Aliyekuwa Afisa Habari wa Simbasc Tanzania, Haji Manara leo kwenye mkutano wake na Waandishi wa habari.
"Sijawahi kugombana na mwandishi yeyote kwa sababu ya masuala yangu binafsi, yote hii ilikuwa ni kwasababu ya Simba Sc, ni katika kutetea kiongozi au mchezaji pamoja na brand ya Simba, mimi sio mkamilifu katika kufanya kazi lazima kuna kukosea"
"Nawashukuru sana Yanga Sc wenyewe wanajiita Dar Es Salaam Young Africans hasa katika kipindi hiki cha usajili, yawezekana utani ulizidi ila lengo langu lilikuwa ni kudumisha utani wa jadi, pale nilipokosea wanisamehe na najua niliwakosea"
"Wanasema hakuna mtu mkubwa kuliko Simba Sc, hapana hiyo ni haramu, kwani kuna mahali niliwahi kusema Haji ni Mkubwa? nimefanya makubwa sana katika kuhamasisha timu, mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni"
"Mkiniona mikoani mjue najitegemea, Msemaji anayepiga promo kubwa na anaisemea timu, nauli anajitegemea, kula anajitegemea, hoteli anajitegemea hadi safari za nje anajitegemea, kila wakisafiri naambiwa jina lako halipo" ameeleza Haji Manara