

Farhan Jr
Kupitia mitandao yake ya Kijamii, Bernard Morrison wa Simba amepost kuwa atatumia jina la Mama yake kwenye jezi yake, EFUA MORRIS kwa heshma yake
Kuweka majina kwenye jezi mfano kwa England walianza rasmi 1993 huku wakianza kwa sheria ngumu ikiwa ni lazima jina la ukoo (surname litumike)
Hii iliwapa tabu mtu kama Jordi Cruyff mtoto wa Johann Cruyff alietaka kucheza nje ya kivuli cha Babake pale Manchester United, akihitaji jezi yake iandikwe tu JORDI, ijapo baadae sheria zikalegezwa
Kwenye mabadiliko ya sheria duniani kuhusu majina kwenye jezi yakaleta matumizi ya Majina ya utani (nicknames) na mengineyo (other names)
Sasa nini vigezo vya majina kwenye jezi kwa wachezaji?
Mosi! Jezi ya Mchezaji inapaswa kuwa na majina yake eidha lake au mzazi, ukoo! Ama jina lolote lile, ambayo yameidhinishwa na bodi ya Ligi, kwa hapa kwetu ni TPLB
Ikumbukwe Klabu yake itajaza fomu maalum yenye majina ya wachezaji, namba zao za jezi na majina mengine, ambayo mchezaji ataandika, iwapo TPLB wataridhia kuwa halina shida kimaadili basi linapita, haswa matusi
Na hapo kwenye majina mengineyo yanaweza hata kuwa ya utani kama vile GAUCHO, NADO, BABI, MACHEJO au SURE BOY kwa kadri Mchezaji anavyojisikia yeye, mfano hayo yamewahi kutumika nchini
Pia katika kupitisha hayo majina mpaka kigezo cha mahusiano ya kifamilia haswa wazazi yanaweza kuchagiza mabadiliko mfano Ravel Morrison kama mnamkumbuka au Nuno Gomez wa Ureno, ama Dele Alli
Hivyo Morrison anaweza kutumia jina la Mama yake bila tatizo lolote, baada ya Bodi ya Ligi (TPLB) kuridhia kuwa hakuna shida kabisa, hiyo ipo duniani kote kama ilivyo kwa CHICHARITO au KUN AGUERO
EFUA MORRIS

! Ready for PREMIER LEAGUE