Makapuku Forum

Makapuku Forum


Linakera hili jamaa
Screenshot_20220317-183151_Instagram.jpg
 
Mnigeria ambaye alijipatia umaarufu kupitia kuishi kifahari ‘Hushpappi’ amepokea mashtaka mapya huku waendesha mashtaka wa Marekani wakiwasilisha nyaraka za mahakama zinazoonyesha jinsi alivyofanya ulaghai na kujipatia zaidi ya $400k ambayo ni zaidi ya million 900 ya kitanzania kutoka gerezani.

Hati mpya ziliwasilishwa mbele ya mahakama jijini California Marekani tarehe 16 March zinamshitaki Hushpappi kwa kufanya ulaghai na utakatishaji fedha haramu akiwa gerezani.

Nyaraka za mahakama zilisema kuwa Hushpappi akiwa gerezani alishiriki katika ununuzi na ufujaji wa kadi za benki zilizopatikana kwa njia ya ulaghai kutoka kwa data iliyoibiwa za raia na wakazi wa Marekani. Kati ya tarehe 28 Januari na 4 Machi 2022 maafisa wa usalama katika gereza hilo walibaini matumizi zaidi ya mtandao kwa Hushpappi. Wakijua kwamba alikamatwa kwa uhalifu unaohusiana na mtandao, walipata kibali cha kurekodi shughuli zake.

Mfumo maalum uliwekwa kwa ajili yake na shughuli zake zilirekodiwa kwa siku 7 na kubainika kuwa Hushpappi alikuwa akinunua kwa bidii kadi za benki za EIP kutoka soko la wahalifu wa mtandao ambapo aliporekodiwa alionekana akinunua kadi za benki 58 zenye thamani ya jumla ya $429,800 kwenye tovuti na kuziba pesa hizo.
Screenshot_20220317-201944_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) linamshikilia Allen Samuel Mhina ( 31), Mkurugenzi wa Mtandao wa kijamii wa U-turn Collection mkazi wa Temeke Mwembeyanga na wenzake 13 kwa tuhuma za kusambaza video katika mitandao ya kijamii kinyume na sheria ikimuonyesha mmoja wa wagonjwa (Polisi hawajamtaja jina) aliyekuwa amelazwa wodi ya ICU Hospitali ya Taifa ya Muhimbili suala lililoleta taharuki kwa Hospitali hiyo na Wafanyakazi wake.

Watuhumiwa hao walikutwa na vifaa mbalimbali vya kieletroniki vya kiuchunguzi ambavyo ni Kamera, Kalamu, Saa Funguo, Miwani, Kofia, Laptop, Memory Card ambavyo vyote vinachunguzwa.

"Kitendo kinachotuhumiwa kufanywa na watuhumiwa hao kililenga kudhalilisha, kutia hofu au kuleta taharuki suala ambalo linalazimisha mamkala hizi mbili za kisheria kuchunguza kwa kina suala hilo, uchunguzi ukikamilika watafikishwa kwenye vyombo vingine vya kisheria"

Itakumbukwa hivi karibuni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi alisema vyombo vya dola vinafanya uchunguzi kubaini aliyemrekodi Prof. Jay (ICU) na akaagiza Hospitali zote nchini kuweka matangazo yanayokataza kupiga picha bila kibali.
Screenshot_20220317-202118_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Jeshi la Polisi Kanda Maalum la Dar es Salaam limewakamata Matapeli sugu wa viwanja kwa tuhuma za kujipatia Tsh. Milioni 100 kwa njia ya udanganyifu wakijifanya wanamiliki na kuuza viwanja vya makazi ambavyo siyo vyao.

Tukio limetokea kati ya mwezi January na February 2022, Watuhumiwa hao 11 akiwemo Mwanamke wamekamatwa maeneo ya Goba Kinondoni baada ya kuwatapeli Ma-sister wa Kanisa Katoliki Shirika la Mabinti wa Mtakatifu Maria Kipalapala Tabora.

"Watuhumiwa hawa watafikishwa kwenye vyombo vingine vya kisheria kwa hatua zaidi"
Screenshot_20220317-202219_Instagram.jpg
 
Diana Bundala (39) maarufu Zumaridi leo March 17, 2022 akiwa na Wafuasi wake 93 wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kusomewa Maelezo ya awali ya Mashtaka matatu yanayowakabili likiwemo shitaka la kumdhuru Afisa wa Polisi pamoja na Usafirishaji wa Binadamu.
Screenshot_20220317-202347_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee

Similar Discussions

Back
Top Bottom