Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohammedi Mchengerwa Bungeni Dodoma leo amesema "Katika kipindi hiki mafanikio lukuki yamepatikana kupitia BAKITA, naweza kujinasibu kuwa matumizi ya Kiswahili yanazidi kukubalika kitaifa, kikanda na kimataifa ambapo jitihada hizo kwa kipindi cha mwaka 2021/22 zimezaa matunda kwa Kiswahili kuvishwa joho jipya kuwa lugha ya kazi katika Umoja wa Afrika"

"Kiswahili kilipitishwa kuwa Lugha ya Kazi ya Umoja wa Afrika katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika tarehe 5 - 6 Februari, 2022 Jijini Addis Ababa, Ethiopia, hatua hii ni fursa muhimu kwa Wataalamu wetu wa Tafsiri na Ukalimani nchini ambao katika muda mfupi tu tayari Watanzania 65 wamesajiliwa kupata fursa za ajira za muda na za kudumu katika Umoja wa Afrika na Kamisheni zake"

"Pia, kutokana na nafasi ya Kiswahili, kuendelea kushamiri, baadhi ya Vyuo Vikuu vya nje ya Tanzania ambavyo awali havikuwa na programu za Kiswahili vimeanza harakati za kuingiza Kiswahili katika programu zao ambapo tayari kuna makubaliano ya awali ya kushirikiana kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Ethiopia, Chuo Kikuu cha Port Harcourt (Nigeria) na Chuo Kikuu cha Joachim Chisano (Msumbiji) katika kufundisha Kiswahili"
Screenshot_20220606-145923_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo. Mchengerwa ameliomba Bunge lipitisha bajeti ya wizara hiyo kiasi cha Sh35.4 bilioni kati ya hizo Sh10 bilioni ni kwa ajili ya kukarabati viwanja saba vya michezo ili kukidhi vigezo Tanzania kuandaa mashindano ya kimataifa ikiwemo Afcon 2027. Picha na Edwin Mjwahuzi
Screenshot_20220606-150038_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge wa Viti Maalumu, Khadija Taya maarufu Keisha akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo.

Khadija amelieleza Bunge kuwa wasanii na muziki si kwamba hawapo waliokwenda shule ambapo amewataja baadhi yao wenye stashahada, shahada na shahada ya uzamili. Picha na Edwin Mjwahuzi
Screenshot_20220606-150142_OGInsta%2B.jpg
 
Ujumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) zaidi ya 1,000 wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa Kenani Kihongosi umewasili katika Hifadhi ya Ngorongoro kwa lengo la kufanya utalii wa kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo ndani Hifadhi hiyo.

Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Kenan Kihongosi ameeleza lengo la ziara hiyo ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwenye fimalu ya The Royal Tour ambayo imeonyesha vivutio mbalimbali vilivyopo ndani ya Nchi yetu.

“Vijana hawa zaidi ya 1,000 wamekodisha magari ya utalii 140 na wameamua kujigharamia kuja hapa Ngorongoro kuona vivutio tulivyonavyo ili kusaidia kutoa hamasa na chachu kwa watanzania wengine wajue kuwa Utalii unaanza na sisi wenyewe ili tuwe mabalozi wa kuhamasisha wageni wengine wa nje ya Nchi kukutembelea”

Amesema uwepo wao katika maeneo ya Wilaya za Karatu na Ngorongoro umesaidia kuongeza mzunguko kwa wajasiriamali hasa Hoteli, Magari ya utalii, biashara za vyakula kwa mama lishe hivyo kusaidia uimarishaji uchumi wa wananchi katika kusukuma agenda ya maendeleo na kuwaambia watu kuwa utalii ni fursa na utalii ni ajira. View attachment 2252262
Wataleta mmomonyoko wa udongo.
 
Mbunge wa Viti Maalumu, Khadija Taya maarufu Keisha akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo.

Khadija amelieleza Bunge kuwa wasanii na muziki si kwamba hawapo waliokwenda shule ambapo amewataja baadhi yao wenye stashahada, shahada na shahada ya uzamili. Picha na Edwin MjwahuziView attachment 2252274
Auntie si ugombee ubunge jamani, hebu acha kuota ndoto ndogo ndogo.
 
Nakuona hapa mataa mbele yangu , kitu kama piruuuu.. tisha sanaaa una issue gani huku mikocheni mala ya tatu nakuona hapa unakata kushoto.. au umehamisha ofisi

Team mbaya mbaya hivi haikufungwa ila iliyotoa draw Jioni utakuwa maeneo yako nini nije na markup pen nipige kachataa kiduchu tu pembeni ya tyre
Kwamba unaniona Mikocheni Mara ya tatu hii?Dah!!! Huyo unayemuona usinifananishe naye kabisa...

Jioni niwe wapi ndugu? Najua wewe Weekend end yako ni J3Enjoy...

Umeshafika 25?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom