Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,008
- 453,986
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza masharti mapya ya kupambana na Corona ambapo amesema ni marufuku kwa Watu kutembea usiku kuanzia saa moja usiku hadi 11:30 alfajiri.
“Watu wote wanapaswa kubaki Majumbani, wanaoruhusiwa kutembea usiku ni Watu wa Ulinzi na Usalama na makundi mengine yaliyopewa ruhusa”
“Baa zitaendelea kufungwa na Askari wanapaswa kuwakamata na kuwatoza faini Wamiliki wa Baa wanaokiuka agizo” ———Museveni.
“Bodaboda wanaruhusiwa kufanya kazi ila mwisho ni saa 12 Jioni na wanapaswa kubeba abiria mmoja (sio mshikaki) au mizigo” ———Museveni.
“Watu wote wanapaswa kubaki Majumbani, wanaoruhusiwa kutembea usiku ni Watu wa Ulinzi na Usalama na makundi mengine yaliyopewa ruhusa”
“Baa zitaendelea kufungwa na Askari wanapaswa kuwakamata na kuwatoza faini Wamiliki wa Baa wanaokiuka agizo” ———Museveni.
“Bodaboda wanaruhusiwa kufanya kazi ila mwisho ni saa 12 Jioni na wanapaswa kubeba abiria mmoja (sio mshikaki) au mizigo” ———Museveni.