Makapuku Forum

Makapuku Forum

"Suala la Machinga si jambo jepesi hata kidogo. Hakuna mtu anayependa kuwa mmachinga bali maisha ndio yamewafikisha hapo. Hakuna anayependa kupanga vitu vyake barabarani apigwe na jua au anyeshewe na mvua au agongwe na gari.

Changamoto kubwa ni ukosefu wa ajira na Kazi ya Machinga imekuwa ni sehemu ya kupumulia.

Hili si suala la mchezo ni kuhusu maisha ya watu tena watu wanyonge kabisa. Hapa tusisukumwe na Wafanyabiasha Wakubwa wakati tunashughulikia suala la MACHINGA.

Ni jambo linalohitaji utulivu na kuangalia mustakabali wa maisha ya watu."
Screenshot_20210910-144243_Instagram.jpg
 
Club ya Simba imethibitisha taarifa za kifo cha Zacharia Hans Pope aliyekua Mjumbe ws Bodi ya Wakurugenzi wa Club hiyo.

Taarifa ya Simba imesema “Uongozi wa Klabu ya Simba umepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Zacharia HansPope ambaye amefariki dunia usiku huu” RIPHansPope
Screenshot_20210911-035311_Instagram.jpg
 
Mahakama Kuu kanda ya Arusha masjala ndogo ya kazi imemuamuru Dalali wa Mahakama aliyepangwa kuhakikisha ifikapo October 15 mwaka huu awe ameuza mali za Mdaiwa ambaye ni hoteli ya Impala na Naura Springs ili kufidia deni la shilingi Bilioni 1.3 linalotokana na malimbikizo ya mishahara ya Wafanyakazi.

Akitoa Amri hiyo Naibu msajili wa mahakama hiyo Ruth Masama alidai kwamba makubaliano yaliyofikiwa na upande wa Mdai na Mdaiwa juu ya uuzwaji wa mali hizo ambazo ni kiwanja cha kitalu namba 16,17,18,19,20,21,22, na 23 vilivyopo eneo la Uzunguni Arusha na kwamba October 15 itapata taarifa ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Afisa kazi Mfawidhi mkoa wa Arusha Emmanuel Mweta ameieleza Mahakama hiyo wamefika Mahakamani hapo kwa ajili ya kusajili mkataba wa maridhiano kwa ajili ya kuuza mali za Mwajiri ili kufidia madai ya Wafanyakazi yanatotokana na malimbikizo ya Mishahara.

Amesema viwanja hivyo vikiuzwa thamani yake inaweza kufikia zaidi ya Billion 2.
Screenshot_20210911-035528_Instagram.jpg
 
Club ya Simba SC. imemtangaza Kocha Thierry Hitimana (42) Raia wa Rwanda kuwa Kocha wao msaidizi kwa lengo la kuimarisha kikosi chao.

Taarifa hizo zinakuja muda mfupi baada ya kuripotiwa kuwa Kocha wao Mkuu Raia wa Ufaransa Didier Gomes hatoruhusiwa kukaa katika benchi katika michuano ya kimataifa kama hatokuwa na CAF License A au UEFA Pro License ambayo hana.

Inaonekana Hitimana ambaye ana CAF License A ndio atashika mikoba wakati huu unaodaiwa kuwa Gomes atakuwa anapambana na kozi.
Screenshot_20210911-035710_Instagram.jpg
 
Safari za ndege za kimataifa zimeanza tena nchini Afghanistan ikiwa hatua muhimu kwenye juhudi za Serikali mpya ya Taliban kurejesha hali ya kawaida baada ya kuchukua madaraka mwezi uliopita.

Ndege ya Shirika la Qatar iliondoka jana kuelekea Doha ikiwa na abiria 113 wakiwemo Raia wa Ujerumani, Marekani, Canada na Uingereza na nyingine ya pili imetua Kabul leo.

Msemaji wa Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani Ned Price amethibitisha kuwa Raia 10 na Wakaazi 11 wa kudumu wa Nchi hiyo walikuwemo kwenye ndege hiyo, Mjumbe maalum wa Qatar nchini Afghanistan, Mutlaq bin Majed al-Qahtani, amesema safari hii ni ya kawaida na si sehemu ya kampeni ya kuwahamisha watu wanaotaka kuikimbia Afghanistan.

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Qatar, Sheikh Mohammed bin Abdulrahman Al-Thani amewashukuru Viongozi wa Taliban kwa kusaidia kwenye kuufungua tena uwanja mkubwa wa ndege wa Kabul.
Screenshot_20210911-035859_Instagram.jpg
 
“Nitumie nafasi hii pia kukipongeza kituo cha matangazo cha Azam (Azam Media) hususan upande wa matangazo ya runinga kwa kuibua na kuutangaza vyema mchezo wa masumbwi nchini, juhudi hizo za Azam Media wakishirikiana na wadau wengine zimewezesha wanamasumbwi wetu kutumia vizuri fursa hiyo kukuza vipaji vyao”

“Nimpongeze Twaha Kiduku kwa kumtwanga Dulla Mbabe katika pambano lililovuta hisia za Watanzania wengi, vilevile nimpongeze Bondia Hassan Mwakinyo kwa kumdunda mpinzani wake Mnamibia Julius Indongo kwa TKO na kutetea mkanda wake wa Chama cha Ngumi Afrika (ABU)”

“Wanamasumbwi wetu wameendelea kuifanya Tanzania itambulike zaidi ulimwenguni sasa tunasubiri pambano la watani Mwakinyo dhidi ya Kiduku” ——— Waziri Mkuu Majaliwa akiahirisha Mkutano wa nne wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Screenshot_20210911-040320_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Kuna taarifa kutoka Shirikisho la soka barani Afrika kuhusiana na Makocha ambao hawapaswi kukaa kwenye mabenchi ya michuano ya Afrika

Kwenye hayo majina kuna jina la Kocha wa Simba, DIDIER GOMES DA ROSA ikanilazimu kwanza niwasiliane na wajuzi wa mambo kutoka CAF na ndani ya nchi

Nikaenda kwanza kwenye page ya CAF kujiridhisha kama taarifa ni sahihi? YES ni kweli ipo pale na ni sahihi kabisa bila shaka

Nikamcheck Mtu wa karibu na Klabu ya Simba kutaka kujua kama taarifa hiyo wameipokea! Akanijibu YES taarifa hiyo ipo, ni sahihi

Kwakuwa FARHAN wa Morogoro sio mbobezi sana wa masuala haya ya Ukufunzi nikalazimika kumtafuta Mwandishi nguli barani Afrika anipe uzoefu wake

Swali langu la kwanza kwake! Kocha GOMES ANA UEFA A! Kwanini CAF hawaitambui na wanataka CAF A? Utofauti ni upi?

Akaniambia Mdogo wangu UEFA A zamani ilikuwa kubwa ila baada ya ujio wa UEFA PRO LICENCE, hii UEFA A kwa Afrika ni sawa na CAF B! Ambayo ilitolewa Morogoro miezi kadhaa nyuma, Matola akiwemo (CAF B) kumaanisha kwamba hakuna Kocha wao mwenye vigezo kwasasa

Nikamuuliza Simba wanapaswa kufanya nini? Akanijibu kuwa cha kwanza wanaweza kumleta Kocha mwenye CAF A kama Thierry Hitimana ambae wanafahamiana vyema, anaweza kupewa mikoba kisha yeye akawa kivuli (Assistant Coach)

Ama plan B ni kuwa Gomes anapaswa kuondoka kwakuwa CAF walishatoa taarifa hii mwaka mzima sasa! Na Makocha wengi walienda kusoma wakiwemo wakina Gavin Hunt wa Afrika Kusini, uwezekano ni mdogo wa CAF kulegeza

Akanambia Makocha wengi Vijana ndio wana CAF A na UEFA PRO LICENCE kama Sundey Oliseh, Benny McCarthy, Sven Van Der Broek! Ila wengi wazee na ambao wapo Afrika kwa muda mrefu hawana

Nikamuuliza kuna shida yoyote kati ya UEFA na CAF? Akanijibu YES! Maana UEFA hawatambui CAF A kama Kocha anaweza kufundisha, hivyo na CAF hawatambui UEFA A kama unaweza kufundisha

Mwisho nikamuuliza unaona Kocha gani anafaa? Kiutani tu akanambia yule Sven wenu ana UEFA PRO LICENCE, mrudisheni bwana Basi tukamalizana hivyo
Screenshot_20210911-042359_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Wakati nimepost andiko langu kuhusu Kocha Didier Gomes wengi wakaniuliza maswali mengi, nami nitajibu baadhi ifuatavyo

Iliwezekana vipi Kocha huyo kuingoza timu msimu uliopita kwenye CAF? Well Kocha alikuja katikati mwa msimu na tangazo la CAF lina mwaka sasa!

Kwenye msimu ule ule Gor Mahia na Platinumz zilipigwa pin kisa Makocha wao hawana vigezo, wakaajiri Deiwaka kuwaongozea timu zao kwenye CAF

Simba ilipata exemption na baadhi kutokana na mahusiano yao! Kwanza SIMBA na CAF, lakini pia TFF na CAF hii wakati mwingine inasaidia sana baadhi ya mambo!

Gor Mahia ya Kenya ilipata wakati mgumu kutokana na mahusiano yao na Shirikisho la soka Afrika, ni hapo Kenya ambapo mpaka marefa wa CAF huwa wanapigwa, hivyo walionja joto la iwe tangu msimu uliopita

Mnakumbuka vyema niliwahi kusema kitu kuhusu NETWORK! NIlisema kuhusu CLUB VS FEDERATIONS! hii ndio leo mnaona namna gani imetumika hapo kwa msimu uliopita

Tumesikia kuwa Kocha anasoma PRO LICENCE ONLINE? Kiukweli hiyo taarifa sina, iwe anasoma au hasomi lakini vigezo ni kuwa kocha awe na LESENI sio Continous au Mwanafunzi bali leseni! As for now hana vigezo

Kuna namna Simba wanaweza kubaki na DIDIER GOMES? YES wanaweza kubaki nae, ila kwa option kuwa waajiri Kocha mwenye vigezo awe CAF A au Pro Licence, huku yeye akiandikishwa kama Msaidizi

Unahisi nani atapewa mikoba ya Simba? Well mimi nampenda THIERRY HITIMANA! wamefanya wote kazi Rwanda, wanafahamiana vyema na ana CAF A hivyo wanaweza kuunda bench la HITIMANA na Wasaidizi wawili, GOMES na MATOLA
Screenshot_20210911-042701_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Posts zangu mbili za mwisho kuhusu Simba nimemtaja sana THIERRY HITIMANA, kwa namna fulani niligusia kuwa huenda akaenda kuwa Kocha wa Simba

Okay! Iko hivi Didier Gomes wakati anakuja Simba aliwaambia anamuhitaji Thierry Hitimana aje nae kama Msaidizi wake, Kwakuwa waliwahi kufanya wote kazi Rwanda

Bahati mbaya kwa namna moja ama nyingine klabu haikuweza kumkamilishia hilo kutokana na hesabu walizopiga wakati huo, hivyo Thierry hakwenda Simba

Sasa wakati msimu huu unaelekea kuanza, Simba walikitazama kikosi chao kina jumla ya wachezaji 31 ambapo Makocha wawili pekee hawawezi kukimudu

Thierry ilikuwa atue nyumbani kwetu huko Morogoro asaini na Mtibwa ila nilipoanza kupata tetesi kutoka nyumbani ni kuwa Thierry haonekani huko Estate, sio Ifakara, Mahenge wala Morogoro Mjini ila yupo Dar

Ni hivi Simba waliwasiliana na Thierry Hitimana na amesaini na Simba tangu siku ya Jumapili ya tarehe 4, Septemba huku wakiwa bado wanafikiria majukumu yake awe Mkurugenzi wa Ufundi au aongeze nguvu kwenye bench

Mwisho ikaamuliwa kuwa Thierry aende kwenye bench la Ufundi, sehemu ambayo kuna Gomes mwenye UEFA A, Thierry mwenye CAF A, Rivelinho (Kocha wa Makipa) ana A ya CONMEBOL, huku Matola akimaliza CAF B

Simba wameipenda hii format kutoka kwa Mamelodi Sundowns kwa Afrika wana Makocha watatu! Wana Manqoba Mngqithi, Steve Komphela na Rhulani Mokwena, wote hao wapo benchini, ni bench haswa!

Ujio wa Thierry sasa utaenda kuwafanyia Simba wepesi kwenye CAF CHAMPIONS LEAGUE, Kwakuwa ana CAF A THIERRY HITIMANA!

Hivi ndivyo ilivyokuwa, walinitonya mapema sana Ndugu zangu wa huko Mvomero ndio maana nikawa naandika kwa kujiamini
Screenshot_20210911-042957_Instagram.jpg
 
Ujenzi wa daraja jipya la Wami umefikia asilimia 57.5 amesema Meneja wa TANROADS Mkoa wa Pwani Eng. Andrea Kasamwa wakati akiielezea kamati ya siasa CCM Pwani iliyoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Ramadhani Maneno pamoja na Mkuu wa Mkoa huo Aboubakar Kunenge waliotembelea eneo la tukio.

Ujenzi wa daraja hili unatumia takribani BILIONI 67.8 ambapo kukamilika kwake kutarahisisha magari yanayoelekea mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha kupita kwa urahisi na usalama kuliko daraja lililopo sasa.

Mkuu wa mkoa Aboubakar Kunenge amewahakikishia Wakandarasi wa ujenzi kwamba pesa za mradi huo zipo na kumshukuru Rais wa Samia kwa kuipatia pesa miradi mikubwa ya kimkakati katika mkoa wake ikiwemo daraja hilo lililopo Halmashauri ya Chalinze, Bandari kavu iliyopo Kwala pamoja na Bwawa la Mwalimu Nyerere.
Screenshot_20210911-130105_Instagram.jpg
Screenshot_20210911-130126_Instagram.jpg
 
Shirikisho la soka Afrika (CAF) kupitia TFF limetangaza kuwa mchezo wa Yanga vs River United ya Nigeria wa round ya awali ya club Bingwa Afrika kesho utachezwa bila mashabiki katika uwanja wa Benjamin Mkapa kutokana na tahadhari ya corona.
Screenshot_20210911-130307_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom