Makapuku Forum

Makapuku Forum

Najidediketia wimbo huu na ballad hii;
Makaburi hayajajaa na yatuita watu, kama yalivyokuita ndugu yangu.
Maisha yanaendelea na siku zote nitakukumbuka maana ulibaki peke yako,
ulituongoza japo kitandani hukuweza kuamka,
tabasamu liliwaka, kila uliponiona.
Uliposikia jina langu ulifurahi na kuonesha meno yako.
hukuwa na pengo.
Pumzika na ni ngumu kusema kwa heri jana.
Hukulipenda giza, kaburini tutakuwekea taa, usiogope,
utamkuta baba (kaka yako) na utamkuta bibi wanakusubiri.
Tunakurudisha kijijini, sio kwamba tunaogopa jinamizi,
tunataka ukafurahie tulipotokea, utakuwa na bibi.
Umeivuta 82, mimi hata nusu sijaikaribia.
Tutakukumbuka wote, mjukuu wako kafunga shule,
atasikia masimulizi, anapenda kusoma,
ataona picha ana macho ya malaika,
hutasikia sauti yake, ila nakuambia tu ana sauti yako na
tutakukumbuka sana.
Pumzika maana siwezi kusema kwaheri jana.
Oh, nimeandika haya, niko njiani, nimefunga mkanda,
unajua ninapenda kuandika na hii itakuwa ni barua yangu ya mwisho.
sikuandikii usome wewe,
namuandikia mjukuu wako ambaye naamini hajabeba miguu yako 😀 na nimeweka hapa ili maandishi haya yaishi
maana yana jina langu


 
Najidediketia wimbo huu na ballad hii;
Makaburi hayajajaa na yatuita watu, kama yalivyokuita ndugu yangu.
Maisha yanaendelea na siku zote nitakukumbuka maana ulibaki peke yako,
ulituongoza japo kitandani hukuweza kuamka,
tabasamu liliwaka, kila uliponiona.
Uliposikia jina langu ulifurahi na kuonesha meno yako.
hukuwa na pengo.
Pumzika na ni ngumu kusema kwa heri jana.
Hukulipenda giza, kaburini tutakuwekea taa, usiogope,
utamkuta baba (kaka yako) na utamkuta bibi wanakusubiri.
Tunakurudisha kijijini, sio kwamba tunaogopa jinamizi,
tunataka ukafurahie tulipotokea, utakuwa na bibi.
Umeivuta 82, mimi hata nusu sijaikaribia.
Tutakukumbuka wote, mjukuu wako kafunga shule,
atasikia masimulizi, anapenda kusoma,
ataona picha ana macho ya malaika,
hutasikia sauti yake, ila nakuambia tu ana sauti yako na
tutakukumbuka sana.
Pumzika maana siwezi kusema kwaheri jana.
Oh, nimeandika haya, niko njiani, nimefunga mkanda,
unajua ninapenda kuandika na hii itakuwa ni barua yangu ya mwisho.
sikuandikii usome wewe,
namuandikia mjukuu wako ambaye naamini hajabeba miguu yako 😀 na nimeweka hapa ili maandishi haya yaishi
maana yana jina langu


@Obe kwema ndugu,?
Haya maneno kukutana nayo asubuhi hii hata km hukuswali,, lzm urudi ndani ukamumbe Muumba kwanza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom