Ukiona kama hivi sijalala nimekesha nipo lindo
Eenh we mzee kumbe ulitabiri kabisa
Eenh we mzee kumbe ulitabiri kabisa


Farhan Jr
RALLY BWALYA UPDATES 
Kutoka kwenye vyanzo vyangu ni kuwa jana Skauti kutoka Afrika Kusini wametimiza mechi zao takribani tatu za kumtazama Kiungo Rally Bwalya wa Simba
Nyota huyo amekuwa akihitajika PSL tangu msimu uliopita, miamba mitatu ikimtazama kama Kiungo anaefaa kucheza kwenye timu zao (Ijapo jana walikuwepo wa timu moja pekee)
Msimamo wa RB tangu msimu uliopita ulikuwa ni kubaki Msimbazi, ijapo bado haifahamiki mwishoni mwa msimu huu atakuwa na msimamo gani ila bado yupo kwenye rada
Bado hakuna ofa yoyote iliyotumwa Simba wala jitihada za kuwasiliana na upande wa Bwalya, bado timu zinatathimini mwishoni mwa msimu