Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imeomba kibali kwa Rais Samia Suluhu Hassan cha kuajiri Walimu 7,000 ili kupunguza upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari nchini.

Waziri wa TAMISEMI Innocent Bashungwa ameyasema hayo kwenye mdahalo maalum wa kujadili mafaniko katika Sekta ya elimu kwa mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan uliofanyika kwa njia ya mtandao wa Zoom.

Amesema ndani ya utawala wa Rais Samia tayari alishatoa kibali cha kuajiri Walimu 6,949 ambapo Walimu 3,000 walikuwa Walimu wa sayansi kwa Shule za Sekondari na wameshaajiriwa na wako kwenye vituo vya kazi.

Bashungwa amesema katika kuendelea kutatua tatizo la uhaba wa Walimu, tayari Ofisi hiyo imeomba kibali hicho kwa Rais ili aridhie kuajiriwa Walimu hao.
Screenshot_20220215-171635_Instagram.jpg
 
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imeomba kibali kwa Rais Samia Suluhu Hassan cha kuajiri Walimu 7,000 ili kupunguza upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari nchini.

Waziri wa TAMISEMI Innocent Bashungwa ameyasema hayo kwenye mdahalo maalum wa kujadili mafaniko katika Sekta ya elimu kwa mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan uliofanyika kwa njia ya mtandao wa Zoom.

Amesema ndani ya utawala wa Rais Samia tayari alishatoa kibali cha kuajiri Walimu 6,949 ambapo Walimu 3,000 walikuwa Walimu wa sayansi kwa Shule za Sekondari na wameshaajiriwa na wako kwenye vituo vya kazi.

Bashungwa amesema katika kuendelea kutatua tatizo la uhaba wa Walimu, tayari Ofisi hiyo imeomba kibali hicho kwa Rais ili aridhie kuajiriwa Walimu hao.
Screenshot_20220215-171635_Instagram.jpg
 
Kama unaikumbuka Filamu iliyotoka mwaka 2006 inayoitwa 'Snakes On A Plane' ambapo Samuel Jackson alicheza kama FBI basi huenda tukio hili ukalihisi ni kama movie lakini hii ni kweli.

Ndege moja ambayo ilikuwa imepaa kutoka Kuala Lumpur nchini Malaysia kwenda Tawau imelazimika kutua kwa dharura baada ya nyoka kuonekana kwenye Ndege hiyo.

Baada ya tukio hilo Kapteni alifanya maamuzi ya kutua katika Jiji la Kuching umbali wa KM 900 kutoka Tawau ambapo abiria walichukua Ndege nyingine na kuendelea na safari.
Screenshot_20220215-172226_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamshikilia Hussein Ramadhani (30), Mkazi wa Sinza baada ya kumkamata Vingunguti akiwa amevaa sare za za Jeshi la Polisi (Jungle Green) akijifanya Askari Polisi na kukamata Watu huku wakati mwingine akijihusisha na matendo ya unyang`anyi wa kutumia nguvu akiwa amevaa sare hizo.

"Upekuzi zadi ulimkuta akiwa na vifaa vingine kama Buti za Jeshi la Polisi, kadi za Benki NMB na CRDB, kadi ya Mpiga kura na kadi za NSSF zenye jina la Florence Victor Kiondo ambazo zinachunguzwa jinsi alivyozipata na kuhusishwa na tukio la kihalifu"

"Kumbukumbu zinaonesha Mtuhumiwa huyo alishawahi kufungwa kwa makosa mbalimbali na taratibu za kisheria zina fanyika ili kumfikisha tena Mahakamani, Mtuhumiwa alishawahi kufungwa jela miaka 4 kwa kosa la Kujeruhi akatumikia kifungo katika Magereza ya Mkuza Kibaha, Rwanda Mbeya na kumalizia kifungo Gereza la Kitai Mbinga Mkoani Ruvuma

"Mtuhumiwa alishawahi pia kuhukumiwa kifungo cha nje miezi 6 na Mahakama ya Mwanzo Buguruni kwa kosa la wizi, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam litaendelea kufuatilia Watu mbalimbali wanaojifanya Watumishi wa Mamoaka za Serikali na kuwabughudhi Raia wakati wao sio Mamlaka hizo husika" Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM, Muliro Jumanne
Screenshot_20220215-184134_Instagram.jpg
 
Klabu ya Yanga SC leo itacheza mechi ya Kombe la Azam Shirikisho dhidi ya Biashara United saa 1:00 usiku ikiwakosa wachezaji wake 9.

Dickson Job (adhabu)
Djuma Shaban (adhabu)
Abdallah Shaibu (majeruhi)
Salum Aboubakar (majeruhi)
Yassin Mustapha (majeruhi)
Kibwana Shomari (majeruhi)
Chrispin Ngushi (majeruhi)
Bryson Raphael (majeruhi)
Chico Ushindi (mgonjwa)
Screenshot_20220215-184401_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom