Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210417_060044.jpg
20210417_060109.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Dkt. Mussa Julius Lulandala kuwa Msaidizi wa Rais Nyaraka na Ukalimani (PAP- TD), amemteua pia Balozi Ali Bujiku Sakila Kuwa Msaidizi wa Rais Hotuba (PAP- DA).
20210417_114732.jpg
 
Rais Samia Suluhu amemteua Said Ali Juma kuwa Mnikulu, amemteua pia Maulidah Bwanaheri Hassan kuwa Msaidizi wa Rais, Diplomasia (PAP-DA), pia amemteua Bi.Felister Peter Mdemu kuwa Msaidizi wa Rais, Maendeleo ya Jamii.
20210417_114833.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Nehemia Ernest Mandia kuwa Msaidizi wa Rais, Sheria (PAP-LA), amemteua pia Dkt. Salim Othman kuwa Msaidizi wa Rais, Siasa (PAP- PA).
20210417_114934.jpg
 
Muonekano wa Daraja la Tanzanite ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 71.3 na linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu, ujenzi wa Daraja hili linalopita katika Bahari ya Hindi Jijini Dar es Salaam unagharimu Tsh. Bilioni 243 na litasaidia kupunguza foleni za Dar es Salaam. (swipe kuona picha nyingine)
20210417_115228.jpg
20210417_115249.jpg
20210417_115308.jpg
 
Mshambuliaji wa Yanga Ditram Nchimbi hadi sasa amecheza mwaka mmoja na siku 47 bila kuifungia Yanga goli, mara ya ya mwisho Nchimbi kufunga Ilikuwa February 29 2020.

“Sijafunga muda mrefu Mimi binafsi sijisikii vizuri na sina furaha kwasababu najua Wana Yanga wanajua kile kitu ninacho, kwahiyo matarajio yao kuniona nafunga”———Nchimbi

“Mimi naamini mvua itakapoanza kunyesha ndio muda wa kupanda mahindi, naamini kuanzia mechi ijayo nikipata nafasi nitafunga magoli”———Ditram Nchimbi akizungumza kupitia YANGA TV
20210417_141006.jpg
 
Club ya Sepsi OSK ya Romania imeripotiwa kukubali ofa ya Euro 700,000 (Tsh Bilioni 1.9) kutoka Club ya Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini ili imuachie Pavol Safranko (26) ajiunge nao.

Mshambuliaji huyo Pavol ambaye ni Raia wa Slovakia amefunga magoli 7, assist 4 katika michezo 25 akiwa na Sepsi OSK huku usajili huo ukitajwa kuwa mkubwa zaidi kuwahi kufanyika katika historia ya Club hiyo ya Ligi Kuu Romania.

Pavol amewahi kucheza Timu ya Taifa ya Slovakia akicheza jumla ya mechi 10, habari hii inakuwa kubwa Afrika sababu ni nadra sana Wachezaji wanaocheza Ligi Kubwa Ulaya au Bara la America kuja Afrika ila Mamelod wameanza kuonesha njia kwa kuwaleta watu kama Gaston Sirino kutokea Uruguay na kuonesha uwezo mkubwa.

Ukiangalia katika viwango vya soka duniani vya FIFA, Taifa la Slovakia analotokea Pavol liko nafasi ya 36 kwa ubora huku Romania anakocheza wako nafasi ya 43 kidunia na anakuja Afrika Kusini katika Taifa lililo nafasi ya 75 hivyo inatafsirila kama dalili njema kwa Soka la Afrika kuleta wachezaji wa viwango.
20210417_141116.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride leo April 17, 2021 wakati wa zoezi la kuwatunuku Kamisheni Maafisa 393 wa kundi la 1/2017 na kundi la 68/2020 katika Uwanja wa Paredi uliopo Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.
20210417_162549.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan akitoa zawadi kwa Maafisa waliofanya vizuri zaidi wakati wa mafunzo, zawadi hizo amezitoa leo April 17, 2021 wakati wa zoezi linaloendelea muda huu la kuwatunuku Kamisheni Maafisa 393 wa kundi la 1/2017 na kundi la 68/2020 katika Uwanja wa Paredi uliopo Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.
20210417_162656.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan leo April 17, 2021 amewatanuku Kamisheni Maafisa 393 wa kundi la 1/2017 na kundi la 68/2020 katika Uwanja wa Paredi uliopo Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.
20210417_162913.jpg
 
Staa wa Juventus Cristiano Ronaldo atakosekana katika mchezo wa Serie A kesho ugenini dhidi ya Atalanta kutokana na kusumbuliwa na misuli.

Kocha wa Juventus Andrea Pirlo amethibitisha hilo na kueleza kuwa Ronaldo hatokuwa sehemu ya mchezo na hataki kumtumia kwa kuogopa kusababisha tatizo kuwa kubwa zaidi.

“Ronaldo hatohusika katika mchezo huo bado hajapona tatizo lake la misuli, kumchezesha kesho ni kumuweka katika hatari ya kuumia zaidi”———Pirlo

“Safari za anga, mechi za usiku na kuwa na mechi mfululizo hakukumpa muda wa kujiuguza na kupona, tuliamua kumuacha apumzike na tunatumaini Jumatano atakuwa sa”———Pirlo
20210417_182610.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom