Makapuku Forum

Makapuku Forum

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango leo tarehe 29 Machi 2022 ameshiriki ufunguzi wa Jukwaa la 8 la Wakuu wa Nchi na Serikali Duniani linalofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu.

Makamu wa Rais anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika jukwaa hilo ambapo pamoja na mambo mengine lina lengo la kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kubadilishana mbinu za kuimarisha utendaji wa Serikali.

Katika Ufunguzi wa Jukwaa hilo Viongozi Wakuu wa Serikali, mashirika ya kimataifa pamoja na sekta binafsi kutoka nchi mbalimbali wamekutana na kujadili namna bora ya kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za Serikali kwa Wananchi na kutatua changamoto mbalimbali kupitia utafiti kwa kuzingatia mabadiliko yanayoendelea duniani.

Hapo kesho tarehe 30 Machi 2022 Makamu wa Rais Dkt. Mpango anatarajiwa kuzungumza katika jukwaa hilo akichangia mada ya “kwanini Afrika imekua ni muhimu sana kwa wakati huu katika uchumi wa dunia”
Screenshot_20220329-160015_Instagram.jpg
 
Mwanamke mmoja aitwae Paschalina Geay (59) mkazi wa mtaa wa Angoni "A" wilaya ya Babati mkoa wa Manyara anashikiliwa na Polisi Manyara kwa kosa la kumuua Mtoto wake wa kiume Nada Peter (6) kwa kumnyonga shingo na Kisha kumjeruhi katika paji la uso kwa kutumia kitu chenye ncha kali.

RPC Manyara, Limited Mhongole amesema tukio hilo limetokea tarehe 26/03/2022 ambapo baada ya Mtuhumiwa kutekeleza mauaji hayo alimshambulia Mtoto wake mwingine Dawii Peter (4)kwa kumpiga maeneo mbalimbali ya mwili wake na kumvunja mkono wa kulia na lengo ikiwa ni kumuua pia Mtoto huyo.

Kamanda Mhongole amesema uchunguzi wa awali umeonesha Mtuhumiwa huyo ana matatizo ya afya ya akili na hivyo upelekezi utakapokamilika atafikishwa Mahakamani.
Screenshot_20220329-160137_Instagram.jpg
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Dmytro Kuleba amewashauri Watu wote sanasana upande wa Ukraine wanaoshiriki mazungumzo ya amani na Urusi kutokula au kunywa chochote na pia waepuke kugusa nyuso zao ambapo tahadhari hii inatokana na Watu watatu akiwemo Bilionea Mrusi Roman Abramovich kupata dalili za kuwekewa sumu.

Hata hivyo Msemaji wa Serikali ya Urusi Dmitry Peskov amekanusha taarifa za Abramovich kuwekewa sumu na kusisitiza kwamba madai hayo ni sehemu ya "vita vya habari".
Screenshot_20220329-160711_Instagram.jpg
 
• China imefanikiwa kutengeneza Drone ambayo ina uwezo wa kubeba mzigo mzito wenye hadi kilo 300 ambapo katika jaribio la kwanza Drone hiyo imebeba kilograms 300 za vifaa vya kujengea na kuvipeleka mita 300 juu ambako shughuli za ujenzi wa miundombinu ya umeme zilikuwa zinafanyika. CGTN
Screenshot_20220329-160928_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom