Makapuku Forum

Makapuku Forum

Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wameridhia rasmi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kujiunga kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuifanya Jumuiya kuwa na Nchi saba.

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Uhuru Kenyatta ametangaza hilo wakati wa Mkutano wa Viongozi hao.
Screenshot_20220329-161117_Instagram.jpg
 
• China imefanikiwa kutengeneza Drone ambayo ina uwezo wa kubeba mzigo mzito wenye hadi kilo 300 ambapo katika jaribio la kwanza Drone hiyo imebeba kilograms 300 za vifaa vya kujengea na kuvipeleka mita 300 juu ambako shughuli za ujenzi wa miundombinu ya umeme zilikuwa zinafanyika. CGTNView attachment 2168323
Hii itatufaa sisi wakulima
 
Jeshi la Polisi mkoani hapa linamsaka mkazi wa Nyarugusu, Masumbuko Sumbu (16) kwa tuhuma za kuwalawiti ndugu zake watatu wenye umri wa miaka 10 na mwingine minane.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amekiri kuwa Sumbu ambaye anajihusisha na shughuli za uchimbaji madini anatuhumiwa kuwalawiti watoto hao ambao ni wajomba zake anaoishi nao nyumbani kwa babu yao Kata ya Bukoli.

Wakizungumza na Mwananchi Digital watoto hao(majina tumeyahifadhi) wamedai kuwa, binamu yao huyo amekuwa akiwaingilia kinyume na maumbile kwa muda mrefu, lakini waliogopa kusema kutokana na kuwatisha kuwa atawaua.

“Usiku ukiingia kila mtu akiwa amelala anatuamsha na kutuambia tuvue nguo kisha anashusha suruali… anatuinamisha kwa zamu akitoka kwangu anakwenda kwa mwingine hadi wote watatu anapomaliza ndio analala,“ amesema mmoja wa watoto hao.
Screenshot_20220329-162141_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi mkoani hapa linamsaka mkazi wa Nyarugusu, Masumbuko Sumbu (16) kwa tuhuma za kuwalawiti ndugu zake watatu wenye umri wa miaka 10 na mwingine minane.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amekiri kuwa Sumbu ambaye anajihusisha na shughuli za uchimbaji madini anatuhumiwa kuwalawiti watoto hao ambao ni wajomba zake anaoishi nao nyumbani kwa babu yao Kata ya Bukoli.

Wakizungumza na Mwananchi Digital watoto hao(majina tumeyahifadhi) wamedai kuwa, binamu yao huyo amekuwa akiwaingilia kinyume na maumbile kwa muda mrefu, lakini waliogopa kusema kutokana na kuwatisha kuwa atawaua.

“Usiku ukiingia kila mtu akiwa amelala anatuamsha na kutuambia tuvue nguo kisha anashusha suruali… anatuinamisha kwa zamu akitoka kwangu anakwenda kwa mwingine hadi wote watatu anapomaliza ndio analala,“ amesema mmoja wa watoto hao.
View attachment 2168329
Kristoo 😳
 
Wajumbe wa timu za kutafuta suluhu ya vita vya Ukraine na Urusi leo Jumanne Machi 29, 2022 wameanza mazungumzo katika mkutano wao ana kwa ana uliofanyika mjini Istanbul, Uturuki.

Mazungumzo hayo yamefunguliwa na Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan akitoa wito wa kuyamaliza mapigano, kati ya nchi hizo mbili yaliyodumu kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.

Watu takribani 20, 000 wamefariki huku wengine milioni 1o wakiachwa bila makazi na wengine zaidi ya milioni tatu wakiikimbia Ukraine.
Screenshot_20220329-162708_Instagram.jpg
 
Rais wa Barcelona, Joan Laporta ameweka wazi kuwa hakuna uwezekano wa Lionel Messi kurejea klabuni hapo kwakuwa hakuna mawasiliano yoyote eidha kwa Messi au wakala wake ambaye ni Baba yake mzazi

Laporta ni rafiki kipenzi wa Messi na wengi walimpa kura wakiamini kuwa angemfanya Messi asalie Camp Nou, ijapo mambo yalienda tofauti na akatimkia zake Paris
Screenshot_20220329-163401_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom