Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mtanzania Thomas Ulimwengu baada ya kukosekana katika michezo kadhaa ya TP Mazembe akisumbuliwa na enka jana amerudi uwanjani na kuisaidia Timu yake kupata ushindi wa magoli 4-1 dhidi AC Rangers katika mchezo wa Ligi Kuu Congo DR, Ulimwengu aliyeibuka Man Of The Match alifunga magoli mawili na kusababisha penati
20210415_130103.jpg
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Selemani Jafo amepanga kukutana na Wawekezaji wote wenye changamoto za kimazingira nchini April 17, 2021 kwa ajili ya kujua changamoto zinazowakwamisha lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi.

Waziri Jafo ameyasema hayo leo akiwa katika Ofisi za NEMC Dar es Salaam.

“April 17 Jumamosi nimewaita Wawekezaji wote ambao wanachangamoto za environmental impact assessment nataka niwasikilize wamekwama wapi na Watu wengine mbalimbali ambao wapo katika eneo hilo, lengo langu nataka tuboreshe utendaji kazi nataka Wizara ya Uwekezaji iweze kufanya kazi vizuri, pia Wizara ya Viwanda na Biashara iweze kufanya kazi vizuri, Mimi ni kama kiunganishi chawao kufanya kazi vizuri”———JAFO
20210415_130222.jpg
 
Rais wa Chama cha Soka Rwanda (FERWAFA) Brigedia Jenerali Mstaafu Sekamana Jean Damascene amejiuzulu nafasi hiyo ya Urais wa FERWAFA kwa kile alichodai chanzo ni sababu binafsi na mambo yake ya kifamilia.
20210415_130415.jpg
 
Kufuatia agizo la Rais Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo chini ya Waziri Innocent Bashungwa pamoja na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari chini ya Waziri Dr. Faustine Ndugulile na zimetatua changamoto mbalimbali zinazotokana na sheria na tararibu za TCRA katika sekta za utangazaji na sanaa.

Kikao cha Mawaziri wa Wizara hizo kilifuatiwa na kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara hizo, miongoni mwa mambo mengi waliyoagiza ni pamoja na kuitaka TCRA kupitia upya kanuni upya ili kupunguza ada za usajili ama kuhuisha usajili wa Online TV———“mapitio ya kanuni yafanyiwe kazi haraka sana ili Bei ya usajili ipungue na kuwasaidie Vijana wengi kujiajiri”

Kwa sasa Blogu, Online Forum na Waombaji wapya wa Radio na Television Mtandaoni wasio na leseni ya Utangazaji unaotumia mitambo iliyosimikwa ardhini hulipia Laki moja ya gharama ya maombi ya usajili, ada ya kupatiwa leseni ni Tsh. Milioni moja, ada ya mwaka ya leseni ni Tsh. Milioni moja na gharama ya kuhuhusisha (Renew) leseni ni Tsh. Milioni moja.

Leseni zote ni za miaka mitatu ambapo baada ya muda huo huitajika kuomba kuhuishwa na kupewa Leseni nyingine kwa anayekidhi vigezo husika.
20210415_130525.jpg
 
Club ya Al Ahly Benghazi ya Libya itatuma malalamiko yake CAF na kuomba uchunguzi ufanyikea baada ya Wachezaji wao watano na Kocha wao Msaidizi kupima na kukutwa na Corona kabla ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Orlando Pirates nchini Afrika Kusini na kupoteza 3-0 ila wakati wanapima kwa ajili ya kuondoka Afrika Kusini wote majibu yakatoka Negative wanaamini hujuma zilifanyika.
20210415_134759.jpg
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa leo amekutana na Mtendaji Mkuu wa Timu ya Simba Sports Club Babra Gonzalez kujadili mgogoro kati ya Timu hiyo na Tume ya Ushindani (FCC).

Waziri Bashungwa amemhakikishia CEO wa Simba SC kwamba maendeleo ya michezo ikiwemo Soka ni moja ya vipaumbele muhimu sana kwa Serikali na Watanzania na ataishirikisha Wizara ya Viwanda na Biashara ili kuupatia suluhu mgogoro huo wa Simba SC na FCC.

Simba SC imekuwa katika mvutano wa kufikia tamati ya mfumo wa mabadiliko wa Club ya Simba, Simba kupitia kwa Muwekezaji wao MO Dewji amekuwa akidai kuwa FCC inakwamisha kukamilika kwa mfumo wa mabadiliko ndani ya Simba.
20210415_142655.jpg
 
Staa wa AC Milan, Raia wa Sweden Zlatan Ibrahimovic (39) anaweza kufungiwa miaka mitatu kucheza soka na faini ya Krona Milioni 1 (Tsh Milioni 273.6) kwa kosa la kumiliki kampuni ya betting (bethard) taarifa iliyotolewa na gazeti la Sweden la Aftonbladet imethibitisha.

Zlatan anadaiwa kumiliki asilimia 10 ya hisa za kampuni ya betting, CEO wa kampuni hiyo iliyosajiliwa Malta amethibitisha Zlatan kuwa Mmiliki mwenza wa kampuni hiyo.

Kama FIFA na UEFA wakifanya uchunguzi na kuthibitisha hilo Zlatan Ibrahimovic atafungiwa miaka mitatu na faini sababu sheria za FIFA haziruhusu Mchezaji kushiriki betting au kuwa sehemu ya umiliki kwa kuondoa mambo ya kupanga matokeo.
20210415_154442.jpg
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima, leo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright Kwenye Ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Katika mazungumzo yao wameongelea maeneo ya mashirikiano ikiwemo kuboresha afya ya Watanzania pamoja na kuwawezesha Vijana wa Tanzania kiuchumi.

Katika kikao hicho kilihudhuriwa na Manaibu Waziri Dkt.Godwin Mollel, Mwanaidi Khamis pamoja na Katibu Mkuu-Afya Prof. Abel Makubi na Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Naftali Ng'ondi.
20210415_154708.jpg
 
Muamuzi Mohamed Ali Adelaid amefungiwa miezi mitatu kuchezesha soka na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) baada ya kuchezesha kiwango cha chini.

Adelaid Raia wa Comoro amepewa adhabu hiyo baada ya kuchezesha chini ya kiwango mchezo wa kuwania kufuzu AFCON 2021 kati ya Algeria na Zambia March 25 2021 na kupelekea FA ya Algeria kupeleka malalamiko CAF.
20210415_154853.jpg
 
Bodi ya maadili ya UEFA imeipiga faini ya Pound 6,000 (Tsh Milioni 19.1) Club ya Man United kwa kosa la Wachezaji wake kuoneshwa kadi 5 za njano katika mchezo wa Europa League dhidi ya Granada.
20210415_172506.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom