mkuu, Jumatatu, Juni 13 kwenye viunga vya soka vya Real Madrid

Baada ya hafla ya kumuaga, Marcelo atapata wasaa wa kuzungumza na Mashabiki wa klabu hiyo kubwa nchini Hispania akiwa sambamba na Rais Perez
Screenshot_20220613-045459_OGInsta%2B.jpg
 
Ukraine inasema Wanajeshi wake 10,000 wameuawa katika vita tangu ulipoanza uvamizi wa Urusi mwishoni mwa mwezi wa February.

Mshauri wa Rais, Oleksiy Arestovych ametoa maelezo katika mahojiano kwenye mitandao ya kijamii, wakati alipoulizwa jinsi makundi mengi ya Ukraine yalivyopoteza maeneo katika siku za mwanzo 100 za kivita hadi kufikia tarehe 3 Juni.

Ukraine inasema inapoteza takribani Wanajeshi 100 katika mapigano ya kila siku, huku mamia zaidi wakijeruhiwa.

Arestovych amesema kupoteza kwa Urusi kulikuwa kukubwa zaidi, Serikali ya Ukraine inasema kuwa zaidi ya Wanajeshi wake 30,000 wa Urusi waliuawa.
Screenshot_20220613-051057_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamtafuta Mtuhumiwa Zheng Lingyao (42) Raia wa China Mkazi wa Dar es salaam kwa tuhuma za kumuua Fu Nannan (26), Raia wa China, Mfanyabishara na mkazi wa Kalenga Ilala Dar es salaam.

"Tukio hilo limetokea tarehe 11/06/2022 mtaa wa Kalenga Ilala kwenye ghorofa ya tatu ya wapangaji majira ya saa tano na dakika arobaini na tano usiku ambapo Mtuhumiwa anayetafutwa alifika eneo hilo na kumjeruhi kwa risasi tumboni Nie Mnqin (32) Raia wa China na badaye alimfyatulia risasi FU, Raia wa China ambaye alipoteza maisha"

"Nie anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Taifa Muhimbili, uchunguzi wa awali wa tukio hili umebaini kuwepo kwa tatizo la kutoelewana lililotokana na masuala ya kimapenzi" Muliro Jumanne, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam
Screenshot_20220613-051210_OGInsta%2B.jpg
 
Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Kanisa Katoliki Mbeya, Mhashamu Gervas Nyaisonga, ametangaza kifo cha Padre Michael Samson wa Shirika la Wamisionari wa Afrika( White Father) aliyetoweka Juni 10 2022 katika kituo cha vijana cha Kanisa Katoliki Mbeya majira ya saa 12:00 jioni na mwili wake kupatikana June 11 majira ya saa nne asubuhi katika eneo la sabasaba karibu na mto Meta huku chanzo cha kifo chake kikiwa bado hakikajulikana.

Hata hivyo Taarifa ya Polisi bado haijatolewa kuthibitisha mazingira ya kifo hicho.
Screenshot_20220613-051341_OGInsta%2B.jpg
 
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbwelwa Kairuki amesema ameiona taarifa inayohusu Tani zaidi ya 200 za muhogo uliochakatwa Handeni kukosa soko hivyo ameahidi kuwa Wiki ijayo Ubalozi utafanya kikao na Uongozi wa Wilaya ya Handeni na wawakilishi wa Wakulima ili kutatua changamoto hiyo huku akisisitiza kwamba mahitaji ya muhogo mkavu nchini China ni makubwa sana kwa kipindi hiki.
Screenshot_20220613-051500_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri Mkuu Kivuli wa ACT WAZALENDO Doroth Semu amesema kwa mujibu wa mashuhuda kwenye eneo la Loliondo, ambako Serikali inaweka alama za mipaka kwenye eneo linalozunguka pori tengefu…. Wananchi waliojeruhiwa ni 14 miongoni mwao Wanawake 8, Vikongwe wawili na Askari mmoja kuuawa kwa mshale.

Kauli hii ya Doroth imekuja siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuthibitisha Askari Polisi mmoja kuuawawa kwa mshale huku akisema hakuna majeruhi yeyote kwenye Hospitali zote au vituo vya afya.
Screenshot_20220613-051613_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi Dodoma wanamshikilia Joachim Joseph mkazi wa Arusha kwa kusafirisha Wahamiaji 16 wasio na vibali ambao ni Raia wa Ethiopia wakitokea mkoa wa Kilimanjaro kuelekea mkoa wa Mbeya ili kuwavusha mpaka kelekea Afrika kusini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma kamishna Msaidizi wa Polisi Martin Otieno amesema Dereva huyu amekamatwa akiwa na gari aina ya Landcruser namba T 752 BVL lakini alitumia mbinu ya kufunga namba za Shirika la Umma ambazo ni SU 35970 ili asishtukiwe au kusimamishwa barabarani.
Screenshot_20220613-051927_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi Dodoma wanamshikilia Joachim Joseph mkazi wa Arusha kwa kusafirisha Wahamiaji 16 wasio na vibali ambao ni Raia wa Ethiopia wakitokea mkoa wa Kilimanjaro kuelekea mkoa wa Mbeya ili kuwavusha mpaka kelekea Afrika kusini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma kamishna Msaidizi wa Polisi Martin Otieno amesema Dereva huyu amekamatwa akiwa na gari aina ya Landcruser namba T 752 BVL lakini alitumia mbinu ya kufunga namba za Shirika la Umma ambazo ni SU 35970 ili asishtukiwe au kusimamishwa barabarani.
Screenshot_20220613-051927_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella amesema kauli ya Waziri Mkuu Bungeni kuhusu hali ilivyo Loliondo aliitoa kabla ya machafuko kutokea na sio baada kama inavyosambazwa na baadhi ya Watu.

Mongella amenukuliwa akisema “endeleeni kuwapuuza wale wote wanaopotosha kuhusu kauli ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kuhusu sakata la Loliondo, kauli yake ilitoka kabla ya tukio la machafuko kutokea"

“Vilevile nasisitiza na kuwaomba Watanzania kuendelee kuwapuuza wale wote wanaotumia kauli ya Waziri Mkuu kwa nia ovu na kwa maslahi yao binafsi” ——— amesema RC Mongella.
Screenshot_20220613-052437_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom