Makapuku Forum

Makapuku Forum

Badili mtazamo, hamisha nguvu na akili hiyo hiyo unayoitumia kwenye mambo ya ovyo yanayochochea MATUMIZI, Ipeleke nguvu hiyo kwenye mambo ya msingi yanayochochea UZALISHAJI. Change attitude. Nguvu unayoitumia kumshawishi mtu usiyemjua ili akukubalie kimahusiano, itumie nguvu hiyo hiyo, jitihada hizo hizo kutafuta na kuwashawishi wateja wanunue bidhaa yako na wanunue kwako siku zote wasikuache. Muda unaoutumia kuchati na wapenzi mitandaoni mara kwa Mara, utumie muda huo ku-close deal na wateja wako wa mtandaoni ili uzalishe pesa.Nguvu unayoitumia kubembeleza Mwenza asikuache tumia nguvu hiyo kuwabembeleza wateja wasiache kununua kwako. Your lifestyle is a full package of business requirements
 
Yes, mtaji hauna hata muda pia hauna?. Uza muda upate mtaji wa kuanzia Biashara. Usiuze Muda milele, ifikie hatua uanze kutumia muda wako. Ili nawe ununue muda wa watu wengine wanaotafuta mtaji.
 
Tonge moja halishibishi hata kama likaongezwa ukubwa. Tonge la kumegewa halifanani na tonge la kumega mwenyewe kwani unamega size ya tonge kulingana na njaa yako ilivyo, ukiongeza speed ya kula matonge zaidi ya moja hata kama madogo madogo automatically tumbo litashiba.Bahari haijazwi na mto mmoja hata Kama huo mto unaingiza maji mengi kiasi gan. Usitafute chuma ulete anayekuibia Ongeza mfereji uone zinakoelekea.
 
Haijalishi unajichukulia Poa kiasi gani amini kuna watu wanajifunza kupitia wewe, japo hawajakuambia. Ukikata tamaa,unapolalamika ugumu wa maisha kila Mara unawavunja moyo, automatically. Pambanaa,,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom