Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210414_054310.jpg
20210414_054332.jpg
 
“Rais wetu Mama Samia alikuja hapa Chunya kwenye Kampeni mwaka jana na safari hii atakuja tena, ametushauri sisi aliotuteua kwamba akifika Wananchi mkanyoosha mabango ya kero halafu tukawanyang’anya mabango anatufukuza siku hiyohiyo, Mimi sipo tayari kufukuzwa”———Albert Chalamila, RC Mbeya

“Mimi sipo tayari kufukuzwa, sipo tayari kuyaona mabango na sipo tayari kuwanyang’anya kwahiyo wenzangu waje wasikilize kero haraka akija kusikiliza Rais tumeliwa na Mimi akiniuliza nasema ni DC huyo nilimtuma akuja na yeye anajua wapi ashushe, najua na nyinyi Wananchi mtasema Mkuu wa Mkoa safi” ——-Chalamila
20210414_122553.jpg
 
Robin Gosens wa Club ya Atalanta ya Italia hivi karibuni alieleza masikitiko yake kwa kugomewa na Cristiano Ronaldo wa Juventus kubadilishana jezi.

Robin (26) ni Shabiki na anamtazama Ronaldo kama role model wake lakini 2019 katika robo fainali ya Coppa Italia baada ya kuitoa Juventus kwa ushindi wa 3-0, baada ya mchezo alimfuata Ronaldo na kumuomba wabadilishane jezi lakini Ronaldo alikataa kwa kumwambia Hapana huku akiwa hamuangalii hata usoni, Gosens hivi karibuni alieleza kuumizwa na tukio hilo.

“Baada ya mchezo nilijaribu kutimiza ndoto yangu hata sikushangilia na wenzangu nikamfuata Ronaldo kutaka kutimiza ndoto ya kuwa na jezi yake kwa kubadilishana lakini alijibu Hapana hata hakuniangalia usoni”

Sasa baada ya wachezaji wenzake wa Atalanta kusikia hilo kupitia interview aliyoifanya hivi karibuni waliamua kum-surprise kwa kumnunulia jezi ya Juventus ya Cristiano Ronaldo na kumpatia kama zawadi
20210414_122843.jpg
 
Simba SC baada ya kumalizana na hatua ya Makundi Afrika leo watarejea Uwanja wa Mkapa kuikabili Mtibwa Sugar katika muendelezo wa michezo ya Ligi Kuu Tanzania bara 2020/21.

Kuelekea mchezo huo Nahodha Msaidizi Simba SC Mohamed Hussein ameweka wazi kuwa licha ya kuulizwa sana kuhusu Ubingwa hususani Yanga mpinzani wao akiongoza Ligi akiwa kawazidi michezo na kama Simba wakishinda mechi za viporo wanaweza kukaa kileleni.

“Suala la Ubingwa naweza kusema kila mmoja ashinde mechi zake, sababu ukiangalia sana mwenzako anafanya nini focus (malengo) yako inaweza ikapotea sisi kama Wachezaji target yetu kila mechi ni kupata point 3”———Mohamed Hussein

Yanga SC kwa anaongoza Ligi kwa kuwa na point 51 akiwa amecheza michezo 24 wakati Simba SC wakiwa nafasi ya tatu kwa kuwa na point 46 akiwa kacheza michezo 20, Yanga akiwa mbele kwa michezo minne.
20210414_123015.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom