Makapuku Forum

Makapuku Forum

MNOGA AWASHTUA WABONGO
.
Beki wa Portsmouth F.C, Haji Mnoga ametoa wito kwa wachezaji wenye asili ya Tanzania ambao wanacheza soka la kulipwa kwenye mataifa yaliyoendelea barani Ulaya wafanye maamuzi ya kuichezea Taifa Stars
.
“Ulikuwa uamuzi mgumu kwa sababu nilizaliwa Uingereza. Lakini, kwangu, niliona fahari zaidi kuichezea Tanzania.
.
“Inawezekana kuifanya Tanzania kuwa moja ya mataifa hatari kwenye mpira wa Afrika, Natumai kaumua kwangu kuichezea Tanzania kutaongeza msukumo kwa wachezaji wengine na kuona kuwa wanakila sababu za kuamua kulitumikia taifa lao na huo ndio uzalendo,” amesema Mnoga.
Screenshot_20220606-115211_OGInsta%2B.jpg
 
| MORLAYE SIMBA SC
.
Kama wewe ni shabiki wa Simba, basi taarifa zikufikie tu, mabosi wa klabu hiyo mezani kwao wana jina la kiungo mshambuliaji Morlaye Sylla anayekipiga kwa sasa AC Horoya ya Guinea
.
Sylla (23) aliyewahi kucheza soka la kulipwa Ureno, ni moja kati ya chaguo katika majina ya sajili zinazotua Msimbazi msimu ujao hii ni baada ya mabosi wa Simba kuridhishwa na Kiwango bora cha staa huyo anayekipiga timu ya taifa pamoja na klabu yake ya Horoya.
Screenshot_20220606-115442_OGInsta%2B.jpg
 
Arsenal yatenga Mshahara mnono kwa Jesus
.
Arsenal inataka kumpa straika wa Manchester City na Brazil Gabriel Jesus, 25, ofa ya mshahara wa Pauni 190,000 (Sh 554m) kwa wiki ili ajiunge nao katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.
.
Jesus ambaye mkataba wake na Manchester City unamalizika mwaka 2023. Msimu huu amecheza mechi 41 za michuano yote, amefunga mabao 13 na kutoa asisti 12.
.
Arsenal ndio imekuwa timu ya kwanza kuhusishwa na supastaa huyu ambaye anataka kuondoka katika kikosi hicho baada ya kuona hatakuwa na nafasi ya kucheza mbele ya Erling Haaland.
Screenshot_20220606-122650_OGInsta%2B.jpg
 
Eriksen Mbioni Kumalizana na Man United
.
Manchester United ina matumaini makubwa ya kuipata huduma ya kiungo wa Brentford na Denmark Christian Eriksen, 30, katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.
.
Mkataba wa sasa wa Eriksen unamalizika mwisho wa mwezi huu na mbali ya Man United kuna Spurs pia inaimezea mate huduma yake.
.
Man United ilifanya vibaya msimu uliopita na moja kati ya eneo ambalo walionekana kuwa na upungufu ni lile la kiungo.
Screenshot_20220606-122817_OGInsta%2B.jpg
 
SINGIDA: KUMSAJILI WAWA HAKUNA !
.
Mabosi wa Singida Big Stars (zamani DTB), wamekiri kutambua ubora wa beki wa kati wa Simba, Pascal Wawa ila wakaweza wazi kwamba hawana mpango wa kumsajili.
.
Mtendaji mkuu wa Singida Big Stars, Muhibu Kanu amefunguka kuwa: “Championship ni tofauti na Ligi Kuu Bara, hivyo umakini unahitajika sana. Tunasajili kwa kutumia ripoti ya benchi la ufundi, lakini licha ya ubora wa Pascal Wawa ila suala la kumsajili halipo akilini mwetu,”
Screenshot_20220606-122939_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kuna binadamu anaitwa Luís Filipe Hipólito Reis Pedrosa Campos ama Luis Campos napenda kumuita jina lake maarufu la The Wizard of the capital gain, huyu ndie aliepika ile Monaco dume

Yes alihakikisha Monaco inatumia pesa ndogo sana ya usajili kisha kwenda kufanya makubwa Ulaya, akahama baadae na kwenda Lille akasuka mfumo ule ule ukaipa ubingwa wa Ufaransa mbele ya PSG, Campos mtu hatari Director of football

Lakini niliwahi kumsikia kwenye interview yake moja aliwahi kusema changamoto kubwa anayopitia ni kitu kinaitwa familia ya mpira, kuna watu wapo kwenye mpira na wanaishi dunia yao kama kisiwa, hawapendi mabadiliko

Kuna watu ukigusa maslahi yao wanageuza nyeupe kuwa nyekundu, Campos aliwahi kusema ilifika muda walitamani afeli ili wazungumze namna hawawezi kutoboa kisa mfumo wake wa utawala, lakini haikuwa hivyo

Kuna muda napenda kumnukuu Fergie aliwahi kusema “One thing about football is not about football” ndio kitu kimoja kuhusu mpira huwa hakihusu mpira wenyewe

Kitu kimoja kuhusu Simba kutofanya vizuri hakihusu Simba, kitu kimoja kuhusu yote yanayotokea hivi sasa wala hayahusu mpira, niamini Mimi, ni matokeo ya kimfumo!

“One thing about football is not about football” Sir Alex Ferguson

“Kitu kimoja kuhusu mpira ni kama kisiwa kuna watu wana nchi yao na maisha yao” Luis Campos
Screenshot_20220606-123223_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge wa Makete, Festo Sanga ameitaka Serikali kuangalia uwezekano wa kuweka kima cha chini cha mshahara kwa wachezaji wa Ligi Kuu na Daraja la kwanza kwenye mpira wa miguu ili kuwaokoa na changamoto za kiuchumi.

Festo amependekeza kima cha chini cha mshara kiwe Sh1,000,000 alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Screenshot_20220606-123627_OGInsta%2B.jpg
 
Klabu ya Biashara United imemtimua kocha mkuu, Vivier Bahati baada ya kudumu kwa miezi mitano klabuni hapo.
Vivier alitambulishwa Januari 18, 2022 kuwa kocha mkuu wa wanajeshi hao wa mpakani baada ya kupewa kandarasi ya miezi sita tu.

Screenshot_20220606-131241_OGInsta%2B.jpg
 
DAVID de Gea amependekezwa kuwa nahodha mpya wa Manchester United msimu mpya utakapoanza chini ya kocha Erik ten Hag.
Kwa mujibu wa taarifa Ten Hag atawapa nafasi wachezaji kuchagua nahodha mpya baada ya kurejea Carrington mwishoni mwa mwezi huu.
Screenshot_20220606-131416_OGInsta%2B.jpg
 
Klabu ya Borrusia Dortmund inayoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani 'Bundesliga' kupitia ukurasa wake wa Twitter wamemposti beki wao, Raphael Guerreiro akiwa kwenye majukumu ya timu ya taifa Ureno na kutumia neno la Kiswahili 'Rafiki'.
Kiswahili ni lugha inayotumika zaidi barani Afrika hasa kwa nchi ya Tanzania lakini tunaona ukuaji wake duniani kila uchao.
Screenshot_20220606-131526_OGInsta%2B.jpg
 
Timu ya taifa Wales imefuzu kucheza Kombe la Dunia mwaka huu nchini Qatar baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ukraine.

Bao la kujifunga la mshambuliaji wa West Ham United, Andriy Yarmelenko limeipa tiketi Wales kushiriki fainali za kombe la dunia baada ya miaka 64.
Screenshot_20220606-131842_OGInsta%2B.jpg
 
Nahodha wa timu ya Taifa Ureno, Cristiano Ronaldo usiku wa jana alifunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Switzerland.

Ronaldo baada ya kufunga bao la pili picha zilimuonyesha mama yake akilia kwa furaha akifurahia mwanaye akifikisha mabao 117 kwenye timu ya taifa.

Screenshot_20220606-132002_OGInsta%2B.jpg
 
Tunaongoza na tunataka kuongeza zaidi idadi ya kura mbele ya mtani.

Piga kura sasa. #NguvuMoja
Screenshot_20220606-132837_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220606-132858_OGInsta%2B.jpg
 
Ujumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) zaidi ya 1,000 wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa Kenani Kihongosi umewasili katika Hifadhi ya Ngorongoro kwa lengo la kufanya utalii wa kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo ndani Hifadhi hiyo.

Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Kenan Kihongosi ameeleza lengo la ziara hiyo ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwenye fimalu ya The Royal Tour ambayo imeonyesha vivutio mbalimbali vilivyopo ndani ya Nchi yetu.

“Vijana hawa zaidi ya 1,000 wamekodisha magari ya utalii 140 na wameamua kujigharamia kuja hapa Ngorongoro kuona vivutio tulivyonavyo ili kusaidia kutoa hamasa na chachu kwa watanzania wengine wajue kuwa Utalii unaanza na sisi wenyewe ili tuwe mabalozi wa kuhamasisha wageni wengine wa nje ya Nchi kukutembelea”

Amesema uwepo wao katika maeneo ya Wilaya za Karatu na Ngorongoro umesaidia kuongeza mzunguko kwa wajasiriamali hasa Hoteli, Magari ya utalii, biashara za vyakula kwa mama lishe hivyo kusaidia uimarishaji uchumi wa wananchi katika kusukuma agenda ya maendeleo na kuwaambia watu kuwa utalii ni fursa na utalii ni ajira.
Screenshot_20220606-145608_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohammedi Mchengerwa Bungeni Dodoma leo amesema "Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Tanzania imepanga kushirikiana na Asasi ya Viacom CBS Network Africa and Peer Lead BET International katika maandalizi ya Tuzo maarufu za Muziki Barani Afrika zinazojulikana kama MTV Africa Music Awards"

"Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Asasi ya Music in Africa Conference for Collaborations, Exchange, and Showcases (ACCES) yenye Makao Makuu yake nchini Afrika Kusini inaandaa Mkutano wa Wadau wa Muziki Afrika utakaofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba, 2022"

"Majukumu mengine ni pamoja na kuratibu maandalizi ya mashindano ya urembo na Mitindo kwa Viziwi Duniani (Miss & Mr. Deaf International), kuratibu na kuandaa Tamasha la Muziki la Serengeti (Serengeti Music Festival), matamasha saba (7) ya Kitaifa na Kimataifa, kusimamia programu ya Sanaa Mtaa kwa Mtaa; kuratibu uanzishwaji wa kikundi cha Sanaa cha Taifa kwa kushirikiana na BASATA, kuratibu mashindano ya Sanaa kwa vijana kupitia UMISSETA, UMITASHUMTA, Taifa Cup Music Challenge na Vyuo mbalimbali"

"Kuratibu ushiriki wa nchi katika Tamasha la JAMAFEST na kuunda Mfumo wa kupokea taarifa kutoka BASATA, BFT na COSOTA za usajili wa Wasanii, vibali vya kuendesha shughuli za Sanaa nchini, leseni za kutumia kazi za Sanaa pamoja na makusanyo na ugawaji wa mirabaha ili kuwa na kanzidata ya kisekta"
Screenshot_20220606-145719_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom