Makapuku Forum

“Tumerudi tena na Operesheni kubwa Kibiti, tuna Askari wa kutosha wapo kule wanafanya operesheni, tunaomba Ndugu zetu kule Kibiti, Mtwara, Lindi Wananchi watupe taarifa kama kuna mambo hayako sawa, kuna operesheni kule Msumbiji tunaamini kuna baadhi ya Watu watarudi hao wanaorudi lazima wapate moto kwa mujibu wa Sheria”

“Tutahakikisha maeneo yanakuwa shwari, kuna wale wa Msumbiji kule tunadhibiti kuhakikisha wasije kuja huku na kama watakuja wabadlike na wasipobadilika moto ni uleule uliowafanya wakimbie kule” ——— Asema Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro leo Dar es salaam.
Screenshot_20210802-195749_GBInsta.jpg
 
SkySports wameripoti kuwa staa wa England Harry Kane hajarejea katika mazoezi ya timu yake ya Tottenham Hotspurs leo kama alivyotakiwa baada ya likizo yake fupi kumalizika, inadaiwa Kane anashinikiza ili Spurs imuuze, baadhi ya vyombo vya habari England vinamuhusisha na Man City
Screenshot_20210802-195939_GBInsta.jpg
 
Ni Mshangao na maajabu ya aina yake yaliyoambatana na simanzi na vilio pale wanandoa wawili waliozaliwa siku moja, mwaka mmoja na kufariki siku moja ambao wamezikwa leo kwa pamoja katika kata ya Rau, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wanandoa hao ambao ni Kundaeli na Monyiaichi Kimaro walizaliwa mwaka 1946.
Screenshot_20210802-200112_GBInsta.jpg
 
Pengine hii ni taarifa isiyopendeza kwa baadhi ya wanaume wenye tabia ya kunyonya maziwa ya wake zao wanaonyonyeshwa katika Mkoa wa Iringa imeelezwa kuwa kitendo hicho ni mojawapo ya sababu zinazochangia tatizo la udumavu kwa watoto mkoani hapo.

wanaume wataelewa sasa
Screenshot_20210802-200348_GBInsta.jpg
 
Polisi Mkoa wa Rukwa inamshikilia kijana mmoja (35) mkazi wa Kata ya Chanji kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi, Thomas Mremi (85) na kumzika kimyakimya nyumbani kwao.

Mremi, aliyekuwa ofisa mstaafu Mwandamizi wa Jeshi la Magereza aliyestaafu utumishi wa umma akiwa na cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Magereza (ASP), aliuawa usiku pasipo watu kufahamu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, William Mwampaghale alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo juzi, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa.

Alisema mtuhumiwa, ambaye hakumtaja jina kwa kuwa uchunguzi unaendelea, anadaiwa kumuua baba yake huyo kwa kumpiga kichwani na kitu kizito katokana na kuwepo kwa mzozo wa muda mrefu kati yao, ambapo mtoto huyo alitakiwa kuondoka nyumbani na baba yake kwa sababu amefikia umri wa kujitegemea.
Screenshot_20210802-200655_GBInsta.jpg
 
Matarajio ya Wakenya wengi yameangulia patupu baada ya mwanariadha wa Morocco Soufiane El Bakkali kushinda mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji mjini Tokyo, Japan.


Mwanariadha wa Kenya Benjamin Kigen alifanikiwa kupata nishani ya shaba.

-
Kigen alijikakamua na kuibuka wa tatu katika muda wa 8:11.45 baada ya kumshinda Getnet Wale katika kihunzi cha mwisho.
Soufiane El Bakkali ni Mmorocco wa kwanza kushinda mbio hizo.

Mwanariadha wa Ethiopia Lamecha Girma aliishindia nchi yake nishani ya fedha baada kuchukua nafasi ya pili kwa kumaliza katika muda wa 8.10.38.

-
Kenya imeshindwa katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1984 katika michezo ya Olimpiki.
Screenshot_20210802-201539_GBInsta.jpg
Screenshot_20210802-201555_GBInsta.jpg
 
Mfahamu nyota wa soka Cristiano Ronaldo uwanjani yumo, na kwa wanawake yumo.

Ukitaja wanasoka mahiri wawili wa kizazi cha sasa duniani, jina la Cristiano Ronaldo lazima liwepo kwenye orodha hiyo, ama litakuwa la kwanza ama la pili, inategemea na tafsiri ya anayeweka orodha hiyo kati yake na Lionel Messi.

Cristiano Ronaldo Dos Santos Aveiro alizaliwa mwaka Februari 5, mwaka 1985 huko Funchal katika visiwa vya Madeira, kwa mama Maria Doroles Dos Santos Aveiro na marehemu baba yake Jose Dinis Aveiro.

Alipozaliwa tu baba yake akampatia jina la Ronaldo akimuona kama Ronald Reagan (Rais wa Marekani) ajae.

Wakati huo baba yake hakuwa na wazo kabisa kuhusu mwanae kuwa mwanasoka, alimpenda sana Rais Reagan, ambaye wakati Ronaldo anazaliwa ndio alikuwa ametoka kuapishwa kuwa rais katika awamu yake ya pili ya uongozi.

Kama si daktari almanusura mama yake aitoe mimba yake leo soka lisingekuwa na Ronaldo na lisingekuwa na mfungaji mahiri wa aina yake.

Tafiti zinaonyesha nyota huyo wa kiataifa wa Ureno ana asili ya Afrika Magharibi
Screenshot_20210802-201959_Instagram%20Lite.jpg
 
Mfahamu Lionel Messi mwanasoka ambaye rekodi yake inasoma kama nyota isiyopungua mwanga.

Ni mchezaji mpole na makali yake yamefahamika na kudhihirika pindi anapojitosa uwanjani.

Ni miongoni mwa wachezaji wanaotambulika sana kote dunia na isitoshe amesalia katika klabu moja tangu alipoanza kucheza-Barcelona .

Jina lake ni Lionel Andrés Messi au Leo Messi, na alizalia Juni tarehe 24 mwaka wa 1987.

Ni Nahodha wa timu ya taifa ya Argentina na anazingatiwa kuwa mojawapo ya wachezaji bora wa nyakati zote .

Messi ameshinda tuzo za Ballon d'Or mara sita.

Tangu 2008, Messi amekuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Antonela Roccuzzo, Anamfahamu mpenzi wake huyo tangu akiwa na umri wa miaka mitano, kwani Roccuzo ni binamu wa rafiki yake wa karibu tangu utotoni, Lucas Scaglia, ambaye pia ni mchezaji wa soka.

Messi na Roccuzzo wana watoto watatu: Thiago (aliyezaliwa 2012), Mateo (aliyezaliwa 2015) na Ciro (aliyezaliwa 2018).
Screenshot_20210802-202305_Instagram%20Lite.jpg
 
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limeingia mkataba wa miaka 10 na TFF wa kutangaza Ligi Kuu Tanzania Bara wenye thamani ya Tsh. bilioni 3.54, mkataba huo unaipa TBC pekee haki ya kurusha matangazo kwa njia ya sauti hivyo chombo chochote kingine cha habari kikitaka kurusha matangazo kwa sauti lazima kiwe na makubaliano na TBC.
Screenshot_20210803-174059_GBInsta.jpg
 
Mshambuliaji wa kimataifa wa Congo DR Heritier Makambo amerejea Yanga SC baada ya kumalizana na club ya Horoya ya Guinea.

Makambo alijiunga na Horoya 2019 na kusaini mkataba wa miaka mitatu akitokea Yanga SC lakini alidumu Horoya kwa miaka miwili na mkataba wake kuvunjwa kwa makubaliano ya pande zote mbili na sasa amerejea Jangwani ambapo alikuwa na msimu mzuri.
Screenshot_20210803-181721_GBInsta.jpg
Screenshot_20210803-181739_GBInsta.jpg
 
Kwa mara ya kwanza tangu aliyekua Rais wa Haiti Jovenel Moïse kuuwawa nyumbani kwake mbele ya Mke wake July 7, Mke wake huyo aitwae Martine Moise ambaye alisafirishwa kwenda Marekani kwa ajili ya matibabu baada ya kujeruhiwa kwenye shambulio hilo, amezungumza kwa mara ya kwanza.

First Lady huyu amesema kuwa mashambulizi siku hiyo yalianza usiku wa saa saba ndipo walianza sikia risasi zinapigwa kwenye chumba chao na wakaamua kujificha lakini Watu hao hawakuishia hapo kwani waliingia mpaka ndani ya nyumba na kuvunja mlango na kuingia mpaka chumbani kwao.

Anasema wale Wauaji walikuwa wametumwa kwani walivyovunja chumba chao walikuwa na kazi moja tu ya kutafuta nyaraka na walipozipata wakapiga simu na kuwaambia waliowatuma kuwa wameshazipata na kisha kumsogelea Rais na kupokea maelekezo ambayo yaliashiria kuwa ndie Mtu sahihi anaetakiwa kuuwawa.

Mpaka wakati huo tayari Rais na Mke wake walikua wameshajeruhiwa kwa risasi nyingi na Wauaji hao wakapewa agizo kuwa wamalizie kumuua Rais Jovenel Moise “hatukujua kama wangefanikiwa kufika kwenye chumba tulikojificha maana nje tulikua na Walinzi 30 au 50”.
Screenshot_20210803-181947_GBInsta.jpg
Screenshot_20210803-182008_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom