Makapuku Forum

Makapuku Forum

“TFF ndio kama baba kwa wachezaji, hivyo wapo pamoja na mimi. FIFA pia tulipopeleka mashtaka wapo pamoja na wachezaji wote wakiangalia haki na kulinda vipaji vyao, kikubwa tusubiri kesi inatoka na majibu gani, nikishindwa sijui itakuaje lakini kama nikishinda basi kuna kiasi kikubwa cha pesa nitapata.”

- Simon Msuva.
Screenshot_20220317-153208_Instagram.jpg
 
Mmemisikia Try Again? Amesema vigogo wa timu hiyo kwa kushirikiana na benchi la Ufundi wamepanga kufanya Usajili wa Kishindo msimu ujao
Screenshot_20220317-153413_Instagram.jpg
 
The streets will never forget

Barcelona yenye nembo ya UNICEF, wakiwa hawalipwi chochote bali waliwaweka kifuani kwa ajili ya kuchangia watoto waliopo kwenye mazingira magumu duniani

Inaaminika ilikuwa moja kati ya mbinu ya jimbo la Catalunya kwenye harakati za kudai uhuru, wakiitambua Barcelona kama wawakilishi wa taifa hilo
Screenshot_20220317-154446_Instagram.jpg
 
Kwenye boti la El Cholo Diego Simeone huwa anapenda kuwa na damu kama hizi za RODRIGO DE PAUL, anapenda watu wasiowaza sana saloon wala mitandao anataka Mtu kazi
Screenshot_20220317-154628_Instagram.jpg
 
Imeandikwa na @swalehmawele

Ngoja niseme kitu kuhusu Romelu Lukaku, kwanza si mshambuliaji mbaya, nenda katazame namba zake, mfungaji bora wa muda wa Ubelgiji akiwa na magoli 67, hakuna namna yeyote unaweza kusema Lukaku ni mshambuliaji mbaya wakati namba zake ni nzuri.

Tatizo ni style of play, kinachomkuta sasa Lukaku ndani ya Chelsea kinafanana na alichokipitia ndani ya Man United, kipindi kile United ilikuwa ikicheza katika mfumo wa 4-2-3-1, timu ilitakiwa kubaki chini muda mwingi na ishambulie kwa counter attacks.

Mawinga walitakiwa kufanya mikimbio kwenye nafasi ambazo zinaachwa baada ya walinzi wa timu pinzani kutoka kwenye position yao, Lukaku alitakiwa kufanya link up play, Lukaku alifeli hapa na kuonekana mchezaji wa hovyo, akaondoka ndani ya United.

Chelsea inacheza katika system ya 3-4-2-1, wanatumia wing backs katika asilimia kubwa ya kutengeneza mashambulizi, mshambuliaji wa kati anatakiwa afanye mikimbio kwenye final zone, asisimame tu na kusubiri kuuweka mpira wavuni.

Unajua kwanini Ki Havertz anakuwa bora mbele ya Lukaku? kwa sababu Kai hasimami tu, atashuka chini na kutengeneza link up play, anavunja mstari wa ulinzi wa timu pinzani kwa kumlazimisha beki wa kati atoke kwenye eneo lake ( positional play ).

Lukaku alifanya vizuri ndani ya Inter Milan kwa sababu alikuwa bosi kwenye final zone, timu ilicheza kwa kumzunguka yeye, alisimama kwenye nafasi na kufunga, hivyo tu na hata kule Belgium anacheza hivi, tumeelewana?.
Screenshot_20220317-154745_Instagram.jpg
 
Kutoka kuwa Ballboy pale Stamford Bridge na kushuhudia tu usiku wa Ulaya akiwa pembeni ya uwanja mpaka kuvaa jezi ya Chelsea na kuipeleka robo fainali ya ligi ya mabingwa

Anaitwa Trevoh Chalobah, zao la academy ya Chelsea pale Cobham

Ndoto sio kuzikalia skani ukilia lia, ndoto ni kuamka mbio kuzikimbilia
Screenshot_20220317-154943_Instagram.jpg
 
Farhan jr

LIONEL MESSI NA ANTONELLA, MAANA NYINGINE YA MAPENZI - PART 2

Wakati wapo zao njiani na Mshikaji wake Lucas, huku wakipiga stori mbalimbali huku wakipitia EP ya Diamond ule usiku wa mbalamwezi pale Rosario, hatimae wakakaribia getini nyumbani kwa wakina Antonella

Walipokelewa na Dada zake Antonella ambao ni Carla na Paula, huko Lucas akiwachangamkia sana Binamu zake! Bila kusahau Messi alikuwa tu mkimya anaendelea kuwatazama wakiwa wanakumbatiana

Lucas kama ilivyo kwa watoto, akamsahau Mshikaji wake Messi yeye akawa busy na Binamu zake wawili, huku Messi akijiinamia kwenye kiti akisubiri zoezi la msosi, ale kisha waondoke zao

Wakati wote huo Messi akiwa mpweke, Antonella alikuwa akimtazama tu! Ikabidi atoke kwenye kiti chake na kujongea mpaka alipo Messi, kisha akamsalimia na kuketi pembeni yake, Messi alikuwa mwingi wa aibu

Lucas anasema ni kama vile Swahiba wake alitamani ardhi ipasuke aingie ndani, mdomo ulijaa mate na sauti ilikuwa haitoki kwa usahihi, wote huo ulikuwa ni uoga na aibu, kiukweli Messi alituangusha sana mwanzoni

Ndio vile Mungu hakupi vyote na akikupa kilema basi anakupa na mwendo! Ingekuwa watoto wetu wa Bongo, angechangamka kama wanajuana miaka mingi, huenda angetupia voko hapo hapo! Ila sio kwa Messi

Wakati Antonella anampigisha stori Messi, Lucas alikuwa akicheka muda wote jinsi Gwiji alivyotulia, sio yule Messi wa uwanjani akilambisha wachezaji nyasi, akikimbia kama mshale na kufunga mabao ya kideo

Lakini licha ya ugumu wote, usiku ule ndio ulikuwa mwanzo wa Messi kuzoeana na Antonella, taratibu wakaanza kupeana nafasi, kuonana na kucheza wote mitaani Rosario wakiwa na umri wa miaka tisa tu

Wakati Messi akiwa kwenye kiwango bora sana, baada ya miaka kama miwili wakati ametimiza miaka 11, alipokea taarifa mbaya sana ambayo iliwaumiza familia yake mpaka Antonella

Jioni moja wakati Messi kakutana na Antonella…..

ITAENDELEA……..
Screenshot_20220317-155211_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom