Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210801-070655_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210801-070711_Opera%20Mini.jpg
 
Je unajua kuwa mzazi anaweza athiri akili ya mwanae na mtoto kujikuta na tabia labda isingelikuwa mzazi wake asingezipata?

Baba yake Michael Jackson alikuwa akimuita mwanae nyampua big nose kila mara, kitendo ambacho kilimyima Michael Jackson uwezo wa kujiamini na kumpelekea afanye upasuaji kadha wa kadhaa ili kuwa na pua ndefu hadi kufikia kupata matatizo ya kushindwa kupumua.

Alipo ulizwa alijibu kuwa hakupenda kabisa jina la nyampua na ilimpa wakati mgumu saana kuishi na babake akiwa anamuita hilo jina.
.
.
Je wewe huwa unamwambia nini mtoto wako? Je ulikuwa unajua kuwa unamuathiri mtoto wako kisaikolojia kwa kumwambia maneno ya kero?
Screenshot_20210801-131929_GBInsta.jpg
 
Je unajua Michael Jackson alikuwa anavaa wigi mda wote na hadi mauti kumkuta alikuwa amevaa wigi? Michael Jackson alipata ajali Jan 27 1984, aliungua na baruti ktk tamasha lililo kuwa limeandaliwa na Pepsi, tamasha hilo lilidhaminiwa na Pepsi na walikuwa wamemlipa Michael Jackson milioni tano sawa na B 11,650,000,000 za madafu ( kumbuka pesa hizo alilipwa mwaka 1984 ).

Majeraha ya kuungua yalimpelekea kukosa nywele za utosi hadi kisogoni na kumsababishia kuwa na maumivu ya kichwa hapa na pale pia kutumia dawa za maumivu kila mara.

Japokuwa Michael Jackson aliendelea kuishi na maumivu hayo , kampuni ya Pepsi iliweza kumlipa dola milioni 10 za kimarekani ili aendelee kufanya kazi na kampuni ya Pepsi.

Michael Jackson alikuwa anasumbuliwa pia na maradhi ya kupumua kwa sababu ya kufanya upasuaji wa pua yake ili ionekane ndogo pia alipatikana na ugonjwa wa "Lupus".

Lupus ni miongoni mwa magonjwa sugu, ambapo kinga za mwili wa binadamu badala ya kumlinda hugeuka na kuanza kumshambulia.

Ugonjwa huo ulimsababishia Michael Jackson kuvimba mkono na mara nyingi kuonekana akiwa amevaa gloves mikononi kwa nia ya kuficha uvimbe na kutotisha mashabiki wake.


Screenshot_20210801-132323_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-132340_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-132355_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-132411_GBInsta.jpg
 
Tuendelee kumjua muimbaji mashuhuri hapa duniani Michael Jackson, ambae awali niliandika magonjwa aliyo kuwa nayo na yalikuwa yakimtatiza saana maishani mwake.

Michael Jackson alikuwa pia na ugonjwa unao itwa VITILIGO.

Vitiligo ni hali ya ngozi kupoteza rangi yake na kuacha madoa/ mabaka katika sehemu fulani za mwili hasa zile zinazopata mwanga wa jua haraka kama mikono, uso na macho.

Hali hii husababishwa na seli zinazoipa ngozi rangi ya mwili zijulikanazo kama Melanocyte kufa au kushindwa kufanya kazi.

Kabla Michael Jackson hajakubaliana na ugonjwa huo alikuwa akitumia make up kuficha huo ugonjwa kwa mashabiki wake na kujikuta jasho likimtoka na ile makeup aliyo paka hutoweka na kuacha mabaka yakionekana.

Hali hiyo ilimpa stress saana ndipo alipo amua kujichubua mwili mzima ili ngozi yake ifanane na si kuwa alikataa kutambulika kama mtu Mweusi.

Baada ya Michael Jackson kubadilisha rangi yake ya mwili kuna baadhi ya fans hawakumuelewa na wakampa jina jako.

jina hilo lilimkera saana Michael Jackson kila mara alipo lisikia. Na ndipo alipo amua kufanya interview na oprah winfrey kuwaeleza fans wake kilicho jiri.

Pia fans walimtania saana Michael Jackson kuwa si rijari kwa kuwa alitengeneza uso wake na kufanana kama dada akee Jannet Jackson.

Pia kitendo hicho kilimkwaza na akaamua kufanya upasuaji wa kuongeza ukubwa wa taya ya chini ya meno ili uso uwe na muonekano wa kiume na si wakike angalia kuanzia picha ya 7 muonekano wake baada
ya upasuaji huo.
Screenshot_20210801-132930_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-132959_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-133019_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-133037_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-133052_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-133108_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-133128_GBInsta.jpg
 
Mgahawa wa Serendipity 3 uliopo New York Marekani wiki hii umevunja rekodi kwa kuonesha sahani ya ‘chips’
wanazotengeneza ambazo wanauza $ 200 ambayo kwa pesa za Tanzania shilingi laki nne na elfu sitini na tatu na mia tano na sita ambapo Taarifa ya Mgahawa huo imesema mapishi ya viazi hivyo yana utofauti na mapishi yaliyozoeleka.

Mgahawa huu tayari upo kwenye kitabu cha rekodi za kipekee duniani cha Guinness kwa kuwa na burger ya bei ghali zaidi duniani ambayo inauzwa $ 295 ambayo kwa pesa za Tanzania ni laki sita na elfu themanini na tatu na mia sita sabini na mbili.
Screenshot_20210801-203252_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-203313_GBInsta.jpg
 
Baada ya Wanajeshi wa Marekani kutangaza kuondoka Afghanistan baada ya miaka 20 ya vita, kundi la kwanza la Raia 221 kati ya 2500 wa Afghanistan ambao walifanya kazi na Wanajeshi hao limewasili kwa Ndege Washington DC Marekani kuanza maisha mapya baada ya Marekani kuwapatia hifadhi ili kukwepa kuuwawa na Wapiganaji wa Taliban.

Chini ya mpango huu wa visa maalum uliidhinishwa na Bunge la Marekani mwaka 2006 ili kuwapatia hifadhi Raia wa Iraq na Afghanistan ambao wamehatarisha maisha yao kwa kufanya kazi na Serikali ya Marekani.

Kwa jumla Marekani na Washirika wake (Nchi nyingine) wanalenga kuwapatia hifadhi Raia 50,000 wa Afghanistan katika juhudi za kuwalinda dhidi ya uwezekano wa kulengwa na kundi la Wanamgambo wa Taliban ambalo liliondolewa madarakani wakati vikosi vya kigeni vilipoingia Afghanistan mwanzoni mwa miaka ya 2000.
Screenshot_20210801-203503_GBInsta.jpg
 
Serikali ya Rwanda imeamuru kuondolewa kwa vizuizi vya Watu kutotoka nje ambavyo viliweka kukabiliana na virusi vya corona katika mji mkuu wa taifa hilo Kigali na Wilaya nyingine nane, vizuizi hivi vimeondolewa pamoja na kwamba maambukizi yanazidi kuongezeka.

Taarifa hii imetolewa baada ya mkutano wa Baraza la Mawaziri uliongozwa na Rais Paul Kagame na kusema marufuku hii imeondolewa kuanzia Agosti 1 hadi 15.

Safari za ndani za Kigali na majimbo na Wilaya zinaweza kuanza upya lakini marufuku ya kutembea nyakati za usiku itaendelea kubaki palepale, mikusanyiko yote pia imepigwa marufuku huku Shule na Makanisa vikiendelea kufungwa japo Watu wanaotaka kufunga ndoa wataruhusiwa lakini kwa idadi ya Watu wachache tu kuhudhuria ambao hawatakiwi kuzidi 10.

