Makapuku Forum

Baada ya kuzuka kwa moto katika jengo la kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Msamvu mapema leo asubuhi na kusababisha kukatika kwa umeme Morogoro, Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Morogoro limeomba radhi wateja wake na kusema Wataalamu wapo eneo la tukio kuhakikisha huduma inarejea kama kawaida

“Maeneo yanayoathirika kwa katizo la umeme ni Manisipaa ya Morogoro, Wilaya ya Mvumero, Kilosa, Mvuha pamoja na maeneo yanayotumia laini inayotoka Msamvu kituo cha kupoozea umeme”———TANESCO Morogoro
Screenshot_20210802-132217_GBInsta.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan akiagana na Viongozi mbalimbali wa Serikali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam leo August 02, 2021 akielekea Kigali Nchini Rwanda kwa ziara ya Kiserikali ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Paul Kagame.
Screenshot_20210802-132413_GBInsta.jpg
 
Baada ya kuzuka kwa moto katika jengo la kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Msamvu mapema leo asubuhi na kusababisha kukatika kwa umeme Morogoro, Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Morogoro limeomba radhi wateja wake na kusema Wataalamu wapo eneo la tukio kuhakikisha huduma inarejea kama kawaida

“Maeneo yanayoathirika kwa katizo la umeme ni Manisipaa ya Morogoro, Wilaya ya Mvumero, Kilosa, Mvuha pamoja na maeneo yanayotumia laini inayotoka Msamvu kituo cha kupoozea umeme”———TANESCO MorogoroView attachment 1877257
Naona na huku Arusha nako tumekatiwa
 
Jeshi la Polisi Nigeria limemsimamisha kazi mmoja wa Polisi wake maarufu na wanaoheshimika baada ya jina lake kujumuishwa kwenye Wanigeria wanaotuhumiwa kushirikiana na Mnigeria Ramon Abbas maarufu kama Hushpuppi ambae anakabiliwa na makosa ya utakatishaji alizokua akiiba kupitia mtandao.

Wanigeria mbalimbali walishtuka na taarifa za Polisi huyu Abba Kyari kuhusishwa na Hushpuppi kwani siku zote ameonekana ni Askari mwenye sifa nzuri na amekua akifanikisha mapambano mengi dhidi ya uhalifu.

Hadi sasa nyaraka za Mahakama Marekani zimeonesha kwamba Hushpuppi (37) ambae alikamatiwa Dubai, alisabishia Watu mbalimbali hasara ya USD milioni 24 (zaidi ya Tsh. Bilioni hamsini na tano).

Hata hivyo Kyari amesema hausiki na chochote kwenye madai hayo na kwamba mikono yake ni misafi, Ripoti zinasema kuwa kutokana na mashtaka dhidi yake… Hushpuppi anaweza kufungwa mpaka miaka 20 jela Nchini Marekani.

Hushpuppi aliekua akiishi Dubai na kutumia ukurasa wake wa Instagram wenye followers milioni 2.5 kuonesha maisha ya kifahari na magari ya bei mbaya, anatajwa na FBI kuwa ni mmoja wa watakatishaji fedha wakubwa wa dunia.
Screenshot_20210802-132518_GBInsta.jpg
 
Watu kadhaa wamehamishwa katika maeneo ya Utalii kusini mwa Uturuki leo Jumapili wakati moto wa msituni unaondelea kuwaka kwa siku ya 5 mfululizo ukisababisha vifo vya Watu 8, Waziri wa Afya Fahrettin Koca kupitia mtandao wa twitter amesema Watu saba wamefariki katika eneo la Antalya na mwingine mmoja amefariki katika eneo la Marmaris huku mamia wakijeruhiwa.

Moto wa porini ulianza katika mikoa mbalimbali nchini Uturuki na vikosi vya dharura vimekuwa vikipambana kudhibiti moto huo hasa katika maeneo ya kusini magharibi ya Antalya na Mugla, kati ya maeneo 100 yaliyokumbwa na moto kwa mara ya kwanza, sita kati yake bado inawaka kutokana na upepo mkali, hatua inayozipa shida juhudi za kuuzima moto huo.
Screenshot_20210802-132833_GBInsta.jpg
 
Kampuni za kutengeneza chanjo ya COVID-19 za Pfizer na Moderna zimepandisha bei ya chanjo katika mikataba yake mipya ya mauzo na Umoja wa Ulaya ambapo Ripoti mpya iliyochapishwa na gazeti la Financial Times iliyotolewa leo Jumapili imenukuu sehemu ya makubaliano hayo ikisema bei mpya ya chanjo ya Pfizer imepanda hadi euro 19.50 (Tsh. 52,288) kutoka euro 15.50 za awali (Tsh. 41,280).

Gazeti hilo limeripoti kuwa dozi ya chanjo ya Mordena iliyokuwa ikiuzwa dola 25.50 (Tsh. 59,117) itauzwa dola 28.50 (Tsh. 66,078) kwenye makubaliano hayo mapya na hii ni kutokana na ongezeko la mahitaji ambapo baada ya bei hizi kupanda juhudi za shirika la habari la Reuters za kupata tamko kutoka kwa kampuni ya Pfizer na Moderna hazikufanikiwa.
Screenshot_20210802-132958_GBInsta.jpg
 
Kampuni za kutengeneza chanjo ya COVID-19 za Pfizer na Moderna zimepandisha bei ya chanjo katika mikataba yake mipya ya mauzo na Umoja wa Ulaya ambapo Ripoti mpya iliyochapishwa na gazeti la Financial Times iliyotolewa leo Jumapili imenukuu sehemu ya makubaliano hayo ikisema bei mpya ya chanjo ya Pfizer imepanda hadi euro 19.50 (Tsh. 52,288) kutoka euro 15.50 za awali (Tsh. 41,280).

Gazeti hilo limeripoti kuwa dozi ya chanjo ya Mordena iliyokuwa ikiuzwa dola 25.50 (Tsh. 59,117) itauzwa dola 28.50 (Tsh. 66,078) kwenye makubaliano hayo mapya na hii ni kutokana na ongezeko la mahitaji ambapo baada ya bei hizi kupanda juhudi za shirika la habari la Reuters za kupata tamko kutoka kwa kampuni ya Pfizer na Moderna hazikufanikiwa. View attachment 1877265
Hiyoya dola 28 ni ujazo gani?
 
Hushpuppi akutwa na hatia ya makosa ya utakatishaji fedha.

Mtu mashuhuri katika mtandao wa Instagram raia wa Nigeria Hushpuppi, ambaye jina lake halisi ni Ramon Abbas, amekiri kosa katika mahakama nchini Marekani la utakatishaji fedha

Alikamatwa, sambamba na washukiwa wengine, huko Dubai mwezi Juni mwaka jana kwa shutuma za ulaghai wa kiasi cha dola milioni 1.1 za Marekani zinazohusishwa na ufadhili wa shule.

Hushpuppi alirejeshwa Marekani ili kuyakabili mashtaka dhidi yake.

Nyaraka zake za kujibu mashtaka zimeonesha kuwa alikiri kuhusika katika sakata ya ufadhili wa shule na vitendo vingine vya ulaghai ikiwemo kinachojulikana kama barua pepe za kibiashara na kuwahadaa watu kupitia mitego iliyohusisha dola milioni 24 taarifa ya Ofisi ya mwendesha mashtaka marekani imesema.
Screenshot_20210802-133805_GBInsta.jpg
 
Ripoti ya Wabunge wa Chama cha Republican cha nchini Marekani iliyochapishwa hii leo imesema kuna ushahidi wa kutosha kwamba virusi vya Corona vilitokea kwenye kituo cha utafiti cha nchini China, ikiwa ni hitimisho ya kile ambacho Taasisi za Kijasusi za Marekani bado hawajaafikiana.

Mbunge Mwandamizi wa Republican katika kamati ya mahusiano ya kigeni Mike McCaul pia ametaja ushahidi wa kutosha kuwa Wanasayansi wa Taasisi ya Wuhan ya utafiti wa virusi, wakisaidiwa na Watalaamu wa Marekani kwa ufadhili wa China na Marekani walikuwa wanatengeza virusi hivyo ili kuathiri Binadamu na udanganyifu kama huo huenda ukafichwa.

Wametaka uchunguzi utakaohusisha Vyama vyote viwili kuhusiana na chimbuko la virusi hivyo.
Screenshot_20210802-194040_GBInsta.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan tayari amewasili Rwanda ambapo amefika Ikulu nchini Rwanda na kupokelewa na Rais Paul Kagame.

Rais Samia ameondoka leo nchini na kuelekea Rwanda kwa ziara ya Kiserikali ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Paul Kagame.
Screenshot_20210802-194307_GBInsta.jpg
Screenshot_20210802-194332_GBInsta.jpg
 
Polisi Mkoani Mtwara wanamshikilia Mwanaume aitwae Hamisi Mmalala kwa tuhuma za kumchoma moto Mtoto wake kwenye vidole kwa kumtuhumu kwamba amemuibia shilingi elfu moja, Kamanda wa Polisi Mark Njera amethibitisha.

Siku ya tukio Dada wa Bashiru alimwambia Baba yao kuwa amepotelewa na Tsh. 1000 na kuhisi kuwa Mtoto huyo wa darasa la tatu ndiye amechukua ndipo Baba akamfungia nyasi mikononi na kumchoma huku akimshikilia ili asikimbie na wala asipige kelele.

Baba huyo amekiri kufanya tukio hilo na kusema hakukusudia kumchoma ila alikuwa akimtishia ili aache tabia yake ya wizi, Mwenyekiti wa kitongoji cha Namivangu Hamisi Mitandi amewataka Wananchi kuendelea kuyafichua mambo ya ukatili yanayotokea katika maeneo yao na kuahidi kumpeleka Hospitali Mtoto huyo.
Screenshot_20210802-194457_GBInsta.jpg
 
Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani amesema leo kuwa hali ya usalama Nchini mwake inaendelea kuzorota na kulalamika kuwa mwenendo huo unatokana na uamuzi wa Marekani wa kuondoa haraka vikosi vyake Nchini humo, ameuambia mkutano wa Bunge mjini Kabul kwamba aliionya Marekani juu ya athari zinatakazojitokeza kwa uamuzi wake wa ghafla wa kuwaondoa Wanajeshi waliobeba dhima ya muda mrefu ya kuwadhibiti Wanamgambo wa Taliban.

Matamshi hayo ya Ghani yanakuja wakati Vikosi vya Afghanistan vinaendelea na mapambano ya kuzuia moja ya miji mikubwa nchini humo kuchukuliwa na Wapiganaji wa Taliban ambapo mapigano yamepamba moto kwenye mji mkuu wa jimbo la Helmand wa Lashkar Gah ambako Taliban wamefanya mashambulizi makali tangu Serikali ilipotangaza kuwa inapeleka mamia ya makomando wa kijeshi kwenye eneo hilo.

Baada ya miaka 20 ya Wanajeshi wa Marekani kuweka kambi zao Nchini Afghanistan, Nchi hiyo imeanza kuyaondoa Majeshi yake Nchini humo na kuiacha Afghanistan ijiendeshe Kijeshi kwa kutumia Wanajeshi wake kitu ambacho kinaonekan ni kigumu kwani Wanamgambo wa Taliban wameanza vita ya kulipa kisali.
Screenshot_20210802-194619_GBInsta.jpg
 
“Tarehe 01 Agosti, 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alifanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Jiji, Manispaa, Miji na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya ambapo Wakurugenzi 70 wamehamishwa vituo vyao vya kazi”

“Wakurugenzi 45 wameendelea kuwepo kwenye vituo vyao vya kazi, Wakurugenzi 69 ni wapya. (Wakurugenzi 15 wamejaza nafasi zilizokua wazi na Wakurugenzi 54 wamechukua nafasi za Wakurugenzi ambao uteuzi wao umetenguliwa).

“Uchambuzi wa awali unaonesha kati ya Wakurugenzi wapya 69 wanawake ni 33 sawa na asilimia 48 hiyo kuwa na idadi ya Wakurugenzi wanawake kuwa 55 sawa na asilimia 29 ya Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa”——— asema Waziri wa TAMISEMI
Screenshot_20210802-194740_GBInsta.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amewataka Wakurugenzi wote wateule wakaripoti kwenye vituo vyao vya kazi kupitia kwa Makatibu Tawala wa Mikoa ndani ya siku tano kuanzia kesho na makabidhiano ya Ofisi yafanyike mara moja.

“Wakurugenzi wawili ambao majina yao yameonekana kutokea kwenye maeneo zaidi ya moja wataripoti kwenye kituo ambacho jina limeonekana kwa mara ya kwanza kwenye orodha ya uteuzi, aidha pale palipojirudia jina patatambulika Kama nafasi wazi na itajazwa hapo baadaye”——— Ummy Mwalimu
Screenshot_20210802-194848_GBInsta.jpg
 
“CHADEMA wanaona Mwenyekiti wao (Mbowe) ameonewa na wanasema hawezi kuwa hivyo wanamuona ni Malaika hawezi kufanya kosa”

“Kabla ya Uchaguzi nilisema kuna Watu wamepanga kuhakikisha Uchaguzi haufanyiki, nilisema kuna baadhi ya Watu wamepanga kulipua visima vya mafuta na kufanya mauaji ya Viongozi na nilisema tutawakamata kabla hawajafanya hivyo”

“Tuliwakamata kabla, hayo ya Mwenyekiti wao (Mbowe) sitaki kuzungumzia sana lipo Mahakama ila wajue yeye ni Binadamu kama Binadamu wengine na anaweza kufanya kosa tumempeleka Mahakamani tuache Mahakama itimize wajibu wake”

“Kama kweli ni mkweli Mwenyekiti wao (Mbowe) na anamuamini Mungu waende wamuulize habari hiyo, kuna mambo unaweza kuyafanya kwamba ni siri lakini ndio mana Vyombo vya Habari vipo, niwaombe Watanzania wenzangu usilolijua ni kama usiku wa giza usiingie kwenye mtego ambao hujui aliyeutega ana jambo gani”

“Waende wamuulize huyo Mtu tuliyempeleka Mahakamani (Mbowe) kwamba hili jambo unalijua na kama ni ukweli ana Dini yake na anamjua Yesu Kristo aende aaambiwe, tunamuonea kwa lipi ?, tupate nini?, tuna ushahidi wa kutosha tuache Mahakama iamue, kafanya Yes hakufanya Yes lakini habari ya kikundi cha Watu kusema tunataka kuandamana wewe ni nani Bro!? hiyo nafasi hauna” ——— asema IGP Simon Sirro akiongea na Waandishi wa Habari leo Dar es salaam.
Screenshot_20210802-195417_GBInsta.jpg
 
“Niwaombe Watanzania tuache wale Watu wachache ambao wanataka kupambana na Serikali wapambane nayo labda wana sababu zake lakini Mtu wenye hekima na busara anielewe, lakini kikubwa kama wameandaa kwenda Canada au Marekani wajiandae ila hatuwezi kuruhusu Watu wachache wavuruge Nchi kwasababu wamekosa madaraka”

“Habari ya kusema mnataka kuandamana mnavunja sheria na ukivunja sheria usilaumu Jeshi, ukivunja sheria umeingia kwenye uhalifu, Sirro hatokuacha na Polisi hawatokuacha na ndio maana wanafanya siasa kwa sababu amani na utulivu upo, Sisi hatufanyi Siasa”

“Niwaombe Watanzania ambao wameambiwa mkusanyike kutoka Mara kutoka wapi sijui na muelewe Mahakamana ni kituo nyeti ni kama Kituo cha Polisi ukitaka kuvamia utakung’utwa kwa mujibu wa sheria sababu umetaka sasa kama kuna Mtu maisha yamemshinda aje ila asije kulalamika, hii kesi iko Mahakamani tuiachie Mahakama iamue” ——— Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro akiongea na Waandishi wa Habari leo DSM. #
Screenshot_20210802-195614_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom