Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ally Hassan Mwinyi akiwasili Uwanja wa Magufuli, Chato inapofanyika Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
20210326_131116.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alivyowasili Uwanja wa Magufuli, Chato inapofanyika Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
20210326_131343.jpg
20210326_131409.jpg
20210326_131436.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alivyowasili Uwanja wa Magufuli, Chato inapofanyika Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
20210326_131604.jpg
 
Wasanii mbalimbali wakiwa wamejumuika na Waombolezaji wengine katika Uwanja wa Magufuli, Chato inapofanyika Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
20210326_131719.jpg
20210326_131737.jpg
20210326_131818.jpg
20210326_131836.jpg
20210326_131853.jpg
 
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ataitwa pia Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania na sio Amirat kama ambavyo ilipendekezwa———“Nashukuru Baraza la Kiswahili limerekebisha uendelee kuitwa Amiri Jeshi Mkuu na sio Amirat kama ilivyokuwa inapendekezwa”

Mabeyo ametoa kauli hiyo kwenye Uwanja wa Magufuli Chato leo wakati akitoa salamu kwenye Misa Takatifu ya Mazishi ya Hayati Dr.John Pombe Magufuli.
20210326_132238.jpg
 
“Nilipokuwa Rais, Hayati Magufuli alikuwa ni mmoja ya Mawaziri niliowaamini na kuwatumaini, alikuwa jembe langu, ndio maana nilimuweka kwenye Wizara tatu zilizokuwa ngumu anyooshe mambo” - Rais Mstaafu, Dr.Jakaya Kikwete Msibani Chato leo

"Alipojitokeza kuomba uteuzi wa kuwa mgombea wa Urais wa CCM mwaka 2015, sikusita kumpendekeza katika majina matano niliyoyafikisha kwenye kikao cha juu cha chama, sikuwa na tabu na Magufuli ndio jina la kwanza halafu yakafuata mengine”- Rais Mstaafu Dr. Kikwete

“Mheshimiwa Magufuli alinitunuku Kiwanja hapa Chato, kipindi akiwa Mbunge na Waziri, alipokuwa Rais akaongeza eneo, ilikuwa matarajio yangu kujenga nyumba, ili siku akistaafu tuendelee kupiga soga hapa Chato”- Dr.Kikwete
20210326_155503.jpg
 
“Nilipokuwa Rais, Hayati Magufuli alikuwa ni mmoja ya Mawaziri niliowaamini na kuwatumaini, alikuwa jembe langu, ndio maana nilimuweka kwenye Wizara tatu zilizokuwa ngumu anyooshe mambo” - Rais Mstaafu, Dr.Jakaya Kikwete Msibani Chato leo

"Alipojitokeza kuomba uteuzi wa kuwa mgombea wa Urais wa CCM mwaka 2015, sikusita kumpendekeza katika majina matano niliyoyafikisha kwenye kikao cha juu cha chama, sikuwa na tabu na Magufuli ndio jina la kwanza halafu yakafuata mengine”- Rais Mstaafu Dr. Kikwete

“Mheshimiwa Magufuli alinitunuku Kiwanja hapa Chato, kipindi akiwa Mbunge na Waziri, alipokuwa Rais akaongeza eneo, ilikuwa matarajio yangu kujenga nyumba, ili siku akistaafu tuendelee kupiga soga hapa Chato”- Dr.KikweteView attachment 1734957
Rest in Power Magufuli
 
"Kila nilipopata fursa ya kutembelea hapa Chato nilipokuwa Waziri na hata Rais sikuacha kufika nyumbani hapa kumsalimia Mama yetu (Mama Mzazi wa JPM) niliketi nae kwenye mkeka tukazungumza ya Mama na Mwanae (iko picha moja maarufu Mtandaoni) nimekaa na Mama na Hayati”-Rais Mstaafu Dr. Jakaya Kikwete Msibani leo
20210326_160252.jpg
 
“Vyombo vya Ulinzi na Usalama vinapenda kukuhakishia kuwa ulinzi wa Nchi na mipaka yake ni salama na kwamba vitaendelea kukulinda Rais Samia, kukutii kama Amiri Jeshi Mkuu na kutekeleza majukumu yake kama ilivyoainishwa katika Katiba” -Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo

“Vyombo vya Ulinzi na Usalama vinakuhakikishia utiifu, uadilifu na uaminifu mkubwa kwako Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu kama ilivyo mila na desturi kwa Majeshi yetu katika awamu zote zilizopita za Uongozi wa Nchi yetu” - CDF, Jenerali Venance Mabeyo

“Tangu aingie madarakani mwaka 2015 Dkt John Pombe Magufuli kwanza alionyesha kuviamini na kuvipenda vyombo vya ulinzi kwa dhati kubwa, alihakikisha anaviwezesha kwa mahitaji ya kiutendaji na mahitaji ya kiutawala” - CDF Jenerali Venance Mabeyo
20210326_160356.jpg
 
“Waswahili wanasema akutukane hakuchagulii tusi unaposikia minong’ono kwamba unasikia Kikwete hakumtaka Magufuli, labda Kikwete mwingine, nimewasimulia leo mchakato tulivyokwenda na yale majina matano nilikuja nayo Mimi na la kwanza lilibaki kuwa la JPM nililoliweka mie“-Rais Mstaafu wa Tanzania, Dr. Jakaya Kikwete

“Oooh! Kikwete anamchukia Magufuli, eeh labda mwingine sio Mimi, unamchukiaje Mtu uliyemkabidhi Ilani ya uchaguzi na ameitekeleza kwa kiwango cha juu sana lakini nikasema Duniani waganga njaa wengi wanapata ulaji wao kwa kuongopa”- Rais Mstaafu Dr.Kikwete

“Sisi Marais wastaafu kumzika Hayati Magufuli, ni jambo ambalo sikulifikiria kabisa, nilitamani akamilishe kazi yake nzuri aliyoianza na atuzike sisi Kaka zake, ambao ni Marais tuliomtangulia”- Rais Mstaafu Dr. Jakaya Kikwete

“Ilikuwa nikutane na Hayati Magufuli March 02 alipokuwa ziarani DSM, alikuwa anikabidhi nyumba aliyonijengea, haikuwezekana kutokana na majukumu, natamani ningerudisha muda nipate picha naye ya mwisho”-Rais Mstaafu Dr. Jakaya Kikwete.
20210326_160535.jpg
 
“Rais Samia hatua zako ni nzuri sana, umetufariji Watanzania, umetufuta machozi na muhimu zaidi umetuhakikishia kuwa Nchi ipo katika mikono salama na hakuna litakalo haribika, binafsi sina shaka na uongozi wako kwani nakufahamu kwa muda mrefu”- Rais Mstaafu Dr. Kikwete

“Baada ya matatizo ya Zanzibar Rais Mkapa aliunda timu niliyoiongoza Mimi, alikuwepo Dkt. Shein alikuwepo na Samia, nimekufahamu zaidi Rais Samia ulipokuja kuwa Waziri wangu katika Serikali, ulisaidia kuimarisha Muungano kwa kushughulikia kero za Muungano”- Rais Mstaafu Dr. Kikwete

“Nchi yetu iko katika mikono salama, na hakuna litakaloharibika, binafsi sina shaka na uongozi wa Rais Samia
Wewe ni mbobevu kabisa, Mimi na wenzangu tutakuwa pamoja na wewe, tutume tutaitika, usipotutuma tutaendelea na shughuli zetu”- Rais Mstaafu Dr.Jakaya Kikwete
20210326_162606.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom