Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,937
Mbunge wa Mlimba Mkoani Morogoro, Godwin Kunambi, amefanikisha ujenzi wa Daraja la muda la mbao katika Mto Mngeta wenye mamba ambalo kwa muda mrefu limekuwa likihatarisha maisha ya wananchi wa Kata ya Mngeta, Kunambi amesema ujenzi wa daraja hilo la muda umegharimu Tsh. Milioni 31.
Wananchi wa Kata ya Mngeta kwa muda mrefu wamekuwa wakipata changamoto ya kivuko katika Mto huo wenye Mamba ambapo mara kadhaa wamesababisha vifo vya Wananchi waliokuwa wakivuka Mto huo kwenda upande wa pili kufanya shughuli zao za kila siku.
"Fabruary mwaka huu nilikuja hapa kujionea changamoto hii ya kivuko na nikawaahidi kwamba hakuna Mwananchi mwingine ambaye ataliwa na Mamba Mimi nikiwa Mbunge wenu, imani mliyonipa mimi na Rais wetu Samia Suluhu Hassan ndio ambayo imelipa leo ambapo sasa tumekamilisha ujenzi wa daraja hili la muda lililogharimu kiasi cha TSh. Milioni 31”———KUNAMBI
“Lengo langu kama Mbunge wenu ni kuhakikisha tunapata Daraja la kudumu ili kuondoa kero hii lakini kwa hatua hii ya kuweka kivuko cha muda ninaimani kuwa kutachochea maendeleo ya Wananchi wetu na kuongeza usalama kwa watumiaji wanaopita hapa”———- Kunambi
Wananchi wa Kata ya Mngeta kwa muda mrefu wamekuwa wakipata changamoto ya kivuko katika Mto huo wenye Mamba ambapo mara kadhaa wamesababisha vifo vya Wananchi waliokuwa wakivuka Mto huo kwenda upande wa pili kufanya shughuli zao za kila siku.
"Fabruary mwaka huu nilikuja hapa kujionea changamoto hii ya kivuko na nikawaahidi kwamba hakuna Mwananchi mwingine ambaye ataliwa na Mamba Mimi nikiwa Mbunge wenu, imani mliyonipa mimi na Rais wetu Samia Suluhu Hassan ndio ambayo imelipa leo ambapo sasa tumekamilisha ujenzi wa daraja hili la muda lililogharimu kiasi cha TSh. Milioni 31”———KUNAMBI
“Lengo langu kama Mbunge wenu ni kuhakikisha tunapata Daraja la kudumu ili kuondoa kero hii lakini kwa hatua hii ya kuweka kivuko cha muda ninaimani kuwa kutachochea maendeleo ya Wananchi wetu na kuongeza usalama kwa watumiaji wanaopita hapa”———- Kunambi