Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mbunge wa Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo ameiomba Serikali kutazama upya sheria inayoruhusu watu kufanya shughuli zao saa 24 huku akisema sheria hizo zimepitwa na wakati hivyo zinapaswa kutazama upya.

Prof. Mkumbo ametoa ombi hilo wakati akichangia mjadala wa makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.

"Majiji yote duniani hufanya kazi saa 24, hii habari ya kwamba watu asubuhi wasifungue biashara, wasifungue baa na wasifurahi mpaka saa sita mchana ni sheria ya kizamani"

"Hii sheria inazuia furaha ya nchi, Waziri uiangalie, tuibadilishe ili watu wawe na uhuru wa kufurahi wakati wowote maadam wanazingatia sheria za nchi"
Screenshot_20220607-041952_OGInsta%2B.jpg
 
Mapato ya Stendi ya Magufuli iliyopo Mkoani Dar es salaam yameongezeka kutoka Sh. 500,000 hadi 1,195,000 kwa siku.

Ongezeko hili limetokana na agizo la Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Innocent Bashungwa alipofanya ziara yake Mei 30,2022 na kuagiza Mabasi yote kushusha na kupakia abiria katika Stendi hiyo na sio kinyume na hapo.

Agizo hilo limefanya Mabasi yanayoingia na kutoka katika stendi hiyo kuongezeka kutoka 100 hadi 265 kwa siku kitu kilichopelekea ongezeko la mapato ya Stendi hiyo.
Screenshot_20220607-042415_OGInsta%2B.jpg
 
Korea Kusini na Marekani zimefyatua mapema leo makombora manane ya kutokea ardhini kwenda angani kwenye pwani ya mashariki mwa Korea Kusini.

Hatua hiyo ni ya kujibu mfululizo wa majaribio ya makombora ya masafa mafupi yaliyofanywa na Korea Kaskazini jana Jumapili.

Shirika la habari la Korea Kusini limenukuu Jeshi la nchi hiyo likisema kuwa hatua ya leo inadhihirisha uwezo na utayari wa kufanya mashambulizi ya makombora yanayopiga maeneo yanayokusudiwa ya vyanzo vya makombora ya Korea Kaskazini.

Rais wa Korea Kusini Yoon Suk-yeol, ambaye aliingia madarakani mwezi uliopita, ameapa kuchukua msimamo mkali dhidi ya Korea Kaskazini na alikubaliana na Rais wa Marekani Joe Biden katika mkutano wa kilele mwezi Mei mjini Seoul kuimarisha mazoezi ya pamoja za kijeshi.
Screenshot_20220607-042555_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo kwa kutekeleza vema majukumu yake katika kipindi chake chote cha utumishi ndani ya Jeshi hilo.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo alipozungumza na Jenerali Mabeyo ambaye alifika Ikulu Zanzibar kumuaga Rais kufuatia kumaliza muda wa utumishi wake ndani ya Jeshi mwisho wa mwezi wa sita kwa mujibu wa sheria.

Rais Dkt. Mwinyi amemtakia kila la heri Mabeyo katika maisha yake ya kustaafu hasa ikikumbukwa amelitumikia kwa mrefu Jeshi hilo na kufanya mambo mengi yatakayoacha alama.

Kwa upande wake Jenerali Mabeyo amesema Jeshi la Ulinzi Tanzania litaendelea kumkumbuka Rais Dk. Mwinyi kwa busara na hekima zake katika kuzishughulikia changamoto mbalimbali ndani ya Jeshi hilo ambalo hatimae limepata mafanikio makubwa.
Screenshot_20220607-042709_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220607-042729_OGInsta%2B.jpg
 
Dembele Kutua Darajani
.
Chelsea ndio inaongoza kwenye harakati za kuiwania saini ya staa wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele, 25, kuelekea dirisha lijalo la majira ya kiangazi.
.
Dembele mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwisho wa mwezi huu na hadi sasa hakuna muafaka uliofikiwa kati yake na mabosi wa Barca juu ya kumuongeza mkataba mpya.
Screenshot_20220607-043158_OGInsta%2B.jpg
 
DE GEA KUMVUA UNAHODHA MAGUIRE
.
David de Gea amependekezwa kuwa nahodha mpya wa Manchester United msimu mpya utakapoanza chini ya kocha Erik ten Hag.
.
Kwa mujibu wa taarifa Ten Hag atawapa nafasi wachezaji kuchagua nahodha mpya baada ya kurejea Carrington mwishoni mwa mwezi huu.
.
Hiyo ni taarifa mbaya kwa Maguire ambaye amekuwa na wakati mgumu tangu alipovalishwa kitambaa cha unahodha huku mashabiki wa timu hiyo wakimponda kutokana na kiwango chake kibovu.
Screenshot_20220607-043306_OGInsta%2B.jpg
 
MTANZANIA ANAKIWASHA NORWAY !!
.
—8 Michezo
️—6 Mabao
—2 Assists
.
Wakati ligi za mataifa mengine Ulaya zikiwa zimemalizika huko Norway anakocheza mchezaji mwenye asili ya Tanzania Amahl Pellegrino ndio kumekucha, akiwa na FK Bodo/Glimt ametupia mabao sita na kutoa asisti mbili kwenye michezo minane.
Screenshot_20220607-043413_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom