

Farhan Jr
Kutoka Manungu mpaka Jangwani, ameenda kutrain na Kipa wa timu ya taifa ya Mali, Djigui Diarra ambaye amecheza mpira kwenye level kubwa zaidi yake
Anaenda kupangua mashuti ya Fiston Mayele moja wapo ya Mastraika wakali kutoka Kongo, atacheza penati za Farid Mussa moja ya vipaji halisi kwenye Ligi yetu
Atapanga ukuta wa Yannick Bangala kutoka Kongo, Captain Bakari Nondo au Dickson Job! Akiwaambia wapi wakae na nini wafanye pale kwenye uwanja wa mazoezi au mechi
Atapokea maelekezo kutoka kwa Prof Nabi, atapata matibabu mazuri kutoka kwa Madaktari wakubwa na atapokea recovery session imara kutoka kwa Physios wa viwango vya juu
Guys ndio maana hata Kabwili alikuwa anaitwa timu ya taifa na Kocha Kim Poulsen, sio kwa bahati mbaya bali unatrain na nani, unacheza wapi na unaishi vipi!
Guys ndio maana hata Jasper Cillesen alikuwa namba mbili Barca ila Uholanzi alikuwa panga pangua, ndio maana Sergio Romero alikuwa namba mbili United ila Argentina ni panga pangua
Kwenye mpira wa miguu kuanza mechi ni kitu kidogo kuliko miezi 10 ambayo mnashinda wote kambini na kutrain wote

experience + exposure
Sitoshangaa Msheri akiitwa National team hivi sasa, unaweza kujiuliza kwanini hakuitwa wakati yupo Manungu! Lakini majibu yapo hapo juu tayari