Kwa mujibu wa takwimu za jana, Ijumaa Rwanda ilikua na maambukizi karibu 70,000 ya covid-19 huku vifo vikifikia 798 ambapo pia katika kipindi cha siku 7 zilizopita Taifa hilo limerekodi maambuzi ya zaidi ya Watu 1,000 kila siku.
Screenshot_20210801-203654_GBInsta.jpg
 
Kwenye list ya habari kubwa za wiki hii imo hii ya Saif al-Islam Mtoto wa aliyekua Rais wa Libya Muammar Muhammad Abu Minyar al-Gaddafi ambapo baada ya miaka 10 ya ukimya, ameibuka na kusema yupo hai na anataka kurudi kuiongoza Libya na kuliunda upya taifa hilo ambalo sasa limepasuka vipandevipande.

Wiki hii New York Times wamemuhoji Islam mwenye umri wa miaka 49 ambae anasema toka kuuwawa kwa Baba yake October 20 2011 Watu wa Libya wamekua wakiishi kwa kuteseka na hakuna chochote bora walichokipata kutoka kwa Watu wanaoiongoza Libya kwa sasa.

Islam ameahidi kurudi tena kufanya siasa kwenye Taifa lake analolipenda na kuongeza kuwa hakuna tena uhasama kati yake na Watu waliowahi kumfunga jela na kumtesa baada ya Baba yake kuuwawa na sasa Watu hao ni Marafiki zake.

Hata hivyo Saif Al Islam ambae ana PhD aliyoipata London School of Economics amekua akitafutwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za uhalifu wa kivita akishutumiwa kuchochea mauaji ya Waandamanaji waliokuwa wakipinga utawala wa baba yake.

Muammar Gaddafi aliiongoza Libya kwa karibu miaka 40 na Taifa hilo lilitajwa kuwa na utulivu na Wananchi kuishi maisha bora tofauti na wanayoishi sasa baada ya kuuwawa kwake mwaka 2011 na Waasi kuibuka, Watoto 7 wa Gaddafi waliuwawa kwenye machafuko hayo ya mwaka 2011 lakini Islam alifanikiwa kuepuka kifo.
Screenshot_20210801-203835_GBInsta.jpg
 
Wizara ya Afya imesema ugawaji wa chanjo umezingatia taarifa ya maambukizi ya Wagonjwa wanaohisiwa kuwa na COVID-19, idadi ya walengwa kwa kundi la kipaumbele pamoja na idadi ya chanjo
zilizopatikana kwa sasa.

Wizara imesema kutokana na muongozo wa chanjo wa Taifa dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19 wa Shirika la Afya Duniani (WHO), maelekezo ya Covax Facility na upungufu wa uzalishaji wa chanjo toka viwandani chanjo hizo kwa sasa zinatolewa kwa kufuata
vipaumbele vya makundi yenye uhitaji mkubwa.

Makundi ambayo yataanza chanjo ni pamoja na Watumishi wa sekta ya Afya (Umma na Binafsi), Watu wazima umri wa miaka 50 na kuendelea na Watu wenye magonjwa sugu na ya muda mrefu———“makundi mengine ya Wananchi yatapata chanjo katika Awamu inayofuata”
Screenshot_20210801-204029_GBInsta.jpg
 
Wizara ya Afya imesema itaanza kutoa chanjo ya COVID 19 kwenye mikoa yote Tanzania kuanzia August 03, 2021 ambapo mambo ya kuzingatia kabla ya kuchanjwa ni kujitathmini kama upo kwenye makundi ya Walengwa.

Jingine ni kuandaa kitambulisho chako cha kazi, NIDA, Leseni ya Udereva, cha Mpiga kura, pasi ya kusafiria (passport) au kitambulisho chochote kinachotambulika kisheria.

Kingine ni kufanya booking ya siku ya kuchanjwa mtandaoni kupitia www.chanjocovid.moh.go.tz au kwenda moja kwa moja kwenye kituo na kujisajili kuanzia August 02,2021 na kujaza fomu ya uhiari wa kuchanjwa.
Screenshot_20210801-204200_GBInsta.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu ameitaka Jamii iache kuwa na dhana potofu kwamba Mtu akionekana amebeba kondomu ni muhuni bali Jamii ijifunze kujilinda na maambukizi yatokanayo na ngono zembe ambazo zimekua zikiharibu maisha ya Watu.

Ummy ameyasema hayo Dodoma alipokuwa anazindua uwekaji wa makasha ya kusambazia kondomu maeneo ya Watu na maeneo yenye mikusanyiko ambapo ameeleza kwamba takwimu zinaonesha kwa mwaka takribani Watu Elfu 72 wanaambukizwa virusi vya UKIMWI nchini Tanzania.

Waziri Ummy amewaagiza Watendaji wa TAMISEMI kwa kushirikiana na TAYOA kuhakikisha wanasambaza makasha hayo na kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI hadi Vijijini ambapo baadhi ya jamii haina uelewa wa kutosha kuhusu ugonjwa huo.

Makasha hayo tayari yamefika kwenye Halmashauri 169 kati ya Halmashauri 184 kwa Tanzania Bara.
Screenshot_20210801-204619_GBInsta.jpg
 
Kwenye matukio ya wiki hii Jijini Arusha, Polisi wamethibitisha kufariki kwa Jacobo Kideku maarufu kama Wami au kichwaa (43) Mkazi wa kata ya Makiba wilayani Arumeru ambaye alikua akituhumiwa kwa mauaji ya Askari Polisi Damasi Magoti aliyefariki kwa kukatwa na panga kichwani alipokwenda kumkamata Mtuhumiwa huyo.

Kamanda wa Polisi Arusha Justine Masejo amesema Mtuhumiwa huyo alifuatwa Mkoani Morogoro alipokimbilia kujificha na baada ya kukamatwa na kurudishwa Arusha alijirusha kutoka kwenye gari walipofika maeneo ya Kisongo.

"Akiwa amefungwa pingu mkononi alijirusha kutoka kwenye gari lilikua kwenye mwendo kasi na kusababisha majeraha kichwani na michubuko katika mwili wake, alifariki akiwa njiani akiwaishwa Hospitali Mount Meru"

"Hata hivyo imebainika kwamba kabla ya tukio la kumuua Askari Polisi Marehemu Jacobo Kideku alikua akitafutwa na Jeshi la Magereza ambapo tarehe 10 September 2018 alifungwa kifungo cha miaka 15 kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia nguvu na kosa la pili shambulio na la tatu kutoroka chini ya ulinzi"

"Mtuhumiwa huyu akiwa anaendelea kutumikia kifungo chake magereza kilichotarajiwa kumalizika mwaka 2026 alitoroka akiwa chini ya ulinzi wa Askari Magereza tarehe 1 April 2017" ——— RPC Arusha, Justin Masejo.
Screenshot_20210801-204821_GBInsta.jpg
 
Mgahawa wa Serendipity 3 uliopo New York Marekani wiki hii umevunja rekodi kwa kuonesha sahani ya ‘chips’
wanazotengeneza ambazo wanauza $ 200 ambayo kwa pesa za Tanzania shilingi laki nne na elfu sitini na tatu na mia tano na sita ambapo Taarifa ya Mgahawa huo imesema mapishi ya viazi hivyo yana utofauti na mapishi yaliyozoeleka.

Mgahawa huu tayari upo kwenye kitabu cha rekodi za kipekee duniani cha Guinness kwa kuwa na burger ya bei ghali zaidi duniani ambayo inauzwa $ 295 ambayo kwa pesa za Tanzania ni laki sita na elfu themanini na tatu na mia sita sabini na mbili. View attachment 1876717View attachment 1876718
Itakua wamezijaza makorokoro...
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu ameitaka Jamii iache kuwa na dhana potofu kwamba Mtu akionekana amebeba kondomu ni muhuni bali Jamii ijifunze kujilinda na maambukizi yatokanayo na ngono zembe ambazo zimekua zikiharibu maisha ya Watu.

Ummy ameyasema hayo Dodoma alipokuwa anazindua uwekaji wa makasha ya kusambazia kondomu maeneo ya Watu na maeneo yenye mikusanyiko ambapo ameeleza kwamba takwimu zinaonesha kwa mwaka takribani Watu Elfu 72 wanaambukizwa virusi vya UKIMWI nchini Tanzania.

Waziri Ummy amewaagiza Watendaji wa TAMISEMI kwa kushirikiana na TAYOA kuhakikisha wanasambaza makasha hayo na kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI hadi Vijijini ambapo baadhi ya jamii haina uelewa wa kutosha kuhusu ugonjwa huo.

Makasha hayo tayari yamefika kwenye Halmashauri 169 kati ya Halmashauri 184 kwa Tanzania Bara.View attachment 1876737
😅😅
Nikikukuta umehifadhi condom au kubeba lazima unitambue au unieleze..
 
Zaidi ya Polisi 3,000 na Maofisa wengine wa usalama wa Ufaransa waliuzunguka Mji Mkuu wa Ufaransa Paris jana Jumamosi ikiwa ni jumamosi ya tatu ya maandamano wakati maelfu ya Waandamanaji wakipinga mpango wa Serikali wa kuanzisha passport au pasi maalumu itakayokua ikitumika na waliopata chanjo dhidi ya virusi vya corona tu.

Nchini kote Ufaransa, Watu wapatao 204,000 wameshiriki maandamano hayo ambapo idadi hiyo ya Waandamanaji imeongezeka ikilinganishwa na ile ya wikiendi iliyopita, ndani ya Paris Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya Waandamanaji katika mikusanyiko minne tofauti mjini humo.

Kuanzia Agosti 9 pasi hizo mpya za afya zitahitajika kwa Raia kuweza kusafiri na kuingia kwenye maeneo ya biashara, kama vile migahawa, vinyozi, pamoja na kupanda kwenye treni au kushiriki kwenye maonyesho tofauti, pendekezo hilo bado linasubiri idhini ya kupitishwa na Baraza la Katiba ambapo itafanya upigaji wa chanjo hiyo ya virusi vya corona kuwa lazima kwa baadhi ya Wafanyakazi.

Maambukizi ya corona yaliyotokana na aina mpya ya kirusi iitwayo Delta yameongezeka nchini Ufaransa ambapo kwa Ijumaa pekee kumeripotiwa maambukizi mapya ya Watu 24,000 huku utafiti ukionesha kuwa Watu ambao bado hawajapata chanjo ni asilimia 85 ya wanaougua COVID-19 hospitalini ikiwa ni pamoja na wale waliolazwa kwenye vyumba vya kutunza wagonjwa mahatuti.

Watu wapatao 112,000 wamefariki dunia Ufaransa kutokana na virusi vya corona tangu janga hilo kuanza mwaka jana na hadi sasa asilimia 52 ya Watu wa Ufaransa wameshachanjwa.
Screenshot_20210801-210405_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-210423_GBInsta.jpg
Screenshot_20210801-210439_GBInsta.jpg
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza masharti mapya ya kupambana na Corona ambapo amesema ni marufuku kwa Watu kutembea usiku kuanzia saa moja usiku hadi 11:30 alfajiri.

“Watu wote wanapaswa kubaki Majumbani, wanaoruhusiwa kutembea usiku ni Watu wa Ulinzi na Usalama na makundi mengine yaliyopewa ruhusa”

“Baa zitaendelea kufungwa na Askari wanapaswa kuwakamata na kuwatoza faini Wamiliki wa Baa wanaokiuka agizo” ———Museveni.

“Bodaboda wanaruhusiwa kufanya kazi ila mwisho ni saa 12 Jioni na wanapaswa kubeba abiria mmoja (sio mshikaki) au mizigo” ———Museveni.
Screenshot_20210801-210847_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom