Matajiri wawapa mzuka mastaa Yanga, kuvuna milioni 500
.
Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Bara, Yanga, kesho jioni wanashuka uwanjani ili kuwakabili Rivers United ya Nigeria, huku mastaa wa Jangwani wakiwa wamejazwa upepo baada ya bilionea wa klabu hiyo kuwawekea mzigo wa maana mezani ili kuhakikisha wanalikamilisha jambo lao la kufika hatua ya makundi.
.
Ipo hivi. Jana jioni mabosi wa Yanga walikutana na mastaa wa timu hiyo kwenye kambi yao ya Avic, Kigamboni jijini Dar es Salaam na matajiri hao wakatoa tamko zito la kufika makundi msimu huu, kwa kuwahakikishia kuwa kwamba wamedhamilia kufanya kweli, basi watachukua si chini ya Sh milioni 500 wakiwatoa Rivers United.
.
Fedha hizo ni kama bonasi tu ambapo Yanga wanataka kuhakikisha wachezaji wao wanahamasika na kushinda.
View attachment 1933355